Nina gari nilinunua kwa mtu miaka mitano iliyopita. Muda wote huo nilikuwa sijabadili kutoka jina la muuzaji kwenda jina langu. Hivi juzi rafiki yangu kaniambia kwamba nikienda tu kubadili jina kuna faini hutozwa kwa kila mwezi niliochelewa tokea pale niliponunua hadi leo. Jamani mwenye ufahamu wa hilo msaada tafadhali.