Msaada: Nifanyaje ili biashara ya kuku inipe mafanikio ya kimaisha

Entreprenuare

JF-Expert Member
Aug 24, 2019
1,616
1,714
Nimeanza na ufugaji wa kuku aina ya kloiler, ninao 40, wa size tofauti tofauti. Sasa hii business nataka iwe ajira yangu,

Swali linakuja:

Je, nifanyaje, hii biashara iweze kunipa mafanikio ya kimaisha.. kama kujenga, kuwa na usafir binasfi etc.

Naombeni mawazo yenu, wataalam. Mm mgeni kwenye hii tasnia.

Ushauri wa wadau
Rudi mezani (mipango). Tengeneza malengo yako kisha hakikisha unayo yafuatayo;

1. Msukumo (drive)
2. Kujiamini (Confidence)
3. Maarifa (Know-how)

Pia kama uko serious sana na unataka uendelevu kwenye biashara hiyo basi yafuatayo ndiyo mihimi mikuu ya biashara yako;

1. Maendeleo ya biashara yaani business devt. Hapo utakuza biashara yako kwa kutatua matatizo makuu mawili;

I. Wateja wapya (new aquisitions)

II. Retention (hakikisha humpotezi mteja kirahisi)

2. Operations mgt. Hakikisha mipangilio sahihi ya shughuli zako kwenye ufugaji. Masuala kama chakula, chanjo, magonjwa, masoko, usafi, nk yapangiliwe vizuri. Vinginevyo muda wote utakuwa behind time.

3. Customer service. Uwe customer focused na siku zote tanguliza maslahi ya mteja kisha wewe ufuate. Hakikisha wateja unawahudumia vyema kama vile unavyohudumiwa ukipigaga simu customer care.

Mf, mteja anaulizia kuku na wewe huna. Usiishie tu kumwambia "kuku wameisha", bali mpe taarifa zaidi. Kwamba, " mimi sina ila waweza wapata sehemu flani, mimi nitakuwa nao baada ya mwezi hivi".

Mteja huyo usishangae akaahirisha kununua kuku mpaka pale wa kwako watakapokuwa tayari ikiwa halazimiki sana kununua kwa wakati huo, (true story).

4. Mwisho ni people management (HR). Hakikisha tangu mwanzo mwa mradi unachagua watu sahihi kuuzunguka mradi wako. Yaani wasaidizi pale utakapohitaji, wateja, washauri, wauzaji pembejeo, saplaya wa chakula, nk.

Ukifungamana na watu wasio sahihi mf wateja wasiokulipa au wafanyakazi wavivu, mradi wako utakwama na si unajua ng'ombe akikonda hachekwi yeye ng'ombe, unachekwa wewe mfugaji.

Kazi kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakushauri. Nimefuga kuku kwa zaidi ya miaka 10. Gharama kubwa ziko kwenye chakula. Na bei huwa zinapanda sana na hazieleweki. Cha kwanza pata eneo la kutosha. Ifahamike kuwa sheria itakuja kuwabana wafugaji wa mijini kuhusu eneo la kufugia tafuta kuanzia hekari 5.

Pia utaweza kupunguza gharama za chakula kwa kuotesha baadhi ya vitu vinavyohitajika ikiwa ni pamoja ma majani kama mlonge au lukina au mulberry. Pia kama ni wa kienyeji utaweza kuwatoa nje wajitaftie.

Cha pili jenga banda ambalo litapunguza magonjwa na hivyo kukupunguzia matumizi ya madawa.

Cha tatu ili mradi wa kuku ukupe faida nono uunganishe na miradi mingine mfano mradi wa bustani na uzalishaji wa biogas au miradi mingine inayohusiana. Hapa nitaweka kiambatanisho cha kuonyesha mfumo wenyewe ukoje.

Chakula kinachukua asilimia kubwa sana hivyo ni vyema mfugaji akawa na stock ya kutumika muda mrefu au akaagiza moja kwa moja kutoka kiwandani ikiwa anafuga kwa kiwango kikubwa.

View attachment 1409082
 
Kufuga unaweza kufuga na kufikisha idadi ya kuku wengi kadri utakavyo. Cha muhimu weka kumbukumbu ya gharama ulizotumia kuhusu ujenzi, chakula, madawa, usafiri, usafi, mishahara, n.k. Baada ya hapo panga bei kila kuku utamuuza bei gani ili upate faida. Nakuambia! Tena nisikilize vizuri. Hiyo bei utakayoipata ukienda nayo kwenye soko utalia! Hapo ndo utajua ufugaji wa kuku ni biashara kichaa! Fuga kwa kitoweo tu basi au labda kama una hoteli au jiko baa basi utapika na kuuza na chakula kupunguza makali ya bei ya soko ambayo haiendani na gharama za ufugaji. Nina uzoefu katika hili!
 
Entreprenuare,

Rudi mezani (mipango). Tengeneza malengo yako kisha hakikisha unayo yafuatayo;

1. Msukumo (drive)
2. Kujiamini (Confidence)
3. Maarifa (Know-how)

Pia kama uko serious sana na unataka uendelevu kwenye biashara hiyo basi yafuatayo ndiyo mihimi mikuu ya biashara yako;

1. Maendeleo ya biashara yaani business devt. Hapo utakuza biashara yako kwa kutatua matatizo makuu mawili;

I. Wateja wapya (new aquisitions)

II. Retention (hakikisha humpotezi mteja kirahisi)

2. Operations mgt. Hakikisha mipangilio sahihi ya shughuli zako kwenye ufugaji. Masuala kama chakula, chanjo, magonjwa, masoko, usafi, nk yapangiliwe vizuri. Vinginevyo muda wote utakuwa behind time.

3. Customer service. Uwe customer focused na siku zote tanguliza maslahi ya mteja kisha wewe ufuate. Hakikisha wateja unawahudumia vyema kama vile unavyohudumiwa ukipigaga simu customer care.

Mf, mteja anaulizia kuku na wewe huna. Usiishie tu kumwambia "kuku wameisha", bali mpe taarifa zaidi. Kwamba, " mimi sina ila waweza wapata sehemu flani, mimi nitakuwa nao baada ya mwezi hivi".

Mteja huyo usishangae akaahirisha kununua kuku mpaka pale wa kwako watakapokuwa tayari ikiwa halazimiki sana kununua kwa wakati huo, (true story).

4. Mwisho ni people management (HR). Hakikisha tangu mwanzo mwa mradi unachagua watu sahihi kuuzunguka mradi wako. Yaani wasaidizi pale utakapohitaji, wateja, washauri, wauzaji pembejeo, saplaya wa chakula, nk.

Ukifungamana na watu wasio sahihi mf wateja wasiokulipa au wafanyakazi wavivu, mradi wako utakwama na si unajua ng'ombe akikonda hachekwi yeye ng'ombe, unachekwa wewe mfugaji.

Kazi kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wateja wa kuku ingekuwa wana ushirikiano ni biashara nzuri sana ila wateja sijui huwa wakoje yaani. Ukipiga gharama ya kumkuza kuku hadi anafika siku ya kuuzwa inaweza kuwa 5000 alafu utakuta kuna mtu anauza 4700! Huwa wanaharibu soko wenyewe kabisa. Inabidi wafike sehemu wawe kama wauza mafuta bei ikipangwa hakuna anaeshuka chini ya bei ng'o!

Sasa utakuta mama kaanzishiwa mradi wa kuku na mumewe na bado mumewe ananunua chukula na madawa siku ya kuuza mama anauza hata 3500 tu mradi anapewa milioni 2 ya pamoja anaona nyiiingi kisha anaenda kwa mumewe tena kuomba hela ya vifaranga wapya na kwa kuwa Mr yuko TRA au Vodacom meneja wa kitu fulani shida yake ni kuona mama yuko busy hakai bure anampa tu. Sasa wewe anza na Kroiler wako watano hao uje ufurahie shoo kwenye market
 
Hizi blahblah za darasani hazifanyikazi katika maisha halisi! Njooo nazo kitaa utalia!
Naamini kuna siku utakuwa mstaarabu na kuniomba radhi kuyaita maarifa yangu ambayo ni mchanganyiko wa kila aina ya elimu na uzoefu "bla bla".

Na pia sijui ni kitaa kipi unakizungumzia. Unadhani mimi ni hayawani kumshauri mtu kitu ambacho sikiishi mkuu. Kweli alichosema Putin. Tatizo kubwa la wa - Afrika ni wao wenyewe.

Naamini mleta maada hana mtazamo dhaifu kiasi cha kupuuza anayoshauriwa kwa kuwa ni ya " darasani".

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wateja wa kuku ingekuwa wana ushirikiano ni biashara nzuri sana ila wateja sijui huwa wakoje yaani. Ukipiga gharama ya kumkuza kuku hadi anafika siku ya kuuzwa inaweza kuwa 5000 alafu utakuta kuna mtu anauza 4700! Huwa wanaharibu soko wenyewe kabisa. Inabidi wafike sehemu wawe kama wauza mafuta bei ikipangwa hakuna anaeshuka chini ya bei ng'o!

