Msaada sehemu ya mbele ya kichwa inauma sana

Its Pancho

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
14,175
22,572
Wakuu
Sehemu ya mbele ya kichwa yaani fore head ama tuite kipanda uso panauma sana siku ya 4 sasa shida ni nini? Na wala sina Mafia Nina kikohozi tu kidogo ..napata tabu kufanya shughuli zangu maana nikiinamisha sura chinj niandike document yoyote napata maumivu sana
 
1. Piga sana Maji.

2. Tumia painkillers.

3. Pumzika. Yaani toa mawazo yote. Jilaze sehemu tulivu.

4. Maumivu yakizidi, muone daktari.
Kwa kweli mkuu napumzika kidogo sanaaa
Halafu itabidi nianze kutekeleza haya hasa kunywa maji mengi nashkuru sana
 
Kuna mtu kasema sababu ni kutumia simu sana je ni kweli? Sababu nimegoogle sijaona hii sababu?
 
Kafanye vipimo.
Yaweza kuwa presha imeshuka. Au damu nyingi. Au macho yanaanza shida. Au hunywi maji ya kutosha. Au hulali usingizi wa kutosha. Mwisho kabisa dalili moja wapo ya covid kichwa kinauma sana sehemu ya forehead.

Pole sana ndio ukubwa huo
 
Chimba mzizi wa mti wa mwarubaini jifukize na unywe fanya ivo unipe feedback utasikia kuumwa tena.
 
Kafanye vipimo.
Yaweza kuwa presha imeshuka. Au damu nyingi. Au macho yanaanza shida. Au hunywi maji ya kutosha. Au hulali usingizi wa kutosha. Mwisho kabisa dalili moja wapo ya covid kichwa kinauma sana sehemu ya forehead.

Pole sana ndio ukubwa huo
Duh covid tena?? Kuna MTU alisema tupunguze matumizi ya simu..sasa mbona situmiagi sana simu labda computer
 
Back
Top Bottom