Msaada: Naweza kupata magari binafsi yatakayoniwezesha kufika Mwanza ikiwa nitapanda saa tisa alasiri?

kalua 89

Member
Sep 22, 2020
54
30
Kwa imani natumaini kuwa wote tu wazima! Wakuu niko DSM na nimepata dharura ya kwenda Mwanza hivyo kulingana na dharura yenyewe sitaweza kupanda mabasi ya asubuhi ili angalau niweke mambo sawa kidogo kisha niondoke na zaidi ni kwamba natakiwa kuwa Mwanza kabla ya saa tatu asubuhi siku ya kesho.

Sasa nauliza naweza kupata magari binafsi yatakayoniwezesha kufika Mwanza ikiwa nitapanda magari hayo saa tisa au kumi alasiri? Na ni wapi naweza pata magari hayo kwa urahisi? Naombeni kusaidiwa wakuu kwa wale wenye uzoefu wa kusafiri na magari binafsi.
 
Hata gari za IT azitembei kwa mwendo huo unaotaka wew panda treni mpya ya Magufuli labuda.
 
Mode of transport hapo ni ndege, hakuna chombo hapo kinaweza kuwa na kasi uitakayo kufika mwanza zaidi ya ndege.
 
Mode of transport hapo ni ndege, hakuna chombo hapo kinaweza kuwa na kasi uitakayo kufika mwanza zaidi ya ndege
Mara nyingi mabasi yanatembea masaa 16-18 kwahiyo nikawa nafikiri kwamba nikipata gari binafsi na vile inatembea usiku pia naweza tumia hayo masaa kufika Mwanza mkuu ndio maana najaribu hiyo njia
 
Ata gari za IT azitembei kwa mwendo huo unaotaka wew panda treni mpya ya Magufuli labuda.
Napigia hesabu kuanza safari leo mkuu ili kufikia kesho asubuhi niwe nimefika yaani nikianza safari leo saa kumi basi nisitumie zaidi ya masaa 18 njiani.
 
Kwa imani natumaini kuwa wote tu wazima! Wakuu niko DSM na nimepata dharura ya kwenda Mwanza hivyo kulingana na dharura yenyewe sitaweza kupanda mabasi ya asubuhi ili angalau niweke mambo sawa kidogo kisha niondoke na zaidi ni kwamba natakiwa kuwa Mwanza kabla ya saa tatu asubuhi siku ya kesho.

Sasa nauliza naweza kupata magari binafsi yatakayoniwezesha kufika Mwanza ikiwa nitapanda magari hayo saa tisa au kumi alasiri? Na ni wapi naweza pata magari hayo kwa urahisi?. Naombeni kusaidiwa wakuu kwa wale wenye uzoefu wa kusafiri na magari binafsi.
Kwa nini unaogopa kupanda ndege.
Zipo kwa ajili hiyo.
 
Mkuu Sogea mbezi Mwisho gari yoyote inayoenda njia ya Dodoma panda nenda kwa kuungaunga. Ukipata hata IT za Burundi na Rwanda panda utashukia Tinde utatafuta kuungaunga mpaka mwaza . Safari njema ila jitahidi angalau saa nane uwe mbezi.
 
Mkuu Sogea mbezi Mwisho gari yoyote inayoenda njia ya Dodoma panda nenda kwa kuungaunga. Ukipata hata IT za Burundi na Rwanda panda utashukia Tinde utatafuta kuungaunga mpaka mwaza . Safari njema ila jitahidi angalau saa nane uwe mbezi.
Sawa mkuu ngoja nitajitahidi kufika hiyo mida
 
To Mwanza & Mbeya nenda ubungo maji mbele ya jengo la Tanesco Kuna gari zinakuja zinasimama na kupakia saa zingine Hadi kwa zamu hizi nyingi n xile zinasafirishwa kwenda nchi jirani Kama Zambia, Congo DRC, Rwanda & Burundi hata pale oilcom ubungo mchana gari zinaingia nakuuliza abiria.

Kwenda Moshi & Arusha ukikosa saibaba, harambee au Lim safari nenda ubungo oil com kuanzia jua linapotoka Hadi usiku saa tano gar la mwisho n la gazeti saa sita kasoro usiku

Ukiwa Arusha au Moshi kwenda dar & tanga ukikosa saibaba, Lim safari au harambee basi nenda himo njia panda Kuna gari ndogo zinakuja pale pia Kuna Costa za kupakia kwazamu Hadi saa nne pia Kuna basi la kutoka Nairobi Hilo linaitwa zoa zoa juz nimewapa 10k likanileta DSM na kurudi nategemea saibaba niwape 7k wanishushe Ars
 
Back
Top Bottom