msaada plz, mama mjamzito anasumbuliwa na jino

Muarubaini

JF-Expert Member
Apr 7, 2012
222
48
naombe anayejua dawa, maana mjamzito harusiwi kung'oa, ametumia panado mpaka amechoka. thanx in advance.
 
Mpeleke Hospital achana na hizo panadol, ila me niliwahi ng'oa nikiwa mjamzito na sikupata tatizo lolote.
 
asante, wamasema eti kama ni la chin haina neno sana, ila lake ni la juu ambolo ndo wanasema linakuwa na shida
 
asante, wamasema eti kama ni la chin haina neno sana, ila lake ni la juu ambolo ndo wanasema linakuwa na shida

kama siku za kujifungua ziko karibu ni vema akaendelea kutumia dawa za kutuliza maumivu tu mara nyingine linaweza kuacha lenyewe. Vile vile unaweza ukang'oa lakini bado asiwe ametibu ugonjwa jino lingine likaendelea kuuma.
 
Je hilo jino limefikia hatua ya kung'oa kama unavyozungumzia? Siyo kwamba jino likiuma dawa yake ni kung'oa. Jino linaweza kuuma lakini likawa halijafikia hatua mbaya ya kung'oa. Amcheki Daktari kwanza na ikiwa halikufikia hatua ya kung'oa basi unipe taarifa sbb wapo wengi wanaolalamika kuhusu meno na matatizo ya kinywa lakini nafahamu product fulani nzuri sana ambayo nawaelekeza na tatizo kusahaulika na kuendelea kula nyama kama kawa. healthwealthfirst@gmail.com
 
Mambo mengi hapa Tz yanazungukwa na tamaduni hasa katka hili la mama wajawazito-kuna vipindi vitatu ktk ujauzito yenye miezi mitatu mitatu yaani Trimester-mbali na hatari zake-mbele ya Madaktari Hakuna kipindi ambacho mjamzito hawezi kutibiwa meno.
 
mimi nina rafiki yangu wakati akiwa mjamzito ikifika second trimister huwa anaumwa sana meno na kila akijifungua huwa anang'oa, daktari alimwambia kuwa ni wakati mtoto anatengeneza mifupa kwahiyo kama hana calcium ya kutosha ndo inasababisha hivyo
 
mimi nina rafiki yangu wakati akiwa mjamzito ikifika second trimister huwa anaumwa sana meno na kila akijifungua huwa anang'oa, daktari alimwambia kuwa ni wakati mtoto anatengeneza mifupa kwahiyo kama hana calcium ya kutosha ndo inasababisha hivyo

asante sana kwa maelezo hayo
 
naombe anayejua dawa, maana mjamzito harusiwi kung'oa, ametumia panado mpaka amechoka. thanx in advance.

Pole sana. Nenda katumie karafuu. saga karafuu kwenye blenda au kinu tengeza juice yake, awe anasukutua kila anaposikia mauumivu. Naomba unijulishe matokeo. Anza usiku wa leo. Asimeze, asimeze, asimeze.
 
mimi nina rafiki yangu wakati akiwa mjamzito ikifika second trimister huwa anaumwa sana meno na kila akijifungua huwa anang'oa, daktari alimwambia kuwa ni wakati mtoto anatengeneza mifupa kwahiyo kama hana calcium ya kutosha ndo inasababisha hivyo
Siyo kweli huo ni upotoshaji-wakati wa ujauzito mbali nakinga kushuka kwa kiwango fulan bado kuna mabadiliko ya uwiano wa homon zinazorahisisha ukuaji wa bacteria kinywani-sasa hali hii ikikutana na hali ya kutokusafisha meno vizuri matokeo yake ndio hayo.
 
jamani tukisemea experience za maudhi ya mimba hapa tutashangaa wenyewe. huwa napenda sana kutumia experience yangu mwenyewe.

nikiwa mjamzito wa 1st born wangu, ilipofika wiki 38 nilianza kuumwa sikio la kushoto, sijawah kuliingiza maji, wala kitu chochote hata iwe pamba lkn liliuma kama nakufa hivi. kwenda muhimbili, wakasema wananilaza, nilifanyiwa x-ray kuangalia kuna nn hakukuwa na fungus wala bakteria na mbaya zaid linawaka moto sana na linatoa maji maji yalipopimwa na kuwa cultured pia hakukuonekana bacteria ambao ni threat. unajua nn siku moja dr anjela thomas alisema hebu leo tumpime njia lolest, sina uchungu wala nn lkn njia ilikuwa imesha funguka cm 5, chupa haijavunjika wala sina dalili yyte ya labour zaid ya sikio tu. you cant believe ilibidi waniwekee maji ya uchungu ili nizae tu na ukweli uchungu ulipoanza tumboni sikio lilikoma na mtoto akazaliwa.

anyways nia yangu hapa nataka nikuonyeshe ndugu mtoa mada kwamba, maudhi ya mimba ni mengi na hayana clinical explanation ila kama kapimwa hana shida yyte ile basi usimsumbue kung'oa vumilie tu huku akitumia pain killer. pole yake sana tu.
 
MATAYARISHO
Chukua majani ya mtunda(muarubaini),majani ya mpera na magome ya muembe.Tia kwenye sufuria kisha

chemsha kwa maji yaliyo safi kwa muda wa dakika 15 hadi 20.

Kisha chukua dafu kubwa lenye nyama, likate sehemu ya juu kwa lengo la kutengeneza mlango

mdogo.Yatoe maji yote ya dafu kwa vile hayahitajiki na bakisha nyama tu.

MATUMIZI
Chukua maji yako ya dawa yaliyo moto na mimina kwenye dafu kiasi kwamba yakaribie kujaa.Kisha weka mdomo wako juu ya mdomo wa dafu kwa lengo la kuingiza mvuke wa dawa kwenye mdomo.Weka kisha

ondosha kulingana na umoto wa maji ya dawa kwa muda wa dakika 3 hadi 5.

Kisha sukutua kwa maji ya dawa ambayo yameshapungua joto kisha uyateme usiyanywe Tafadhali.

Endelea na zoezi hili asubuhi,mchana na jioni kwa muda wa siku tatu na kwa uwezo wa mwenyezi Mungu

atapona. Akitumia akipona tafadhali njoo hapa useme dawa ipi iliyomsaidia kupona uje utoe shukrani zako.

Please Give me your Feedback.
 
Back
Top Bottom