Msaada: Niufundi gani nikajifunze veta ambao utaendana na soko la ajira

kipapi

JF-Expert Member
Sep 13, 2016
1,056
1,374
Awali ya yote napenda kumshukuru muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake.

Ni matumaini yangu hamjambo na wote ni wazima wa afya. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 elimu yangu ni kidato cha nne (form four) sikuweza kujiendeleza kwa njia yoyote kielimu kutokana na hali ya maisha yangu, hivyo kutokana na maisha yangu kuwa magumu na kukulia katika umaskini mkubwa baada tu ya kumaliza kidato cha nne niliamua kutafuta kazi na kufanikiwa kupata kazi ya ulinzi katika kampuni moja hapa mjini.

Kulingana na hali yangu nikawa naweka pesa kama akiba ili nije kujiendeleza kielimu kwani naamini maisha bila elimu ni sawa na bure. Nimefanya kazi ya ulinzi kwa muda wa miaka sita (6) na sasa nimekusanya pesa kwa kiasi lakini ndoto yangu ni ileile bado nataka kujiendeleza kielimu, sitaki kurudia masomo ninachohitaji sasa ni ufundi (taaluma) yoyote iwe kama fani yangu.
Hivyo napata tabu na shida sana nikifikiria ni fani ipi nijifunze na sina hata aidia (idea) na fani yoyote.

Naombeni msaada wa mawazo yenu wanajamvi wenzangu, ahsanteni na Mungu awabariki sana,..

Nawasilisha
 
Awali ya yote napenda kumshukuru muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake,
Ni matumaini yangu hamjambo na wote ni wazima wa afya.
Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 elimu yangu ni kidato cha nne (form four) sikuweza kujiendeleza kwa njia yoyote kielimu kutokana na hali ya maisha yangu, hivyo kutokana na maisha yangu kuwa magumu na kukulia katika umaskini mkubwa baada tu ya kumaliza kidato cha nne niliamua kutafuta kazi na kufanikiwa kupata kazi ya ulinzi katika kampuni moja hapa mjini.
Kulingana na hali yangu nikawa naweka pesa kama akiba ili nije kujiendeleza kielimu kwani naamini maisha bila elimu ni sawa na bure. Nimefanya kazi ya ulinzi kwa muda wa miaka sita (6) na sasa nimekusanya pesa kwa kiasi lakini ndoto yangu ni ileile bado nataka kujiendeleza kielimu, sitaki kurudia masomo ninachohitaji sasa ni ufundi (taaluma) yoyote iwe kama fani yangu.
Hivyo napata tabu na shida sana nikifikiria ni fani ipi nijifunze na sina hata aidia (idea) na fani yoyote.
Naombeni msaada wa mawazo yenu wanajamvi wenzangu, ahsanteni na Mungu awabariki sana,.. Nawasilisha
Ufundi magari mkuu
 
Kwenye sector ya ujenzi nashauri ufanye kati ya haya,
1. Installation ya umeme kwenye majengo
2. Plumbing( maji safi na taka kwenye majumba)
3.air conditining installation
4.lift installation
Sina hakika kama lift unaweza kuipata veta.ila katika hiyo list chagua kozi yeyote moja
 
Kwenye sector ya ujenzi nashauri ufanye kati ya haya,
1. Installation ya umeme kwenye majengo
2. Plumbing( maji safi na taka kwenye majumba)
3.air conditining installation
4.lift installation
Sina hakika kama lift unaweza kuipata veta.ila katika hiyo list chagua kozi yeyote moja
Asante kwa ushirikiano mkuu.... Hapo kwenye hii list kozi zote nimezipenda ila sijajua itachukua muda gani maana kutokana na umri wangu ningependa kozi ambayo haitagharimu muda (zaidi ya miaka miwili) upande wa Ada sio tatizo. Na ningependelea unichagulie moja kati ya hizo ambayo nitaweza kuajiliwa kwanza na Baadae kujiajiri mm mwenywe. Ahsante
 
Naendelea kupokea mawazo tofauti tuendelee kuchangia
 
Awali ya yote napenda kumshukuru muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo ndani yake.

Ni matumaini yangu hamjambo na wote ni wazima wa afya. Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28 elimu yangu ni kidato cha nne (form four) sikuweza kujiendeleza kwa njia yoyote kielimu kutokana na hali ya maisha yangu, hivyo kutokana na maisha yangu kuwa magumu na kukulia katika umaskini mkubwa baada tu ya kumaliza kidato cha nne niliamua kutafuta kazi na kufanikiwa kupata kazi ya ulinzi katika kampuni moja hapa mjini.

Kulingana na hali yangu nikawa naweka pesa kama akiba ili nije kujiendeleza kielimu kwani naamini maisha bila elimu ni sawa na bure. Nimefanya kazi ya ulinzi kwa muda wa miaka sita (6) na sasa nimekusanya pesa kwa kiasi lakini ndoto yangu ni ileile bado nataka kujiendeleza kielimu, sitaki kurudia masomo ninachohitaji sasa ni ufundi (taaluma) yoyote iwe kama fani yangu.
Hivyo napata tabu na shida sana nikifikiria ni fani ipi nijifunze na sina hata aidia (idea) na fani yoyote.

Naombeni msaada wa mawazo yenu wanajamvi wenzangu, ahsanteni na Mungu awabariki sana,..

Nawasilisha
fundi majeneza mkuuu
 
Kajifunze ufundi Cherehani, jifunze mambo ya kupamba wanaita kudarizi! Na utundu mwingine, Ukimaliza hapo fungua Tailoring Mart yako, anza na cherehani hata mbili tu na tafuta MTU mfanye colabo, kisha lipia kibanda shona Mashati ya kudarizi na magauni yake. Shona Suti na mavazi ya kibubifu!!! Kuwa mwaminifu Kwa kazi yako, tembea huku na huko uone Mungu atakavyobariki kazi za mikono yako hadi ukimbie
 
Back
Top Bottom