Msaada ugonjwa wa Mutlinodular Goitre R/O Malignancy

Loeli

JF-Expert Member
Jan 26, 2014
997
763
Kwenu JF Doctors,
Kuna ndugu yangu wa kike amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya ambayo alionekana kama stress, anxiety, depression ,high pulse rate, fluctuating pressure, short memory/low memory, poor concentration, fluctuating menstrual cycles, etc. Tatizo lilianza toka 2014 na alifanyiwa vipimo akaonekana hana tatizo kwa vingi vyake. Baadaye Dr. aliyekuwa anahudhuria kwake akamuunganisha kwa Neurophycician ambako kule alikutana na issues za Peripheral nerves na akapewa dawa za kuzibua mishipa na hapo pressure ikanza kuondoka hivyo akapewa dawa pia kwa ajili ya ku boost memory.

Hata hivyo kadri siku zinaenda zile symptoms hapo ju zikawa hazikomi hivyo akaenda tena kwa Dr Mwingine ambaye yeye alipima Hormones akatutwa kuwa T3 ziko Juu na T4 ziko normal ila TSH zikawa ziko low sana. Ila pia akaandikiwa kipimo cha Cortisol AM na PM vyote vikawa viko low yaani havikuwa sawa kabisa vyote. Ndipo Dr akaamwandikia akafanye ultrasound ya Thyroid Gland. Alitumia High Resolution Ultrasound of Neck (Thyroid) na Majibu yakawa kama ifuatavyo:

Both lobes were normal in size with normal homogeneous parenchymal echo-pattern. Normal blood flow on colour Doppler interrogation. No focal nodule, cyst (or) abnormal calcification. But the following were observed:

1. Right Lobe measures 3.8X1.6X1.7cm - Heterogeneous mass predominantly cystic with no vascularity measuring 1.5X0.8cm

2. Left Lobe measuring 3.8X1.9X1.1 - multiple heterogeneous masses with the largest measuring 1.9X1.1 cm with increased vascularity.

Conclusion:
Features are suggestive of : Multi-nodular Goiter
R/o malignancy


Suggestion: Clinical correlation and + Biopsy.


Aliporudhisha majibu kwa Dr akaambiwa akafanye kipimo cha Thyroid Fine-Needle Aspiration Cytology (FNAC). Hapa akaogopa mno kwa sababu baada ya kusoma mitandaoni anaona kama inaweza kuwa ana Thyroid Cancer. Yaani amepatwa na kiwewe kiasi kwamba anaogopa kwenda kufanya hicho kipimo maana watu left right and centre wanamwambia kama ni cancer akishaitoboa ni matatizo zaidi. Basi ndugu hapa hatuna amani kabisa na kila akishauriwa ni kulia tu maana pia ana watoto ambao hawajajitegemea kabisa na ni mjane.

Ninaomba tu madaktari na wana JF ambao wameshakutana na tatizo kama lake wanipe ushauri kama kweli hicho kipimo cha fine needle wakitoboa hakiweze eneza kama itakuwa ni cancer. Ukweli hata mimi nimeogopa kidogo japo ni kama nimehamia nyumbani kwake kila wakati kwenda kumpa moyo. Karatasi ya kipimo anayo ila hataki kabisa kwenda kufanya kipimo. Ameanza kunywa mitishamba na natural therapy za Goitre huko U tube tu na kusali tu na kulia.

Please hebu tupeni msaasa wa mawazo.

Shukrani sana.
 
Hicho kipimo ni for Confirmatory purpose ili kujua kama shida ni Cancer au la.

Mpaka wanaamua kuandika kipimo hicho,hata kama ni Cancer itakuwa ipo kwenye hatua za awali na haijaanza kusambaa sehemu mbalimbali mwilini,hivyo kwake ni salama.

Ushauri wangu ni muhimu zaidi kufanya hicho kipimo ili kuweza kutoa tiba kulingana na hali ya mgonjwa.
 
Hicho kipimo ni for Confirmatory purpose ili kujua kama shida ni Cancer au la.

Mpaka wanaamua kuandika kipimo hicho,hata kama ni Cancer itakuwa ipo kwenye hatua za awali na haijaanza kusambaa sehemu mbalimbali mwilini,hivyo kwake ni salama.

Ushauri wangu ni muhimu zaidi kufanya hicho kipimo ili kuweza kutoa tiba kulingana na hali ya mgonjwa.
Barikiwa sana sana mkuu. Ukweli majibu yote nitampa asome. Hata mimi nilimwambia kuwa hatakuwa na tatizo kwa kuwa amegundua mapema. Pia mpaka sasa haumwi lolote zaidi ya hizo sign za low/high thyroid. Bado ninakaribisha utaalam na uzoefu wanandugu wa JF.
 
Wakuu ninasubiri wataalam msaidie japo mawili matatu kuhusu hicho kipimi cha FNAC je kama ni cancer hakiwezi kusambaza zaidi akichomwa? Ninajua kuna natural herbs ambazo zinatibu kabisa cancer early stages ambayo haijaguswa kwa kutobolewa. Tatizo ni je dalili hizi na majibu hayo inaweza suggest cancer at early stage? Wataalam please need your help.
 
Wakuu ninasubiri wataalam msaidie japo mawili matatu kuhusu hicho kipimi cha FNAC je kama ni cancer hakiwezi kusambaza zaidi akichomwa? Ninajua kuna natural herbs ambazo zinatibu kabisa cancer early stages ambayo haijaguswa kwa kutobolewa. Tatizo ni je dalili hizi na majibu hayo inaweza suggest cancer at early stage? Wataalam please need your help.
Kipimo sahihi kwa kuthibitisha Cancer n mpka afanyiwe icho kipimo, ww mshauri apunguze hofu na akapime hcho kipimo kwa mustakabali wa afya yake.na hcho kipimo cha FNAC hakisambazi cancer maana wanachukua hyo tissue iliyokua suspected kuwa na na abdnormality then wanaingalia kwa ukaribu zaidi au kwa kutumia chemicals maalumu kutambua hyo abnormality n ya aina gan

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kipimo sahihi kwa kuthibitisha Cancer n mpka afanyiwe icho kipimo, ww mshauri apunguze hofu na akapime hcho kipimo kwa mustakabali wa afya yake.na hcho kipimo cha FNAC hakisambazi cancer maana wanachukua hyo tissue iliyokua suspected kuwa na na abdnormality then wanaingalia kwa ukaribu zaidi au kwa kutumia chemicals maalumu kutambua hyo abnormality n ya aina gan

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukrani Mkuu kwa ushauri wa kitaalam.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom