SALOK
JF-Expert Member
- Sep 20, 2011
- 3,318
- 1,936
Habari wakuu...!!!
Heshima kwenu nyote, wadau na wapenzi wa jukwaa hili na JF's members wote kwa ujumla!!
Shukrani za dhati na za kipekee kwa wale wote wenye moyo wa kujitolea maarifa, ushauri, nasaha na kutiana moyo wa pole kutokana na matatizo/magonjwa ambayo huletwa humu. Ahsanteni sana endeleeni na mioyo hiyo hiyo ya kusaidia wengine
Ndugu zangu, leo hii naomba niwashirikishe tatizo nililonalo ikiwa ni ktk jitihada za kutafuta ufumbuzi.
Ndugu zangu katika siku za hivi karibuni nimepatwa na tatizo la ngozi, katika sehemu za kwapa la kulia kuna hali ya ngozi kubabuka ambapo sehemu zenye tatizo ngozi imekuwa nyeusi hali hiyo inaenda sambamba na muwasho pamoja na maumivu, muwasho unaoelekea kuwa katika hali ya utamu utamu hivi tatizo lilianzia shingoni upande wa nyuma ya shingo kulia, ikaja upande wa nyuma kushoto.
Hali hii ya mabaka kama haya iliwahi kunitokea wakati niko mdogo sana, nakumbuka bibi alisumbuka sana kunitibu kwa dawa za miti na majani tatizo lilikuja kunitokea tena kama miaka 12 iliyopita, lakini halikudumu sasa hivi limekuja kuibukia tena shingoni na kwapani.
Kinachonipa shaka ni je inawezekana ikawa ni dalili ya ukoma, je ukoma ni ktk magonjwa yanayorithishana?? Mama yake bibi mzaa baba na babu mzaa baba wote waliwahi kuugua ugonjwa wa ukoma.
Natanguliza shukrani za dhati
Picha nitazipandisha....
Muathiriko kwapani...
Hapo shingoni...
Heshima kwenu nyote, wadau na wapenzi wa jukwaa hili na JF's members wote kwa ujumla!!
Shukrani za dhati na za kipekee kwa wale wote wenye moyo wa kujitolea maarifa, ushauri, nasaha na kutiana moyo wa pole kutokana na matatizo/magonjwa ambayo huletwa humu. Ahsanteni sana endeleeni na mioyo hiyo hiyo ya kusaidia wengine
Ndugu zangu, leo hii naomba niwashirikishe tatizo nililonalo ikiwa ni ktk jitihada za kutafuta ufumbuzi.
Ndugu zangu katika siku za hivi karibuni nimepatwa na tatizo la ngozi, katika sehemu za kwapa la kulia kuna hali ya ngozi kubabuka ambapo sehemu zenye tatizo ngozi imekuwa nyeusi hali hiyo inaenda sambamba na muwasho pamoja na maumivu, muwasho unaoelekea kuwa katika hali ya utamu utamu hivi tatizo lilianzia shingoni upande wa nyuma ya shingo kulia, ikaja upande wa nyuma kushoto.
Hali hii ya mabaka kama haya iliwahi kunitokea wakati niko mdogo sana, nakumbuka bibi alisumbuka sana kunitibu kwa dawa za miti na majani tatizo lilikuja kunitokea tena kama miaka 12 iliyopita, lakini halikudumu sasa hivi limekuja kuibukia tena shingoni na kwapani.
Kinachonipa shaka ni je inawezekana ikawa ni dalili ya ukoma, je ukoma ni ktk magonjwa yanayorithishana?? Mama yake bibi mzaa baba na babu mzaa baba wote waliwahi kuugua ugonjwa wa ukoma.
Natanguliza shukrani za dhati
Picha nitazipandisha....
Muathiriko kwapani...
Hapo shingoni...