Faith
Member
- Jul 9, 2008
- 52
- 11
BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA NA WADAU KUHUSU TATIZO HILI
Je, hii husababishwa na nini? Naweza kumsaidiaje mwanangu aache kukoroma alalapo, maana hata kama ameanza kukoroma nikamstua/kumtingisha na kumlaza vizuri akilala hukoloma tena.
Iila, pia ninae sista wangu nae ni mkoromaji sana tu, je inawezekana amerithi ama? Naye huyu nitamsaidiaje japo ameshakua mtu mzima?
Msaada wenu wana JF unahitajika!
---
---Wapendwa hope doing great,
Nahisi hili tatizo wengi tunao lakini kwa baadhi yetu it's too much unakuata watu mmelala lakini mwenzenu anakoroma kama trekta au mashine ya kupasua mbao.
Baadhi ukiwageuza wanaacha lakini kwa wengi hakuna kruuuuuuu......krooooooooo..krrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr krrooookruruuuukokookoo....yaani sijui nieleze vipi majirani hawalali kabisa. Sasa wadau tuelimishane,
Kukoroma inasababishwa na nini?
Dawa yake ni ipi?
Je, kuna baadhi ya vyakula/shughuli/dawa au mazingira yanayochangia tatizo hili?
Kuna namna yeyote ya kuepuka/kupunguza tatizo hili?
Thank you kwa ushauri wenu wan JF GREAT PLATFORM!!!1
Wakuu habari ya siku nyingi!!
Wakuu nina mdogo wangu yaani ana hilo tatizo hapo juu mpaka natamani kutengeneza bit za mziki kwani akiweka kichwa tu kitandani hapohapo anaanza na base yaani hata ukimshitua anatulia mara anarudia tena.
Wakuu naomba kama kuna mtu yeyote anayejua dawa la hii tatizo anijuze nimsaidie ndugu yangu asije kimbiwa na mchuchu wake kwa makelele hayo.
UFAFANUZI WA JUMLA WA TATIZO HILI
Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wakati wanapolala ambalo linaweza kuwatokea watu wa kila umri ingawa hutokea mara nyingi kwa wanaume au watu wanene. Kukoroma huzidi kwa kadri umri unavyoongezeka na
asilimia 54 ya watu wazima hukoroma baadhi ya wakati huku asilimia 25 ya wengine wakiwa na tabia ya kukoroma kila wakati. Kukoroma baadhi ya wakati kwa kawaida sio tatizo kubwa na mara nyingi huleta tu karaha
kwa mtu anayelala karibu na mkoromaji. Hata hivyo kukoroma huko sio tu kwamba huharibu usingizi wa anayekoroma bali pia huwasumbua na kuwakeresha wanaolala karibu na mkoromaji. Wale wenye tabia ya
kukoroma, hukoroma kila wanapolala na mara nyingi huchoka wanapoamka, na watu wa aina hii hushauriwa kumuona daktari na kushauriwa kuhusiana na tatizo hilo. Lakini kabla hatujaendela mbele ni bora tujue kukoroma hasa ni nini au hutokea vipi?
Mtu huwa anakoroma pale kunapokuwa na kitu au sababu yoyote itakayoziba kuingia au kutoka kwa hewa mdomoni na katika pua. Kuta za koo hutikisika wakati wa kupumua na matokeo yake ni sauti inayosikika ya kukoroma. Kuingia au kutoka kwa hewa huweza kuzuiwa na sababu mbalimbali kama vile:
Kuziba tundu za pua kusiko kamili ambako husababisha nguvu zaidi zitumike katika kupitisha hewa kwenye pua wakati mtu akiwa amelala. Kitendo hicho hupelekea nyama laini za pua na koo zijikusanye na kusababisha mkoromo. Kuna baadhi ya watu wanakoroma tu kipindi cha allergy (allergy season) au wanapatwa na matatizo ya sinus.
Baadhi ya matatizo kama vile kupinda pua (deviated septum) au ukuta unaotenganisha tundu za pua na polyps za pua pia huweza kufanya pua zizibe na kusababisha kukoroma. Watu wengi wanaofanya operesheni za pua pia hupatwa na tatizo la kukoroma.
Kuwa na misuli dhaifu katika koo na ulimi. Misuli au nyama za koo na ulimi zinapokuwa dhaifu sana hulegea na kuanguka upande wa nyuma wa sehemu inayopita hewa. Suala hilo hutokea pale mtu anapolala fofofo au kuwa na usingizi mzito na kusababisha kukoroma.
Kuwa na misuli minene ya koo. Hii ni kwa wale watu wanene ambao hata nyama zao za koo pia hunenepa na kupanuka na suala hilo husababisha kukoroma, Pia watoto wenye tonsesi kubwa na adenoids baadhi ya wakati hukoroma.
Kuwa na kilimi kikubwa ni mojawapo ya sababu zinazosababisha kukoroma. Kilimi kirefu kinaweza kuzuia koo na pale kinapotikisika wakati hewa inapita kwa msukumo husababisha kukoroma.
Sababu nyinginezo zinazoweza kumsababishia mtu akorome anapolala ni kuwa na umri mkubwa au uzee, imeshuhudiwa kuwa watu wa makamo na wazee hukoroma, kwani misuli na nyama za koo huanza kuzeeka na kulegea kadri umri unayoongezeka. Vilevile wanaume wanakoroma zaidi kuliko wanawake hii ni kutokana na wanaume kuwa na njia nyembamba zaidi ya hewa kuliko wanawake. Kukoroma pia kunaweza kuwa ni tatizo la kurithi.
Pombe, kuvuta sigara na matumizi ya baadhi ya dawa pia husababisha misuli ya koo ilegee na hivyo hupelekea mtu akorome. Kulala vibaya pia husababisha kukoroka kama vile kulala kichalichali, kwani hufanya nyama za koo zilegee na kuziba hewa.
Je, Dawa ya kukoroma ni nini?
Swali hilo limeuliwa sana na mimi katika kulijibu ningependa kusema kuwa, kujua sababu inayosababisha mtu akorome na kuitatua au kuiondoa sababu hiyo ndiko kunakotibu kukoroma. Sote tunajua adha inayotokana na
kukoroma, na sauti hiyo inavyosumbua hasa iwapo anayekoroma ni mtu wako wa karibu kama vile mumeo, mwenzi wako au yoyote yule inayekubidi ulale naye karibu au katika kitanda kimojana hata chumba kimoja. Kukoroma pia huathiri usingizi wa mkoromaji kwani anayekoroka humbidi aamke mara kadhaa usingizini akijua au
bila kujua kutokana njia zake za hewa kufunga kwa sekunde kadhaa ambapo usingizi pia hukatika. Wanaokoroma pia hushindwa kulala vizuri suala linalopelekea asubuhi wawe wamechoka na kutofanya majukumu yao vyema, na pia wale wanaolala nao karibu hupatwa na matatizo kama hayo. Vilevile tunapaswa kujua kuwa kukoroma kuna
athari za kiafya za muda mrefu kwa mtu anayekoroma hivyo si jambo la kufanyia mzaha na ni tatizo ambalo linapaswa kushughulikiwa na kutatuliwa.
Wataalamu wanatuambia kuwa ili kujua kukoroma kwako kunasababishwa na nini ni bora ushirikiane na mwenzi wako au yoyote unayelala naye ili akuchunguze pale unapolala na kujua jinsi mwili wako unavyokuwa pale unapokoroma. Ni bora aandae orodha na kuchunguza yafuatayo:
1. Kufunga mdomo na kukoroma kunaonyesha kuwa kuna matatizo ya ulimi.
2. Kufungua mdomo na kukoroma kunaonyesha unaweza kuwa na tatizo katika misuli au nyama za koo.
3. Kukoroma unapolala kichalichali kunaonyesha kuwa pengine kwa kubadilisha namna unavyolala kukoroma nako kunaweza kwisha.
4. Kukoroma wakati unapolala kwa kila mlalo kunaonyesha kwamba tatizo lako ni kubwa na pengine kunahitajia tiba kubwa zaidi.
Iwapo umebadilisha namna unavyolala na haikusaidia, unashauriwa ujaribu yafuatayo:
; Punguza uzito
; Safisha njia yako ya hewa. Kuwa na pua iliyoziba hufanya kupumua kuwe kugumu na kusababisha kukoroma. Unaweza kufanya hivyo kwa kutumia dawa za kusaidia kupumua kwa urahisi (nasal decongestants) zinazopatikana kwa urahisi katika maduka ya dawa.
