Msaada tafadhali,binti kagundua mme mtarajiwa anaigiza ulokole, kumbe .......!

hujasema kama njemba ilifanikisha azma yake au lah, poor jane, hapo sijui kama atataka tena kusikia mchumba maana atajua ni wale waleeeeeeee! mijanaume mingine bwana, ni kazi kutuharibia sisi tulio waaminifu, hovyo sana
 
Inasikitisha .. Mwambie dada jenny ajaribu kuwa convince wazazi kwamba jamaa hafai.... pia mambo ya kulazimishana ndoa yameshapitwa na wakati..

Ni kweli kbs,but ndio tunatafuta namna ya kuwashawishi hao wazazi waelewe japo wakubali hata ndoa iairishwe huyu jamaa aulizwe!
 
Habari zenu wapendwa,,kuna binti flan nampa jina la Jen,huyu jen na familia yao yote ni walokole,jen elimu yake ni ya form four na ana miaka 20 kwa sasa,wazazi wake ni wakulima tu na wana elimu ya darasa la saba na yeye ndio mtoto wa kwanza ana wadogo zake wawili.

Mwezi wa pili mwaka huu alikutana na jamaa mmoja maeneo ya kibaha akiwa anatoka kanisani mida ya saa mbili usiku kwa vile mvua ilikuwa inanyesha yule jamaa akapaki gari na kumpa lifti ktk maongezi yao jamaa akasema ni mgen sehemu ile yeye anaishi dar ni mfanya biashara wakapeana contact alipofika anaposhuka karibu na kwao jamaa akamshusha na kuendelea na safari zake.

Basi tangu siku ile jen akaendelea kuwasiliana na jamaa na wakawa marafiki akamkaribisha kanisani kwao jamaa akawa anakuja mpaka naye akaokoka baada ya miezi km mitatu jamaa kwa vile alijiweka karibu na wazee wa kanisa na kuwa anatoa misaada na akawa anaheshimika pale kanisani basi akawajulisha wazee kuwa amempenda yule binti na anataka kumuoa kwani ameonna anamfaa,Basi wazee wakakubali na mipango ya uchumba ikaanza kwa taratibu za kilokole.

Katika harakati zote hizo aliwaleta baadhi ya ndugu wa binti na kuwatambulisha kwa watu aliodai ni dada zake maeneo ya magomen ambapo alisema anaishi nao wale ndugu pamoja na jen waliamini na akawa anaenda kuwatembelea mara chache na jamaa akampeleka kkoo kwenye kwenye duka la nguo ambalo alisema ndio ofic yake na yy ndio mmiliki so akaaminika na kila kitu kikaenda sawa.


Harusi imepangwa kufungwa jmosi ijayo,sas juzi jmosi jamaa akaenda kumchukua mchumba wake waje mjini kukamilisha kununua baadhi ya vitu amabvyo walikuwa hawajakamilisha kwa ajili ya harusi,kabla ya kwenda madukani akampeleka hotelin maeneo ya magomen jen hakuwa na wasiwasi akashangaa jamaa kachukua chumba na kumtaka waingie ana maongezi jen anasema alianza kupata hofu ila akaingia jamaa akaagiza vinywaji na vyakula na kuanza kuongea ambapo jamaa alimwambia jen anataka wafanye mapnz ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na itakuwa ni siri kati yao na kwa vile wameshapima afya na arusi ni wiki ijayo haina shida,jen akakataa basi jamaa wala hakulazimisha akamwomba anywe wine jen hajui wine na hajawahi kunywa akabembelezwa mpaka akanywa na akawa najisikia km kulala akajiegesha na jamaa akawa anachati kwenye komyuta na kunywa wine.

Jamaa akajua jen kalala kumbe hajalala na anaona na kusikia kila kitu hata jamaa alipokuwa anaongea na simu,basi kuna wakati jamaa akavua shati jeni akaona na kushangaa jamaa mwili mzima umejaa tatuu!basi akiwa anavua shati simu ya jamaa ikaita akawa anaongea na watu kuhusu biashara ila ktk maongezi akawa haelewi ni aina gani ya biashara na gafla jamaa akatoka kwenda kuongelea nje ya chumba jen akasogea mlangoni akasikia jamaa akimwambia huyo mtu kuwa karibia atatoka kwenye kifungo cha ulokole feki kwan arusi ni jmosi na akishaoa basi na ulokole ndio mwisho.

Jen aliposikia hivyo akachanganyikiwa na zile tatuu ndio zikammaliza kbs,na kurudi kitandani jamaa aliporudi jen akamwambia anajisikia kuumwa anaomba waondoke jamaa akakaataa ila jen alipoanza kulia jamaa akakubali na wakarudi kibaha hawakwenda madukani tena,alipofika kwao akawaambia wazazi na ndugu zake hakuna aliyeamini na wote wanamtetea jamaa,na wanachofanya ni kumwombea jen wasema kaingiwa na pepo,badala ya kutafakari na kutafuta suluhisho la tataizo.

Jana jen akaja kwa rafiki yake ambaye ni jiran yangu akamsimulia huo mkasa,wakaamua kwenda kule magomen kwa wale wifi zake ikabidi awaeleze lile tatizo wale wadada wakaingiwa na huruma wakamwabia ukweli kuwa yule wala sio ndugu yao ni rafiki wa kaka yao anayeishi nje ya nchi na anatumia chumba cha kaka yao na nimuuza unga hata hilo duka analosema ndio oficn kwake ni uongo na walishindwa kumwambia mapema coz hakutaka kuwa karibu nao na walionekana wanapendana na wakamwomba vyovyote atakavyoamua asiwataje kwan atawagombanisha mpaka kwa kaka yao ambae ndio km mzazi wao ndio anawalea hapa mjin!

Hapo ndio jen akachanganyikiwa,wakaamua kwenda na kule kkoo bahati mbaya wakakuta duka limefungwa kumbe hawaji kazin cku za jpili.mpaka hapo anawasiliana na mchumba vizuri tu bila kumjulisha wala kuonyesha tofauti yoyote,jana jion wakautana na jamaa maeneo ya ubungo akamrudisha kibaha,usiku ameongea na wazazi na baadhi ya ndugu hakuna anayemuelewa wanamuona muongo na wanamtetea jamaa,mpaka wazazi wakaanzisha maombi wanamwombea jen eti kaingiwa na pepo na wamemkataza asiondoke hm tena mpaka siku ya arusi.

Leo asubuhi imebidi nimpigie jiran yangu anambie kinachoendelea akanambia jen kampigia analia amechanganyikiwa na hamtaki tena huyo bwana,wazazi hawamwelewi kinachofanyika ni maombi tu na jamaa kwa vile ana pesa kawashika wazazi vizuri wanamkubalia kila analosema huyo jamaa yani wanamthamini kuliko hata jen,na baba kasema lzm ndoa ifungwe,sasa jen anahitaji msaada wa mawazo afanyeje yy hataki kuolewa tena baada ya kugundua jamaa ni tapeli tu,na wazazi wanataka aolewe,nyumbani haruhusiwi tena kutoka sasa hajui la kufanya amechanganyikiwa jirani yangu ameiomba tushirikiane namna ya kumsaidia jen hata kimawazo nami nimeamua kuwaletea wana jamii tunaomba mawazo yenu kwan jen anasema ni bora afe kuliko kuolewa na huyo mtu,wazazi hawajali wanafanya maombi tu na wanataka aolewe.
Nawasilisha.

Kinachotakiwa hapo ni watu kama ww ambao tayari wanajua kinachoendelea kutoa taarifa kwenye uongozi wa mtaa kwani hiyo ni kama kulazimisha ndoa isiyo ya ridhaa ya upande mmoja yaan wa JENI, yaan CANTALISIA ww kama kweli umeingiwa na huruma juu ya kinachoendelea fanya ivyo ukishirikiana na wale mawifi wa JENI kwani hata kaka yao atawaelewa tu,mbona mtakuwa Heroes Kwa JENI na kwangu pia
 
Toeni ripoti kwa mamlaka husika kuhusu jamaa kama kweli ni muuza unga na atafatiliwa tu. Pili huyo binti amkatae altareni kama hakuna njia mbadala maana akisema I DONT badala ya I DO inaweza kusaidia mambo yasiendelee mbele.
 
Huyo binti anatakiwa atoroshwe-then aje aonekane baada ya tarehe ya harusi kupita-hao wazazi wake akiwaendekeza atakuja kujuta maisha yake yote,
MSAIDIE KWA KUMTOROSHA
 
Najua kinachpaswa kufanyika hapo ni mgogoro huu kuingiliwa na mtu wa tatu (3rd party) nje ya familia.Jeni aseme anahitaji kuongea na mchungaji angalau na wazee wa kanisa wenye kuheshimika sana ktk kanisa hilo.Atoe ukweli wake.Tena kama mwana JF mmoja alivyosema kwamba ni risk kwa kuyasema hayo, ila mungu aliyemfunulia maono hatomwacha kabisa atamwonesha njia.Mie ndhani kwa vile wazazi ni walokole na kwa vile wanamwombea akimtaka mchungaji wazazi watamsikiliza.
 
Utamwua Bwana arusi mtarajiwa kwa BP. Sio ushauri mzuri huo, hebu fikiria kukataliwa hadaharini mbele ya wazazi, ndugu, jamaa na marafiki. Unaweza anguka chini. Tena hapo watu watamwona Jen kama hakutumia akili, watauliza kwa ni asubiri hadi kanisani.

binafsi naona ushauri wangu ni mzuri kabisa..
Hatoki ndai kafugiwa , hawezi kuongea na wazazi wake
wakamwelewa, ni analazimishwa kuolewa na mtu ambaye
hampendi khaaaaa. kilichobakia ni yeye kuwa mkweli na nafsi yake..

binafsi nadhani afanye awezalo kutoka kwenye hili balaa..
na muda mbae kila mtu atakuwa anamsikiliza ni pale akiwa
kanisani wakati wa "I DO" aseme tu ukweli au asema hataki
kuolewa....
 
Inasikitisha .. Mwambie dada jenny ajaribu kuwa convince wazazi kwamba jamaa hafai.... pia mambo ya kulazimishana ndoa yameshapitwa na wakati..
Hicho ndio tunachoomba kwan wazazi mpaka jana jion bado wamekomaa wanadai kuwa watu wanawaonea wivu ndio maana wanamjaza mtoto wao maneno ya uongo ili asiolewe!
 
ndoa hailazimishwi hata siku moja. hakuna kufunga wala kuomba, kwani Mungu ameshaweka wazi kila kitu. Jeny aache kuwasiliana na huyu jamaa amkane kwa uwazi. hao wanaoendelea kumwombea jeni waendelee na maombi yao. siku ifkifika hawatamlazimisha kufanya agano la ndoa na huyo mjamaa.

onyo kwa Dada zetu:
msikubali lift ovyo na hata kuzoewa ovyo. mvua haiui, siku ile angenyeshewa tu hakuna tatizo kuliko hii njia panda aliyoingia sasa. wewe mtu humjui anakwambia upande gari yake wewe unapanda, hivi inawezekanaje?. Ashukuru amemvutia pumzi maana siku ileile angesha.... hata hii ya kubadilsihana contact na mtu humjui, ya nini? ivi duniani hapa watu unaowafahamu ni wachache sana kiasi cha kutaka contact mpya zisizo hata fahamika zitokako???. tujifunze kuwa sisi wenyewe. mara nyingi dada zetu huwapuuza watu ambao mnawafahamu, halafu mnaanguka kwa mijitu hata haifahamiki
Uko sahihi kbs kindimbajuu,yani km siku ile angempotezea wala haya yote yasingemfika!
kwa upande wa wazazi mpaka sasa hawaelewi kitu na jeny jana usiku ameshamwambia huyo mchumba waairishe ndoa mpaka mwakani kwan kuna mambo anataka ayafahamu kuhusu huyo bwana,jamaa hakuibu na akakata simu na haikupatikana mpaka asubuhi ya leo!
 
hujasema kama njemba ilifanikisha azma yake au lah, poor jane, hapo sijui kama atataka tena kusikia mchumba maana atajua ni wale waleeeeeeee! mijanaume mingine bwana, ni kazi kutuharibia sisi tulio waaminifu, hovyo sana
Siku ile hakufanikisha,ndio hivyo km hili litapita itamchukua mda sn kusahu,pole zenu!
 
Back
Top Bottom