kipapi
JF-Expert Member
- Sep 13, 2016
- 1,056
- 1,374
Awali ya yote napenda kumshukuru muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake.
Ni matumaini yangu hamjambo na wote ni wazima wa afya. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 elimu yangu ni kidato cha nne (form four) sikuweza kujiendeleza kwa njia yoyote kielimu kutokana na hali ya maisha yangu, hivyo kutokana na maisha yangu kuwa magumu na kukulia katika umaskini mkubwa baada tu ya kumaliza kidato cha nne niliamua kutafuta kazi na kufanikiwa kupata kazi ya ulinzi katika kampuni moja hapa mjini.
Kulingana na hali yangu nikawa naweka pesa kama akiba ili nije kujiendeleza kielimu kwani naamini maisha bila elimu ni sawa na bure. Nimefanya kazi ya ulinzi kwa muda wa miaka sita (6) na sasa nimekusanya pesa kwa kiasi lakini ndoto yangu ni ileile bado nataka kujiendeleza kielimu, sitaki kurudia masomo ninachohitaji sasa ni ufundi (taaluma) yoyote iwe kama fani yangu.
Hivyo napata tabu na shida sana nikifikiria ni fani ipi nijifunze na sina hata aidia (idea) na fani yoyote.
Naombeni msaada wa mawazo yenu wanajamvi wenzangu, ahsanteni na Mungu awabariki sana,..
Nawasilisha
Ni matumaini yangu hamjambo na wote ni wazima wa afya. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 elimu yangu ni kidato cha nne (form four) sikuweza kujiendeleza kwa njia yoyote kielimu kutokana na hali ya maisha yangu, hivyo kutokana na maisha yangu kuwa magumu na kukulia katika umaskini mkubwa baada tu ya kumaliza kidato cha nne niliamua kutafuta kazi na kufanikiwa kupata kazi ya ulinzi katika kampuni moja hapa mjini.
Kulingana na hali yangu nikawa naweka pesa kama akiba ili nije kujiendeleza kielimu kwani naamini maisha bila elimu ni sawa na bure. Nimefanya kazi ya ulinzi kwa muda wa miaka sita (6) na sasa nimekusanya pesa kwa kiasi lakini ndoto yangu ni ileile bado nataka kujiendeleza kielimu, sitaki kurudia masomo ninachohitaji sasa ni ufundi (taaluma) yoyote iwe kama fani yangu.
Hivyo napata tabu na shida sana nikifikiria ni fani ipi nijifunze na sina hata aidia (idea) na fani yoyote.
Naombeni msaada wa mawazo yenu wanajamvi wenzangu, ahsanteni na Mungu awabariki sana,..
Nawasilisha