Msaada: Taasisi gani naweza pata mkopo wa Tsh Milioni 2

deni

JF-Expert Member
Aug 7, 2011
255
186
Habarini Wana JF,

Nnahitaji Mkopo wa 2M kwa ajili ya maswala ya biashara. Mimi ni muajiriwa katika shirika lisilo la kiserikali yaani NGO.

Nimejaribu kuulizia NMB ambayo ni bank ninayopokelea mshahara nimekwama kwa sababu muajiri wangu huwa hadhamini wafanyakazi wake kukopa.

Taasisi gani naweza kupata huduma hii ya mkopo kwa urahisi?
 
Nimeshaanza, nipo mwanzoni. Nimechukua frame, nimeweka mzigo kidogo. Nataka kuongezea. Licha ya hivyo sitegemei biashara kulipa mkopo, nategemea mishahara wangu!
Tafuta Saccos serious Jiunge huku ukiangalia mwenendo wa biashara yako.

Bank hazikopeshi biashara isiyo na cash flow na tayari ajira yako umesema mwajiri hataki kudhamini.

Na ukisema ukope kwenye taasisi ndogo za fedha utakwama kutokana na ukubwa wa riba.
 
Tafuta Saccos serious Jiunge huku ukiangalia mwenendo wa biashara yako.

Bank hazikopeshi biashara isiyo na cash flow na tayari ajira yako umesema mwajiri hataki kudhamini.
Na ukisema ukope kwenye taasisi ndogo za fedha utakwama kutokana na ukubwa wa riba.
Asante kwa ushauri mzuri. Nitatafuta saccos. Samahani nikuulize, kwenye hizi saccos unaweza kupata mkopo immedietly baada ya kuingia au ni baada ya kukaaa na kuweka kwa muda kidogo?
 
Asante kwa ushauri mzuri. Nitatafuta saccos. Samahani nikuulize, kwenye hizi saccos unaweza kupata mkopo immedietly baada ya kuingia au ni baada ya kukaaa na kuweka kwa muda kidogo?
Kila Saccos ina utaratibu wake. Nyingine zipo janjajanja sana, zinaendeshwa na kundi la wachache wapigaji.

Tena SACCOS kama hizo mara nyingi zinakopa Bank halafu na zenyewe zinaongeza riba na kukopesha wanachama.

Lakini mostly, Ukishajiunga SACCOS kwa kununua hisa, then ukaanza kuweka akiba unaruhusiwa kukopa mara 3 ya akiba yako uliyoweka.

Jambo la msingi ni hiyo biashara yako, watakuja kuingakia then unapewa pesa malipo unatoa kokote.
 
Kila Saccos ina utaratibu wake. Nyingine zipo janjajanja sana, zinaendeshwa na kundi la wachache wapigaji.

Tena SACCOS kama hizo mara nyingi zinakopa Bank halafu na zenyewe zinaongeza riba na kukopesha wanachama.

Lakini mostly, Ukishajiunga SACCOS kwa kununua hisa, then ukaanza kuweka akiba unaruhusiwa kukopa mara 3 ya akiba yako uliyoweka.

Jambo la msingi ni hiyo biashara yako, watakuja kuingakia then unapewa pesa malipo unatoa kokote.
Asante, ngoja nifanye ufuatiliaji.
 
Mkuu 2m usikope - unaweza kuitafuta tu ukaipata within very short time - ni mipango tu ikiwa madhubuti
 
Back
Top Bottom