; Wacha kuvuta sigara.
; Lala mapema na pata usingizi wa kutosha kila mara huku ukijiepusha na kuchoka sana. Kunyanyua kichwa kwa nchi 4 huweza kupunguza kasi ya kupumua na kusaidia ulimi na taya kwenda mbele hali ambayo hupunguza kukoroma. Fanya hilo kwa tumia mito maalum ya kupunguza kukoroma au lala bila mto.
Wataalamu pia wanasema kwamba unaweza kupunguza kukoroma kwa kutokula baadhi ya vyakula au dawa kabla ya kulala ambavyo huongeza kukoroma. Vitu hivyo ni kama vile
o Kutokula mlo mkubwa kabla ya kulala.
o Kutokula vyakula vinavyotokana na maziwa au maziwa ya soya.
o Kutokunywa pombe kabla ya kulala.
o Kutotumia dawa aina ya antihistamines.
o Kutotumia vyakula au vinjwaji venye kafeini.
Vilevile wanaokoroma wanashauriwa kufanya mazoezi ya koo ambayo ni pamoja na kuimba, kusoma kwa kurudia rudia voweli (a,e,i,o,u) kwa nguvu kwa dakika tatu mara kadhaa kwa siku, kuweka ncha ya ulimi chini ya meno ya mbele na kurudisha ulimi nyuma kwa dakika 3 kila siku au huku mdomo ukiwa wazi pelekea taya yako upande wa
kulia na wacha ibakie katika hali hiyo kwa sekunde 30. Huku mdomo ukiwa wazi, kaza misuli ya nyuma ya koo na rudia kitendo hicho kwa sekunde thelathini. Unaweza kutizama kwenye kioo na kuona jinsi kilimi kinavyokwenda juu na chini.
Iwapo kukoroma hakutoisha kwa kutumia njia hizo tofauti zilizoelezwa, usife moyo jaribu kumuona daktari na akupe ushauri wa kitiba kuhusiana na tatizo hilo. Madakatari wataalamu wa magonjwa ya pua, masikio na koo au ENT wanaweza kukusaidia zaidi kutatua tatizo hilo. Siku hizi kuna vifaa mbalimbali vinavyotumiwa mahospitalini ili kuondoa kukoroma kama vile kifaa kinachowekwa kwenye meno, CPAP, kidude kinachowekwa mdomoni au hata kufanyiwa operesheni ili kuondoa tatizo hilo.
Dawa ya kukoroma Fanya hivi: Fungua mdomo wako mpaka mwisho, toa ulimi na usukume nje mpaka mwisho,rudisha ulimi ndani mpaka mwisho-rudia mara 20. Ukimaliza utahisi kuna misuli nyuma
na pembeni ya koo umeifanyisha kazi,sasa misuli hii ikilegea ndio inayosababisha kukoroma. Fanya zoezi hili mara 2 mpaka 3 kwa siku na tatizo hili litaisha baada ya siku 10-20 kutegemea mtu hadi mtu.
BAADHI YA MICHANGO NA UFAFANUZI ULIOTOLEWA NA WADAUI
---Kwa wanaJF wa siku nyingi bila shaka watakumbuka kwamba kuna member mmoja aliwahi kuleta suala hili hapa akiomba msaada. Alipewa majibu kibao lakini alijitokeza member mmoja aliyeeeleza kwamba akiwa safarini siku moja na mchina, walifika mahali wakalazimika kutokuendelea na safari na kuamua kutafuta guest house ili walale pale. Kwa bahati mbaya kulikuwa na chumba kimoja double ambacho hawa wawili walilazimika kukishare. Huyu Bwana alisema alikuwa anakoroma SANA na kesho yake mchina alimwambia ni kipi cha kufanya ili aondokane na tatizo hilo. Juzi nilikutana na mtu eti anaenda kufanyiwa operation ili kutibu kukoroma. Nilimwambia hao wanataka pesa zake hawana chochote.
Dawa hii hapa: Fanya mazoezi ya kuachama na kuutoa ulimi nje kwa nguvu kama mara ishirini au 30 kwa siku. Zoezi hili linasaidia kuirelax mishipa ambayo ikigangamala, inasababisha mtu kukoroma. Nilikuwa na tatizo kama lako lakini tangia mdau alipotoa ushauri wake hapa, kukoroma kwangu sasa imekuwa ni ndoto na hata ndugu zangu walishangaa ni kitu gani kimetokea mpaka nikaacha kukoroma. Just give a try and come back with the results. I believe you will successed.