Sasa utakuta mama kaanzishiwa mradi wa kuku na mumewe na bado mumewe ananunua chukula na madawa siku ya kuuza mama anauza hata 3500 tu mradi anapewa milioni 2 ya pamoja anaona nyiiingi kisha anaenda kwa mumewe tena kuomba hela ya vifaranga wapya na kwa kuwa Mr yuko TRA au Vodacom meneja wa kitu fulani shida yake ni kuona mama yuko busy hakai bure anampa tu. Sasa wewe anza na Kroiler wako watano hao uje ufurahie shoo kwenye market
Tatizo tunapuuza sana "ushirika" baina ya wafugaji. Ni kitu muhimu sana kwani huwasaidia kuwa na bei ya pamoja na pia kuongeza bargaining power kwa suppliers. Hii ni ukiwa ushirikiano utawekwa vema.

Kwa mfano. Kwa huku Kyela mfuko mmoja wa kg 50 wa complete layers mash ya Silverlands inauzwa elfu 58 Nilipoanzisha ushirika na jamaa yangu na kufanya manunuzi/mauzo kwa pamoja tukaweza kumshawishi muuzaji kutushushia bei na sasa tunanunua kwa elfu 54 kwani frequency ya kununua kama mteja mmoja imeongezeka.

Kabla ya hapo mimi nilikuwa nikinunua kwa frequency ndogo na jamaa yangu hakuwa akitumia hizo commercial feeds. Sasa unaweza ona hapo mimi nimenufaika na kushuka kwa bei. Jamaa yangu kanufaika kwa kuongeza mazao ya kuku wake (utagaji).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo tunapuuza sana "ushirika" baina ya wafugaji. Ni kitu muhimu sana kwani huwasaidia kuwa na bei ya pamoja na pia kuongeza bargaining power kwa suppliers. Hii ni ukiwa ushirikiano utawekwa vema.

Kwa mfano. Kwa huku Kyela mfuko mmoja wa kg 50 wa complete layers mash ya Silverlands inauzwa elfu 48 Nilipoanzisha ushirika na jamaa yangu na kufanya manunuzi/mauzo kwa pamoja tukaweza kumshawishi muuzaji kutushushia bei na sasa tunanunua kwa elfu 54 kwani frequency ya kununua kama mteja mmoja imeongezeka.

Kabla ya hapo mimi nilikuwa nikinunua kwa frequency ndogo na jamaa yangu hakuwa akitumia hizo commercial feeds. Sasa unaweza ona hapo mimi nimenufaika na kushuka kwa bei. Jamaa yangu kanufaika kwa kuongeza mazao ya kuku wake (utagaji).

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwanzoni mlikuwa manunua Kwa elfu 48 sasa mmepunguziwa ni elfu 54 au sijaelewa?
 
Nakushauri. Nimefuga kuku kwa zaidi ya miaka 10. Gharama kubwa ziko kwenye chakula. Na bei huwa zinapanda sana na hazieleweki. Cha kwanza pata eneo la kutosha. Ifahamike kuwa sheria itakuja kuwabana wafugaji wa mijini kuhusu eneo la kufugia tafuta kuanzia hekari 5.

Pia utaweza kupunguza gharama za chakula kwa kuotesha baadhi ya vitu vinavyohitajika ikiwa ni pamoja ma majani kama mlonge au lukina au mulberry. Pia kama ni wa kienyeji utaweza kuwatoa nje wajitaftie.

Cha pili jenga banda ambalo litapunguza magonjwa na hivyo kukupunguzia matumizi ya madawa.

Cha tatu ili mradi wa kuku ukupe faida nono uunganishe na miradi mingine mfano mradi wa bustani na uzalishaji wa biogas au miradi mingine inayohusiana. Hapa nitaweka kiambatanisho cha kuonyesha mfumo wenyewe ukoje.

Chakula kinachukua asilimia kubwa sana hivyo ni vyema mfugaji akawa na stock ya kutumika muda mrefu au akaagiza moja kwa moja kutoka kiwandani ikiwa anafuga kwa kiwango kikubwa.

Screenshot_20200405-095156.png
 
Write your reply. Hongera kwa kuweza kuaanza kufuga. ushauri wangu ninkuwa ungeanza na kuku wa lika moija (the same age) ua hapo wangeanza kutaga wakauyu mmoja na hapo ugeweza kupata tray 1.5 kila siiku. kama unaweza kuanza upya anza na kuku 100.
 
Write your reply. Hongera kwa kuweza kuaanza kufuga. ushauri wangu ninkuwa ungeanza na kuku wa lika moija (the same age) ua hapo wangeanza kutaga wakauyu mmoja na hapo ugeweza kupata tray 1.5 kila siiku. kama unaweza kuanza upya anza na kuku 100.
 
Back
Top Bottom