rich1
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,967
- 3,189
Asante Kwa Somo ZuriMBINU 10 ZA KUONGEZA WINGI WA MBEGU ZA KIUME (sperm count)
1. Kula lishe bora
Chakula unachokula kina mchango mkubwa katika kutibu tatizo hili. Vyakula vingi vya kisasa havina uwezo wa kuongeza uwingi wa mbegu.
Kama utarekebisha tu aina ya chakula unachokula kunaweza kupelekea kutibu tatizo lako.
Punguza matumizi ya sukari na vyakula vya ngano. Ongeza zaidi matunda, mboga za majani na mafuta yenye afya.
Hii inaweza kusaidia kutibu tatizo lako la kuwa na mbegu chache kwa haraka sana.
2. Acha kutumia vinywaji au vyakula vyenye kaffeina
Kama una tatizo la kuwa na mbegu chache ni vizuri ukaacha kutumia vinywaji au vyakula vyote vyenye kaffeina kwanza.
Navyo ni pamoja na chai ya rangi, kahawa, soda nyeusi zote, malta, redbull, chokoleti nk.
Hivi vitu vyenye kaffeina ni sababu ya kupungua kwa uwingi wa mbegu za kiume.
3. Tumia kitunguu swaumu
Kitunguu swaumu ni maajabu ya Mungu mwenyewe. Kitunguu swaumu kina Selenium na pia kinaondoa sumu mwilini vitu viwili mhimu kwa ajili ya kuongeza spidi ya mbegu.
Kitunguu swaumu kina kitu kingine kiitwacho ‘Allicin’ ambacho huongeza msukumo wa damu kwenda kwenye uume.
Ongeza kitunguu swaumu kwenye chakula unachopika.
Pia unaweza kutafuna punje 2 au 3 kila unapoenda kulala au unaweza kukatakata hizo punje 3 vipande vidogo vido (chop) kisha unywe na maji.
Usizidishe zaidi ya punje 3 kwa siku.
4. Kula ndizi
Ndizi hazifanani tu na uume kama unavyoweza kuwaza bali pia ni chakula kizuri kwa ajili ya afya ya uume wako. Ndizi zina kimeng’enya kimoja adimu sana kijulikanacho kama ‘Bromeliad’ ambacho husaidia kuziweka sawa homoni zinazohusiana na tendo la ndoa.
Ndizi pia zina Magnesiamu, Vitamini B1 na Vitamini C, vitu ambavyo ni mhimu sana kwa ajili ya kutengeneza mbegu za kiume.
5. Kula mbegu za maboga
Mbegu za maboga zina kiasi kingi ccha madini ya Zinki ambayo ni mhimu katika kuundwa au kutengenezwa kwa mbegu za kiume na homoni ya testosterone.
Pia zina vitamini B, C, D, E, na K ambazo zote ni vitamini mhimu katika kuongeza hamu ya kushiriki tendo la ndoa na nguvu kwa ujumla.
Pia mbegu za maboga zina kalsiamu, potasiaumu, niacin na phosphorous.
6. Kula zaidi mboga za majani
Mama alikuwa sahihi kumbe ingawa nilikuwa nachukia nikikuta mboga majani badala ya nyama nikirudi kutoka shule.
Mboga za majani zinapunguza homoni ya ‘estrogen’ na hivyo kufanya homoni ya ‘testosterone’ ipatikane kwa wingi na kiurahisi zaidi na hivyo mbegu zako ziweze kuongezeka bila vipangamizi vyovyote.
7. Kunywa maji mengi kila siku
Maji ya kunywa
Hili ni suluhisho rahisi lisilohitaji gharama wala ugomvi wowote kukuelewesha. Mwenyewe unajua kuwa maji ni uhai na kuwa asilimia 75 ya mwili wako ni maji, sasa kama huna tabia ya kunywa maji ya kutosha kila siku sijuwi unategemea miujiza kutoka wapi.
Huhitaji kusikia kiu au mpaka upate hamu ya kunywa maji bali hili ni jambo la lazima kwamba huwezi kukaa bila kunywa maji halafu ubaki na afya bora.
Mbegu zako zimetengenezwa kwa maji, zipo kwenye hali ya kimiminika.
Kutokunywa maji ya kutosha kila siku kuna uhusiano wa moja kwa moja na kupungua kwa uwingi wa mbegu.
Kama utatekeleza mengine yote niliyoelekeza hapo juu halafu ukasahau kunywa maji hesabu umeshachemka tayari.
Kutegemea na uzito wako unaweza kuhitaji maji lita 2 mpaka 3 kila siku.
8. Tumia vyakula vyenye folic asidi kwa wingi
Katika utafiti mmoja wanaume walioongeza utumiaji wa folic asidi na zink waliongeza uwingi wa mbegu zao kwa zaidi ya asilimia 74 kwa muda wiki 2 tu.
Vyakula hivi ni pamoja na tunda la parachichi na karoti.
Hivyo isipite siku bila kula parachichi 1 kutafuna karoti moja kama una tatizo la mbegu chache.
Vingine ni pamoja na mbegu za maboga, ufuta, alizeti, maharage, chungwa, papai, bamia nk
9. Mayai
Mayai yanachukuliwa kama mbadala wa uhakika zaidi katika kuongeza uwingi wa mbegu pamoja na kuongeza spidi au kasi yake. Yana vitamini E nyingi na protini ya kutosha vitu viwili mhimu katika kuongeza mbegu.
Mayai yanafanya kazi nyingine mhimu nayo ni kuzilinda seli za mbegu za kiume kutoshambuliwa na vijidudu nyemelezi kirahisi ambavyo vinaweza kuwa sababu ya kupungua kwa mbegu zako.
Viinilishe vilivyomo kwenye mayai vinafanya kazi ya ziada ya kuzifanya mbegu zenye afya zaidi na zenye nguvu zaidi jambo ambalo ni mhimu kwa ajili ya uzazi kwa upande wa mwanaume.
Kumbuka ni mayai ya kuku wa kienyeji tu yanayofaa kwa kazi hii. Kila siku kula mayai mawili mpaka matatu kama una tatizo hili la kuwa na mbegu chache.
10. Spinach
Folic asidi ni kitu mhimu katika kuongezeka kwa mbegu za kiume. Spinachi na mboga nyingine za majani zenye rangi ya kijani ni mhimu kwa ajili hii sababu ya vitamini na kuweka sawa usawa wa ‘folate’ kwenye mfumo wako wa mwili.
Kama folate ipo chini kuna uwezekano ukawa unatengeneza mbegu zisizo na umbile linalotakiwa kwa uzazi na hiyo hupelekea shida na matatizo mengine ya uzazi upande wa mwanamke (birth defects) kama ujauzito kutoka mara tu mimba inapotungwa
AmenKama ngoma inasimama vizuri sidhani kama hili in tatizo kubwa kihivi ,cheki na wataalamu pia Muombe Mungu sana atakusaidia .
Sent using Jamii Forums mobile app
duh!! huyo ana tatizo mkuuMarinda unayo?
Subiri kwenye uzao wako upate mtoto wa kiume...zen yamkute yaliyo nilikita ntaomba umuulize marinda unayo...maana wewe c umeaagana na mungu.Marinda unayo?
Tatizo pacha langu liko hivi, mie mabao hamna kabisa! Uume unadinda vizuri na kuingia kwa bibi kama kawa, ila nitapiga mashine hata zaidi ya nusu saa au saa nzima lakini babu hatemi ng'o! Tatizo hili limenianza kwenye age ya 53, ila kabla ya hapo mambo yalikuwa mubashar! Solution please!Si kwamba hana mabao ni kwamba mabao yapo ila hayana sile sperm mbegu si swala la kumbeza mtu anaeomba msaa mahala ambapo anaamin atapata msaada halaf anapuuzwa ki hivi
Nenda hospital kachek mirija kama IPO sawaTatizo pacha langu liko hivi, mie mabao hamna kabisa! Uume unadinda vizuri na kuingia kwa bibi kama kawa, ila nitapiga mashine hata zaidi ya nusu saa au saa nzima lakini babu hatemi ng'o! Tatizo hili limenianza kwenye age ya 53, ila kabla ya hapo mambo yalikuwa mubashar! Solution please!
Sent using Jamii Forums mobile app
Ingekua ni case ya low sperm count tu
Yan doctor alivyo niambia nilimcheki Mara 2....nikasema moyoni daaaa yan hapa ata nauli ya ndege kutoka DSM mpaka mwanza sinaIngekua ni case ya low sperm count tu
Isingekua issue sna mkuu
Ila azoospermia maana yake ni hali yakua hamna hata sperm mmoja ktk yale maji yooote ya manii unayotoa
Sasa tiba yake ni ndefu mkuu , kwa hapa kwetu
Wengi ambao walimepatikana na hio condition wanakata tamaa kutibika but nothing is imposible mkuu
Pambana na mungu atakufanyia miujiza yke utafanikiwa tu
Sent using Jamii Forums mobile app
Bila ya shaka ni tangazo la biashara labda tumshauri alipie kodi.....kama ulikuwa na nia ya kutujuza, weka kila kitu hapa , weka formula yote hiyo.. otherwise utuambie hili ni tangazo la biashara.