Msaada: Scholarship

Mtoto wa Mkulima

JF-Expert Member
Apr 12, 2007
681
126
wakuu habarini za asubuhi? natumaini mko poa kaisa. EE bwana wana JF naombeni msaada wa informations. Naombeni kama kunamtu yeyote mwenye taarifa za namna ya kupata scholarship ya MA iwe kule nyumbani Tz au nnje ya nchi naomba anisaidie. Scholarship yenyewe ikiwa ya Uchumi releted itakuwa bomba sana. Nitashukuru sana wakuu.
 
Wakubwa
kwakuwa fani yangu ni sanaa
nadhani kuna member anazo infos za programme za sanaa abroad maana nchini humu hakuna skolaship za art.
nazisaka kufa na kupona hivyo naomba msaada wenu
(still in fungate)
 
Msanii,
Angalia hiyo link ya eu. ina programme zaidi ya 100 katika fani zote, Sayansi, uchumi,sheria, Computer, Agriculture , Technolojia nk. Have time to go through the website and you will find one that suites you most
 
Msanii,
Fuatilia hiyo link ya eu, kuna scholarship kwa fani zote Sayansi, art, ICT, etc
 
Labda kuwasaidia wengine wote. Sweden, Finland na nadhani Norway(sina uhakika100% kwa Norway, Shule ni Bure kwanzia high school to Masters hivyo ukienda kwenye website zao mfano www.studyinsweden.se utaweza kufanya application moja kwa vyuo 8 na course 8 tofauti kazi kwenu
 
Nadhani tatizo ni namna ya kupata pesa kwa ajili ya kukidhi gharama za kuishi kama vile kulipia malazi, chakula na usafiri pamoja na viandika/viandikwa. Vinginevyo no tuition fee. Hata Ujerumani hakuna tuition fee. ila unatakiwa uwe na uwezo wa kumudu gharama za kuishi tu ambazo kwa wastani ni kati ya Euro 600-1000. Kusema kweli hii ni nafuu sana ukilinganisha na Uingereza ampapo tuition fee pekee ni kati ya Pound 9,000 hadi 14, 000 kwa mwaka na bado hujaongeza daily expenses ambazo ni kati ya Pound 600 - 1000 kwa mwezi.
 
Jibu Kwa Mtu na Mashoo: Kinachotakiwa ni kuonyesha proof of funds, sio lazima uwe nazo zako. Wanachofanya wanafunzi wengi huku ni kuchangiana, pesa zikitimia unaweka bank, halafu unaonyesha bank statement. Baada ya hapo unawarudishia waliokukopesha pesa zao. Halafu pia njia nyingine kama utaonyesha ushahidi kuwa unafanya kazi kwa kuonyesha pay slips za mishahara, hizo zinakubalika pia. Hizo shule nyingi hufundisha kwa kiingereza. Ni wengi tu wamesoma na kupata Ph.D zao hapa.
 
Wakubwa
kwakuwa fani yangu ni sanaa
nadhani kuna member anazo infos za programme za sanaa abroad maana nchini humu hakuna skolaship za art.
nazisaka kufa na kupona hivyo naomba msaada wenu
(still in fungate)

Mkuu heshima Mbele

Katika usanii hujasema haswa unataka kozi gani ktk sanaa na kiwango kipi cha elimu.
 
Mie nachukua nafasi hii kuchukua challenge hii na kutangaza scholarship ya $ 1500 mwaka wa kwanza kwa mwanafunzi wa kike kutoka vijijini (sio Dar-es-salaaam) anayequalify kusoma Computer Science katika Chuo Cha Elimu ya Juu Tanzania.

Niungeni mkono washikadau wa nchi.
 
Ndg Pundit na wengine hapo juu

Natoa pongezi nyingi kwenu kwa uzalendo mnaouonyesha wa kusaidia Watanzania wenzetu kwa hali na mali

keep up the spirit na Mola akuzidishieni
 
Jibu Kwa Mtu na Mashoo: Kinachotakiwa ni kuonyesha proof of funds, sio lazima uwe nazo zako. Wanachofanya wanafunzi wengi huku ni kuchangiana, pesa zikitimia unaweka bank, halafu unaonyesha bank statement. Baada ya hapo unawarudishia waliokukopesha pesa zao. Halafu pia njia nyingine kama utaonyesha ushahidi kuwa unafanya kazi kwa kuonyesha pay slips za mishahara, hizo zinakubalika pia. Hizo shule nyingi hufundisha kwa kiingereza. Ni wengi tu wamesoma na kupata Ph.D zao hapa.
Thanks kitia.Kwa maelezo yako ni kipindi mwanafunzi huyo atakuwa tayari yuko Ufini,mfano sasa mtu yuko tanzania na kapata chuo huko na najua ili kupata Visa inabidi uonyeshe bank statement ya hiyo Euro 6000.Hapo ndio ngoma kwa watanzania na kuona ni ngumu kwao kuona kama elimu ie ya bure.

Jamaa wangu mmoja alipata shule huko lakini alishindwa kwa sababu ya hio proof ya Euro 6000,labda kama sijakupata hapo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom