Msaada; Nina tatizo la kuona na kusikia vyote kwa pamoja

bachelor sugu

JF-Expert Member
Jan 30, 2018
2,689
3,641
Ni miaka saba sasa imepita tangu nipate tatizo hili la kuona na kusikia,macho yangu hayana maumivu ya aina yoyote, hayawashi, hayachomi wala hayanisumbui kwa chochote isipokuwa kutoona vizuri.

Masikio yenyewe hunipa usumbufu wa kutoa mwangwi ndani yake (yaani nikiongea najisikia) hasa naposimama kwa muda mrefu, napotembea juani sana, ninapokuwa na njaa ila nikikaa chini mwangwi hupotea au ninapogeuza shingo.

Matatizo mengine yanayoambatana na hili ni kupatwa na ganzi ktk ncha za vidole vyote vya mikono, Kukosa balance napokuwa natembea pamoja na kutokuwa na nguvu ya kutosha ya mwili.

TAFADHALI KAMA KUNA MWENYE UELEWA AU DAKTARI BINGWA NAOMBA MSAADA KUJUA TATIZO LANGU LINATIBIKA AU LA.
 
Pole sana. ... upande wa macho jaribu kuwaona Dr Agarwal's Eye Hospital Morocco nyuma ya jengo la airtel japo ni gharama kidogo
Nimeanza kuhisi kuwa yawezekana kuwa tatizo langu sio la macho wala masikio Bali yawezekana linahusiana na mjshipa ya fahamu so maybe kama kuna specialist wa nerves huyo na anaweza kunifaa zaidi.
 
Mkuu utakuwa na tatizo kwenye ubongo kulingana na maelezo yako

Nakushauri nenda Muhimbili/MOI pale utafanya CT SCAN ya kichwa
 
Mkuu utakuwa na tatizo kwenye ubongo kulingana na maelezo yako

Nakushauri nenda Muhimbili/MOI pale utafanya CT SCAN ya kichwa
It might be true siwezi bisha.Ofcourse CT SCAN inaweza toa majibu ya nn hasa tatizo.
 
Nilishajiribu kwenda hospitali baadhi ya hospitali km vile CCBRT,Hindu Mandal but I wasn't satisfied with the treatment at all and my condition is still the same.
Pole sana ndugu.
Kwa Yesu kuna uponyaji wa kweli wanaposhindwa madakitari wa elimu dunia YESU hashindwi

Nakuomba uje ktk ibada upokee uponyaji wako utaombewa na utapona.

Kama upo Dar nijurishe pm ili nikuelekeze pahali pa kufanyiwa maombi upone.
 
Pole sana ndugu.
Kwa Yesu kuna uponyaji wa kweli wanaposhindwa madakitari wa elimu dunia YESU hashindwi

Nakuomba uje ktk ibada upokee uponyaji wako utaombewa na utapona.

Kama upo Dar nijurishe pm ili nikuelekeze pahali pa kufanyiwa maombi upone.
Thank you brother for your concern and touch in my problem but I still hope hospital treatment can work.Thanks again.
 
Unasema ulikwenda hospital hujaeidhika na matibabu why
Nilienda CCBRT tena kule fast track but docta alinipima macho very roughly kisha akaniambia ww una low vision hivyo nenda kule kwenye department ya low vision,kufika kule wakaanza kuniambia tu ule mboga za majani sana,matunda,karoti wakanipa na lundo la vidonge vinaitwa neurobion Forte wakaniruhusu ss binafsi sikuridhika na matibabu yale.
 
Back
Top Bottom