Msaada: Nyoka wananimalizia mayai ya kuku wangu

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.
Ninafuga kuku wa kienyeji hapa shambani kwangu. Kwa kweli kuku wanastawi vizuri na nilishaanza kufurahia matunda ya jasho langu, lakini ghafla nilianza kuona mayai yakipungua wakati kuku wanataga kila siku. Niliamini pasipo na shaka itakuwa nyoka. Hivi majuzi tukafanikiwa kumdaka nyoka mkubwa akiwa amemvamia kuku anayelalia. Kuku alianza kupiga kelele usiku ndipo tulipokurupuka na kwenda kuangalia, tukamkuta ameshameza mayai mawili tayari. Tulifanikiwa kumwua huyo nyoka.

Lakini hata baada ya kumwua huyo nyoka, bado mayai yameendelea kupungua. Pamoja na jitihada za kumwaga mafuta ya taa mlangoni na maeneo yanayozunguka nyumba lakini ufanisi ni mdogo. Hii mbinu ya kumvizia nayo ni ya kubahatisha. Je naweza kutumia mtego gani kuwamaliza nyoka shambani mwangu? Au nitumie dawa gani?
Mkuu unapatikana mkoa gani kwanza maana hao nyoka wanafaida sana kuliko hayo mayai ebu niambie unapatikana wapi nikupe dili la nyoka!
 
Huyo ni nyoka MTU
Hapo naona sio nyoka bali kuna mtu anaiba hayo mayai
Nilikuwa na kuku wengi sana na kulikuwa na joka kubwa sana ambalo ni la miaka lakini hata siku moja hajala mayai
Na ni msaidizi mzuri sana kwa vibaka kwani wanajua uwepo wake hapo na hawasogei
Asubuhi huwa anaota jua kwenye barabara ya kuingilia shambani
We achana na nyoka mwizi yupo hapo mvizie tu


Sent from my iPhone using Tapatalk
Hilo litakuwa joka la kibisa
 
Unawezaje kugundua idadi ya nyoka kwenye eneo lako?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni ngumu kugundua kiukweli..ila ni mara chache sana eneo la nyumbani kuwa na nyoka wengi.. Kwa kawaida anaweza akawa mmoja au wawili tu(dume na jike) ata wakizaa au kutotoa vile vitoto vinaenda kutafuta maisha mbali na hapo

Pia inategemea na mkoa uliopo..
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.
Ninafuga kuku wa kienyeji hapa shambani kwangu. Kwa kweli kuku wanastawi vizuri na nilishaanza kufurahia matunda ya jasho langu, lakini ghafla nilianza kuona mayai yakipungua wakati kuku wanataga kila siku. Niliamini pasipo na shaka itakuwa nyoka. Hivi majuzi tukafanikiwa kumdaka nyoka mkubwa akiwa amemvamia kuku anayelalia. Kuku alianza kupiga kelele usiku ndipo tulipokurupuka na kwenda kuangalia, tukamkuta ameshameza mayai mawili tayari. Tulifanikiwa kumwua huyo nyoka.

Lakini hata baada ya kumwua huyo nyoka, bado mayai yameendelea kupungua. Pamoja na jitihada za kumwaga mafuta ya taa mlangoni na maeneo yanayozunguka nyumba lakini ufanisi ni mdogo. Hii mbinu ya kumvizia nayo ni ya kubahatisha. Je naweza kutumia mtego gani kuwamaliza nyoka shambani mwangu? Au nitumie dawa gani?
Mjomba huyo ni nyoka mtu anayeishi hapo shamba....otherwise atakuwa ni kenge siyo nyoka huyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi nawaza nikichukua yai nikatoboa kidogo nikaingiza sumu ya panya. Huyo nyoka atakula? Hebu jaribu hii. Toboa kwa ustadhi ingiza sumu ndani ya yake. Pia wanasema ukilichemsha yai halafu umamtegea. Kwa kuwa analimeza halitakaa lipasuke au kuyeyuka na atakufa.

Yai ukilitoboa tu linaliwa na kuku.. sasa ukiweka sumu kwenye yai basi umetega kuku wako mwenyewe
 
Yai ukilitoboa tu linaliwa na kuku.. sasa ukiweka sumu kwenye yai basi umetega kuku wako mwenyewe
Mkuu kama ukitoboa ni lazima kuku uwafungie kwanza eneo lingine mpaka yai limezwe. Ila pia ukilichemsha ndiyo imara kabisa maana haliyeyuki. Ni lazima afe tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom