Msaada: Ndoa bila idhini ya wazazi inawezekana?

fiksiman

JF-Expert Member
May 17, 2008
402
104
Jamani naombeni msaada wa kisheria na hata ushauri. Nataka kuoa mtoto mmoja wa Kiunguja ila wazazi wake na familia yake haitaki kwasababu mi natoka Bara na pia ngozi yangu nyeusi (huyo mtoto ni mwarabu). Sasa wameanza juhudi za kumtafutia Mume.

Huyo mtoto yuko tayari kutoroka kuja kuishi na mimi, sasa nataka kujua kama naweza kumuoa bila idhini ya wazazi wake au ndugu maana hakuna njia nyingine na ameniambia ikishindakana basi yeye bora atangulie kaburini kuliko kuolewa na Babu mwenye wake wanne.

Kwa taarifa mimi ni muislam.

Mwenzenu katika Mashaka
Fiksi.
 
Jamani naombeni msaada wa kisheria na hata ushauri. Nataka kuoa mtoto mmoja wa Kiunguja ila wazazi wake na familia yake haitaki kwasababu mi natoka Bara na pia ngozi yangu nyeusi (huyo mtoto ni mwarabu). Sasa wameanza juhudi za kumtafutia Mume.

Huyo mtoto yuko tayari kutoroka kuja kuishi na mimi, sasa nataka kujua kama naweza kumuoa bila idhini ya wazazi wake au ndugu maana hakuna njia nyingine na ameniambia ikishindakana basi yeye bora atangulie kaburini kuliko kuolewa na Babu mwenye wake wanne.

Kwa taarifa mimi ni muislam.

Mwenzenu katika Mashaka
Fiksi.


Kwanza ningependa kujua kutoka kwako.......je wewe ulishawahi kuoa au kuishi na mwanamke? umeshawahi kuwa na mtoto?
 
Sijawahi ndo nataka kuanza maisha mkuu. Na sio siri nampenda sana huyo mtoto niko tayari kwa lolote ilimradi awe mke wangu
 
Sijawahi ndo nataka kuanza maisha mkuu. Na sio siri nampenda sana huyo mtoto niko tayari kwa lolote ilimradi awe mke wangu

Asante kwa kujibu.

Je umeshawahi kumuona? namaanisha mmewahi kuonana na kuishi pamoja au unampenda kwa kuona picha kwa kusikia sauti tu?
 
Sijawahi ndo nataka kuanza maisha mkuu. Na sio siri nampenda sana huyo mtoto niko tayari kwa lolote ilimradi awe mke wangu


Chukua mtoto huyo nenda kaoe,, kama ametimiza umri wa kuolewa. Ndoa ni mkataba kati ya watu wawili, mke na mume.....na mashahid wawili. Kisheria hawawezi kukushtaki, na baadaye wataelewa tu. Ila kiislamu sijui sana maana mimi sio muislamu, ila unaweza kutengwa kama ndoa inahitaji idhini ya wazazi....unajua zaidi, lakini move on!
 
mkuu fiksi vipi yule unaye-share na jini! umemuacha au ndio huyu huyu? kwa hiyo umefanikiwa kumthibiti yule jini!?
mpe mimba then wazazi wataridhia tuu
 
Kwa vile nyote ni waislamu mntakiwa kwenda ofisi ya kadhi kwa kule zanzibar mtatowa maelezo yenu na wazee watatoa maelezo yao mbele ya kadhi iwapo maelezo ya wazee hayana nguvu ni ya kibaguzi tu! Basi kadhi anayo mamlaka kufungisha ndoa hatakama walii wake hataki.
 
Sijawahi ndo nataka kuanza maisha mkuu. Na sio siri nampenda sana huyo mtoto niko tayari kwa lolote ilimradi awe mke wangu

We fiksi nawe,

Muoaji wewe! Muolewaji yeye (na yuko tayari), sijui nini kimebaki... If you are really serious then oa!! But incase lolote likitokea badae ujue ni at your own risk!!

Butua uwaokoe wenzio

.....Dad:)
 
mkuu fiksi vipi yule unaye-share na jini! umemuacha au ndio huyu huyu? kwa hiyo umefanikiwa kumthibiti yule jini!?
mpe mimba then wazazi wataridhia tuu

Huyu huyu mwana ila kuna wadau wamenipa ushauri wa namna ya kumkabiri...ni ushauri unaotoa moyo. Mi bwana nasonga front lolote na lliwe. Maisha ni kuchukua hatari.
 
kwa vile nyinyi ndio mtakao ishi pamoja na kukabiliana na ndoa yenyu wakati wote wa raha na shida basi wao hawana huwezi wa kusimamisha ndoa yenu.kwahio kusiwe kipingamizi kabisa fanya mpango mtoto aje bara umuoe muishi pamoja na mungu hawajalie ndoa yenu hidumu na hawaepushe na matatizo yoyote ambayo ndugu zake wataleta.kila kheri muheshimiwa .
 
kwa vile nyinyi ndio mtakao ishi pamoja na kukabiliana na ndoa yenyu wakati wote wa raha na shida basi wao hawana huwezi wa kusimamisha ndoa yenu.kwahio kusiwe kipingamizi kabisa fanya mpango mtoto aje bara umuoe muishi pamoja na mungu hawajalie ndoa yenu hidumu na hawaepushe na matatizo yoyote ambayo ndugu zake wataleta.kila kheri muheshimiwa .

Ndugu yangu ndo maana nataka ushauri wa kisheria maana sipendi kuishi na mwanamke kinyumba, isitoshe mtoto mwenye sala tano nitamtia dhambi bure maana yuko tayari nifanye lolote hapa naposema sijamgusa baada kugundua ni bikra. Nataka nichukue jumla ndo nikapasue kwenye honeymoon. kiufupi am madly in love with her. Huyo mtoto ni wa pwani kweli kweli maana hajui hata kukasirika.
 
Hakuna ndoa isiyokuwa na baraka za wazazi ikadumu kuwa serious man

Kwani wazazi ndo wanaotufanya tupendane hadi bila wao tusidumu. Narudia nataka ushauri wa kisheria sio hisia kama hizi kwa kweli hazitanisaidia kabisa. Sawa na kunaniambia nile wali bila kunywa maji au kimiminika cha kusukumia. kama yupo anayejua sheria hasa kwa upande wa uislam unasemaje katika suala kama hili.

Je inawezekana msichana kujipa idhini mwenyewe, weka na mandiko au hadithi za manabii zinasemaje kuhusu jambo hili. Tutapata athari gani endapo tutaendelea na adhma yetu ya kuishi pamoja bila wazazi kutoa hiari yao?
 
Back
Top Bottom