Tiba
---Watu wengi wana tabia ya kukoroma wanapolala, lakini kukoroma siyo kuzuri sana kwani familia yako pengine ishindwe kupata usingizi vizuri kutokana na makelele.
ulnayoyatengeneza na kwa upande mwingine, kukoroma kunamaanisha kuwa pumzi zako haziko sawa, hata baadhi ya wakati kukoroma kunaweza kusababisha kukosa pumzi na kupelekea kifo. Kwa hivyo, tuangalie tips kadhaa zinazoweza kubadilisha hali hiyo:
Kwanza ni kuchagua mito laini na inayoweza kufanya shingo yako iwe vizuri, ambayo itasaidia kupumua;
Pili ni kutumia mashine ya (humidifier) ili hewa ndani ya chumba iwe ya unyevu na kuepuka koo yako kuwa kavu;
Tatu, kunywa asali kidogo kulainisha koo yako na usinywe pombe kwani inapandisha shinikizo lako la damu na kuwa juu na kubana koo lako pamoja na kuzuia pumzi.
Nne, kama tunavyosema kila siku, fanya mazoezi mara kwa mara
---Si jambo geni kusikia mtu wako wa karibu au mwenza wako anapokuwa amelala kuwa na kawaida akikoroma au kuwa na mikwamo mikwamo ya milio isiyo ya kawaida akiwa katika usingizi mzito.Iwapo utamtikisa au kumgusa hali hiyo hupotea kwa sekunde kadhaa na kama atapata tena usingizi mlio huo hujirudia tena.
Wengi wamekuwa wakijiuliza ni kipi husababisha hali ya kukoroma na wengine wamelichukulia kuwa ni suala la kimaumbile kama vile unene lakini sababu hasa wamekuwa hawaijui lakini kwa upande wa afya linaweza kuwa ni kiashiria cha tatizo la kiafya mwilini.Tayari kuna tafiti za sayansi ya tiba zinaonyesha mahusiano makubwa ya magonjwa ya moyo na watu wanaokoroma au pingamizi la usingizi.Watu wenye pingamizi la usingizi hasa watu wazima wameonyesha kuwa na dalili za magonjwa ya moyo.
Pingamizi la usingizi ni nini?
Pingamizi la upumuaji usingizini ni hali ya kushindwa kupumua kwa kutumia pua au mdomo kwa muda wa sekunde kumi. Tatizo hili hutokea zaidi ya mara 30 katika hatua za vipindi viwili ambavyo kitaalamu hujulikana kama mjongeo wa kasi wa macho na mjongea wa kawaida wa macho.Mjongeo wa kasi wa macho wakati wa usingizi ni kipindi kimojawapo cha usingizi wa kawaida ambacho huambatana na macho kucheza cheza yaani mtu anakuwa yupo usingizini huku macho yake yakicheza cheza.Kwa kawaida wakati mtu amelala hupitia hatua hii mojawapo ya usingizi na hutokea mara nne hadi tano katika usingizi.
Hali hii huweza kutokea kwa muda mfupi na mwishowe kipindi hiki hukawia kwa muda mrefu hasa inapokaribia asubuhi.
Inakisiwa kuwa mjongeo wa kasi wa macho huchukua asilimia 20-25 ya usingizi wa mtu mzima yaani dakika 90-120 kwa ujumla.Katika hali ya mjongeo wa kawaida wa macho ni hatua ambayo mtu anakuwa amelala lakini hawezi kuchezesha macho, kuota ndoto ni nadra sana kwa wenye kupata hatua hii. Akili huwa katika hali njema kabisa viungo vya mwili wake kutolegea ndio maana mtu anaweza kutembea huku akiwa usingizini. (sleep walk)Tatizo la pingamizi la upumuaji usingizini huathiri zaidi wanaume kuliko wanawake.
Watu gani wako kwenye hatari ya tatizo hili?
