Msaada: Nina kesi ya wizi baada ya kununua bidhaa Kupatana.com

kichui2018

Member
Jan 10, 2019
7
7
Habari, naomba ushauri juu hili suala.

Nilinunua bidhaa kupitia mtandao wa Kupatana. Sasa nakabiliwa na kesi ya wizi.

Naombeni ushauri juu ya hili.
 
Yeah ninavyo mkuu
Bidhaa Gani?
Aliekuuzia umewasiliana nae anasemaje?
Alipokuuzia alikupa na Risiti ya bidhaa alivonunua yeye dukani?
Una ata conversation WhatsApp, SMS, zinazoonesha uliuziana na uyo mtu?
Una screenshot la ilo Tangazo Kupatana?

tuanzie hapo.
 
Kwako mleta uzi. Hii kesi hao askari wanataka pesa yaani hata ukiwaonyesha convo na ushahidi haitasaidia. Waweza kuta hata aliyekuuzia wakampata na bado na wewe wakakung'ang'ania.

Kama unaona una time ya kuburuzana nao ng'ang'ana na kusema una ushahidi nje ya hapo pesa itakutoka.
 
Tabia ya kupenda kununua electronic equipments au magari kutoka mikononi mwa watu ni hatarishi sana. Kuna rafiki yangu mmoja alidhani kaokota dodo jangwani na kununua Ipad kwa bei poa. Alikuja kuokotwa Mlimani City kama kifaranga cha bata. He had to pay excessively kumaliza lile soo.
 
Mkuu vitu second hand vya mbongo ni mkosi, utakuja kupata kesi ya kichwa.
fikiria kama iliko ibwa kauwawa mtu, au vyuma vya moto vilitumika.

Only buy what you can afford, if you can't buy direct from the shop because it's expensive, then wait until you can afford it.
 
Kwa nchi zetu hizi kununua kitu mkononi kwa mtu inaweza kuwa rahisi lakini inaweza kukuletea matatizo makubwa sana. Chukua tahadhali inapobidi kununua kitu kwa mtu.

Vuta subira, weka fedha na nenda kanunue dukani.

Wengi wamepata kesi kubwa na kutoa fedha nyingi zaidi kwa mali za mikononi ambazo huwa rahisi sana.

Ikibidi kununua basi walau nenda kwenye maduka maalumu yanayouza vitu vilivyotumika.
 
joshua_ok,
]Ni vyema tukajadili hili kwa hekima kwani lisipokukuta la aina hii laweza kukukuta la aina nyingine...:p
::Aliyekuuzia jitahidini kum track maana namba yake si unayo?"
::Toa maelezo clear kwa hao police,ambatanisha screen shorts zote na namba ya aliyekuuzia,ukiona tabu,panda ngazi ya juu kidogo ya kipolisi maana polisi wa ngazi ndogo huwa wako kirushwa na kiuonevu zaidi.usiogope kupanda ngazi za ikibidi ya juu zaidi.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom