Kazetela
JF-Expert Member
- Nov 12, 2016
- 1,714
- 1,618
Jameni kama Kichwa cha uzi kinavyojieleza,
mimi ni kijana ambae nina ndoto nyingi tu za maisha na Mungu akisaidia nitazitimiza.
Juzi kati nilipewa zawadi na rafiki yangu mzungu kutoka USA. Bwana Lenox,Simu aina ya TECNO CX mpya toleo jipya.
Na mpaka sasa simu ninayo.
Lakini ndugu zangu mimi nina hali mbaya kiuchumi na hata vocha muda mwingine huwa nakoswa.
Sasa ili kukabiliana na ugumu wa maisha ningependa,nyinyi wana JamiiForums,Mnikopeshe kiasi cha Tsh.150,000/=.
Mtanipa hicho kiasi cha pesa kwa kuiweka simu hii Bond kwenu,kwa makubaliano ya kurejesha hiyo pesa badae,kulingana na makubaliano yetu tutakayoyafanya.
Siyo kwamba siipendi hii simu,la hasha.
Lengo ni kukuza kibiashara changu hapa ili angalau niweze kuukabili umasikini ulio tukuka.
Kwasasa natumia hiki kimeo changu cha zamani kuingilia humu JF na simu hii niliyopewa ama kuachiwa kama zawadi na rafiki yangu Bw.Lenox nimeitunza tu simu na wala sijaitoa kwenye karatasi zake wala maboksi lake,Naitamani na mimi kuitumia lakini hakuna namna.
Nawatakieni Jumapili njema.