Unene uliopitiliza
Shinikizo la damu (Hypertension)
Moyo kushindwa kufanya kazi vizuri (Congestive Cardiac Failure)
Matatizo katika mishipa ya damu ya moyo (Coronary Heart Disease)
Uchovu
&[HASHTAG]#8226[/HASHTAG]; Kuamka usiku kwenda kukojoa mara kwa mara
Vipimo Vya Uchunguzi
&[HASHTAG]#8226[/HASHTAG]; Polysomnogram-kipimo cha picha kina choonyesha hali ya tishu za njiani ya hewa (puani).
&[HASHTAG]#8226[/HASHTAG]; Actigraphy
Matibabu:
1. Muendelezo chanya wa shinikizo katika mfumo wa hewa
2. Matibabu ya matatizo yanayoweza kupelekea kupata tatizo hili mfano kupunguza uzito kwa wale wenye uzito uliopitiliza, kutibu shinikizo la damu, kupunguza unywaji wa pombe na uvutaji sigara.
Lakini zipo dawa ambazo zimezagaa mtaani zinazodaiwa kuponya ukoromaji hata hivyo hazijathibitishwa kumaliza tatizo hilo.
Jambo la muhimu ni kufuata hatua muhimu na kujua chanzo kinachokufanya ukorome hasa kwa kuwashirikisha unaolala nao.
Kwa mfano waweza kumwambia unayelala naye akuangalie wakati unaokoroma ni wakati gani na hivyo kujua chanzo. Hapo utajua kipi kinasababisha ukoromaji wako na namna ya kukomesha.Lakini kwa ujumla waweza kubadili aina ya kulala, kwa mfano kuacha kulala chali, penga kamasi kabla ya kulala, safisha chumba kabla ya kulala ili kuondoa hewa chafu inayoweza kusababisha vumbi na hatimaye mikoromo.
Chanzo: Mwananchi
---Angalizo!
Makala hii nimeinakili kutoka katika blogu ya ISSA MICHUZI, kwa hiyo mwanzilishi wa mada sio mimi.
Endelea.......
Habari za kazi mheshimiwa Michuzi,
nilipitia hapa kwenye blog yako nikakuta bwana Chumaka wa Korogwe akiomba msaada wa namna ya kutatua tatizo lake la kukoroma ambalo linamnyima mkewe usingizi.Majibu mengine niliyoyasoma yalikua ya ajabu na pia hayakuweza kumsaidia bwana Chumaka.
Na vifaa vingi vilivozungumzwa kwa mtu aliyopo Korogwe sidhani angevipata kwa urahisi. Kwakua kulikua na comments zaidi ya 35 nikahisi nikiweka na yangu pale wengi hawataiona,naomba uiweke peke yake ili iweze kusaidia watu kama mimi ilivyonisaidia.
Niliwahi kusafiri na mzee wa kijapani kwenda mikoani kikazi na katika safari zetu kuna siku ilibidi tulale kwenye mji mdogo ambao tulikosa vyumba na kupata kimoja tu ambacho kilikua na vitanda viwili.Watu wengi walishaniambia kuwa nakoroma sana nilalapo usiku.Siku ya pili tulipokua tunapata kifungua kinywa yule mzee akaniambia nina tatizo la kukoroma na atanifundisha namna ya kulitatua bila kutumia dawa,mbinu ambayo wanaitumia kwao.
Fungua mdomo wako mpaka mwisho, toa ulimi na usukume nje mpaka mwisho,rudisha ulimi ndani mpaka mwisho-rudia mara 20.
Ukimaliza utahisi kuna misuli nyuma na pembeni ya koo umeifanyisha kazi,sasa misuli hii ikilegea ndio inayosababisha kukoroma.Fanya zoezi hili mara 2 mpaka 3 kwa siku na tatizo hili litaisha baada ya siku 10-20 kutegemea mtu hadi mtu.
Mzee huyu aliniambia mtu anaekoroma mwili wake haupati mapumziko ya kutosha na mara nyingi huamka huku bado akihisi uchovu na husababisha watu wengine kunenepa sana na wengine kukonda ikitegemea mwili wa muhusika na homoni zake.
Tatizo langu liliisha kabisa baada ya wiki 2 lakini naendelea na mazoezi hata mara mbili kwa wiki ili misuli isilegee tena.Kwakua naishi peke yangu ilibidi nimchukue waifu wa siku 2-3 anihakikishie sikoromi kabisa.Nikiamka siku hizi sihisi uchovu ule wa zamani.
Mdau Ibrahim,D'salaam.
Chanzo: MICHUZI
---UHUSIANO WA KUKOROMA NA MAGONJWA YA MOYO
Si jambo geni kusikia mtu wako wa karibu au mwenza wako anapokuwa amelala kuwa na kawaida akikoroma au kuwa na mikwamo mikwamo ya milio isiyo ya kawaida akiwa katika usingizi mzito.
Iwapo utamtikisa au kumgusa hali hiyo hupotea kwa sekunde kadhaa na kama atapata tena usingizi mlio huo hujirudia tena.
Wengi wamekuwa wakijiuliza ni kipi husababisha hali ya kukoroma na wengine wamelichukulia kuwa ni suala la kimaumbile kama vile unene lakini sababu hasa wamekuwa hawaijui lakini kwa upande wa afya linaweza kuwa ni kiashiria cha tatizo la kiafya mwilini.
Tayari kuna tafiti za sayansi ya tiba zinaonyesha mahusiano makubwa ya magonjwa ya moyo na watu wanaokoroma au pingamizi la usingizi.
Watu wenye pingamizi la usingizi hasa watu wazima wameonyesha kuwa na dalili za magonjwa ya moyo.
Pingamizi la usingizi ni nini?
Pingamizi la upumuaji usingizini ni hali ya kushindwa kupumua kwa kutumia pua au mdomo kwa muda wa sekunde kumi.
Tatizo hili hutokea zaidi ya mara 30 katika hatua za vipindi viwili ambavyo kitaalamu hujulikana kama mjongeo wa kasi wa macho na mjongea wa kawaida wa macho.
Mjongeo wa kasi wa macho wakati wa usingizi ni kipindi kimojawapo cha usingizi wa kawaida ambacho huambatana na macho kucheza cheza yaani mtu anakuwa yupo usingizini huku macho yake yakicheza cheza.
Kwa kawaida wakati mtu amelala hupitia hatua hii mojawapo ya usingizi na hutokea mara nne hadi tano katika usingizi.
Hali hii huweza kutokea kwa muda mfupi na mwishowe kipindi hiki hukawia kwa muda mrefu hasa inapokaribia asubuhi. Inakisiwa kuwa mjongeo wa kasi wa macho huchukua asilimia 20-25 ya usingizi wa mtu mzima yaani dakika 90-120 kwa ujumla.
Katika hali ya mjongeo wa kawaida wa macho ni hatua ambayo mtu anakuwa amelala lakini hawezi kuchezesha macho, kuota ndoto ni nadra sana kwa wenye kupata hatua hii. Akili huwa katika hali njema kabisa viungo vya mwili wake kutolegea ndio maana mtu anaweza kutembea huku akiwa usingizini. (sleep walk)
---MBONA MKALI HIVYO,NADHANI NIMEJARIBU KUTENGEZA INITIAL CLUE TORWADS A SOLUTION,KUFUATANA NA JINSI SWALI LILIVYOULIZWA.WEWE UMESOMA BWANA,..NADHANI SIKU ZOTE HUWA UNAJIBU ULICHOULIZWA.
SABABU KWA UJUMLA
1.Physiologica;inaweza kuwa kawaida kama hakuambatani na maradhi au pindi hamna malalamiko toka kwa wenzi unao ishi nao,kama wenzio wana malalamiko ambayo yatageuka kuwa kero kwako binafsi,basi tayari huo ni ugonjwa na una matibabu yake.
2. Pathological process; mara nyingi ni matokeo ya ugonjwa/magonjwa ambayo hupelekea tendo la kukoroma,nayo hutofautiana kufuatana na umri.Hata watu wazima kuna wengine utakuta walikuwa hawana historia ya kukoroma,lakini GHAFLA ukubwani wanakumbwa na ugonjwa huo.[mfano ni baadhi ya wagonjwa wa ukimwi,ingawa sio wote,na sio lazima kuwa kila mwenye hali hiyo basi awe ni mgonjwa wa ukimwi lakini huonekana kwa (some HIV and someof the CANCER PATIENTS)]
3.Congenital;Huanza kuonekana pale tu baada ya kuzaliwa,kisababisho kinaweza kuwa ni URITHI[ hereditary]kutoka kwa waliomtangulia au kama sio urithi basi ni tokeo la hitilafu za kimuundo
zilizotokea kipindi cha uumbaji wa mtoto, wakati akiwa bado yupo tumboni mwa mama yake [fetal development]
4 Drug induced;Husababishwa na matumizi ya baadhi ya dawa,ambazo mbali na kutibu ugonjwa hutowa matokeo ambayo hayakutarajiwa medically known as adverse drug reactions [An unwanted effect caused by the administration of a drug] Hali hii huweza kutokea ghafla au taratibu.
5 Traumatic or corrosive injury;Ikitokea kwenye larynx au trachea huweza pia kusababisha.Unywaji wa sumu pindi watu wanapotaka kujiua ,sumu wavutayo wafanyakazi kwenye baadhi ya viwanda n.k. ambayo ina uwezo wa kusababisha kusinyaa kwa larynx au trachea[capable of causing their stenosis or narrowing]
6. Post thyroidectomy ;Hutokea baada ya kufanyiwa opration ya kuondoaTezi THYROID.Sababu moja wapo ni kuumizwa,au kukatwa kwa recurrent laryngeal nerve wakati wa kuiodoa hiyo tezi[thyroid]
SABABU ZIPO NYINGI MNO NA NDIO MAANA NIKAANZIA NA SUALA LA UMRI KWANZA,..ILI TUWEZE KUTOA USHAURI WA WAPI PA KUANZIA..KAMA NITAZUNGUMZIA YOYE HAYO juu ,NA KUTOA USHAURI WA TIBA NADHANI NITAKUA SIJAJIBU SWALI,NA WALA SITAELEWEKA.
SABABU KWA UJUMLA
1.Physiologica; inaweza kuwa kawaida kama hakuambatani na maradhi au pindi hamna malalamiko toka kwa wenzi unao ishi nao,kama wenzio wana malalamiko ambayo yatageuka kuwa kero kwako binafsi,basi tayari huo ni ugonjwa na una matibabu yake.
2. Pathological process; mara nyingi ni matokeo ya ugonjwa/magonjwa ambayo hupelekea tendo la kukoroma,nayo hutofautiana kufuatana na umri.Hata watu wazima kuna wengine utakuta walikuwa hawana historia ya kukoroma,lakini GHAFLA ukubwani wanakumbwa na ugonjwa huo.[mfano ni baadhi ya wagonjwa wa ukimwi,ingawa sio wote,na sio lazima kuwa kila mwenye hali hiyo basi awe ni mgonjwa wa ukimwi lakini huonekana kwa (some HIV and someof the CANCER PATIENTS)]
3.Congenital; Huanza kuonekana pale tu baada ya kuzaliwa,kisababisho kinaweza kuwa ni URITHI[ hereditary]kutoka kwa waliomtangulia au kama sio urithi basi ni tokeo la hitilafu za kimuundo
zilizotokea kipindi cha uumbaji wa mtoto, wakati akiwa bado yupo tumboni mwa mama yake [fetal development]
4 Drug induced; Husababishwa na matumizi ya baadhi ya dawa,ambazo mbali na kutibu ugonjwa hutowa matokeo ambayo hayakutarajiwa medically known as adverse drug reactions [An unwanted effect caused by the administration of a drug] Hali hii huweza kutokea ghafla au taratibu.
5 Traumatic or corrosive injury; Ikitokea kwenye larynx au trachea huweza pia kusababisha.Unywaji wa sumu pindi watu wanapotaka kujiua ,sumu wavutayo wafanyakazi kwenye baadhi ya viwanda n.k. ambayo ina uwezo wa kusababisha kusinyaa kwa larynx au trachea[capable of causing their stenosis or narrowing]
6.Post thyroidectomy; Hutokea baada ya kufanyiwa opration ya kuondoaTezi THYROID.Sababu moja wapo ni kuumizwa,au kukatwa kwa recurrent laryngeal nerve wakati wa kuiodoa hiyo tezi[thyroid]
SABABU ZIPO NYINGI MNO NA NDIO MAANA NIKAANZIA NA SUALA LA UMRI KWANZA,..ILI TUWEZE KUTOA USHAURI WA WAPI PA KUANZIA..KAMA NITAZUNGUMZIA YOYE HAYO juu ,NA KUTOA USHAURI WA TIBA NADHANI NITAKUA SIJAJIBU SWALI,NA WALA SITAELEWEKA.