Msaada: Nataka kwenda Kenya

My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Wakuu habari,

Nilipoteza passport yangu ya international sasa bado sijapewa nyingine.
Sijawahi kufika Kenya, nataka kwenda kesho nina shida muhimu sana Nairobi.

Sasa nataka kujua endapo naweza kwenda bila passport sababu ya ujirani wetu mwema au ni lazima niwe na passport hata ya muda mfupi.

Nawasilisha wakuu.
 
Lazma uwe na temporary passport
Nashukuru Kwa msaada mkuu
Wakuu habari.
Nilipoteza passport yangu ya international sasa bado sijapewa nyingine.
Sijawahi kufika Kenya, nataka kwenda kesho nina shida muhimu Sana Nairobi.
Sasa nataka kujua endapo naweza kwenda bila passport Sababu ya ujirani wetu mwema au ni lazima niwe na passport hata ya muda mfupi, nawasilisha wakuu.
 
Mkuu hakuna kitu kizuri Kama Uhuru, Uhuru ni mambo yote, Kwa nini niende Kwa mashaka? Acha nitafute hiyo temporary passport, nimeambiwa ni elfu 30 tu
Unataka kuibiwa punda wewe,, tangu lini hiyo ya kijikaratasi ikawa elfu 30? Mbona hiyo huwa ni elfu 10 tu?
 
Kama huendi kukaa muda mrefu, nenda ukifika mpakani useme wewe ni mfanyabiashara na kuna kitu unaenda Kununua. Watakupa karatasi ya kukaa kule ndani ya siku 14 tu ambayo utailipia sh 5,000 ambayo ukilipishwa kwa hela ya Kenya ni ksh 200 tu.

Siku 14 hizo zikiisha ukiwa kule, kama wewe hupendi kuishi kwa wasiwasi na unataka kuendelea kukaa kule kwa muda zaidi unaenda Nyayo kwenye ofisi zao pale Nairobi.
Ila kwa sababu wewe ni mtanzania sioni haja ya kujihangaisha kwenda kuongeza muda kwasababu polisi wa kule huwa wanawauliza sana wasomali mambo ya I'D sababu ya kutamhulika kwa sura zao
 
Mimi nataka kupitua njia ya panya kwa sababu kuu moja, naenda kununu mbegu ya ng'ombe wa maziwa ( mbegu ya kupandikiza kwa njia ya chupa) najua fika nikipitia njia halali huo usumbufu wa wizara ya kilimo na mifugo, mkemia mkuu,....acha nifanye magendo tu maana hakuna namna!
 
Unataka kuibiwa punda wewe,, tangu lini hiyo ya kijikaratasi ikawa elfu 30? Mbona hiyo huwa ni elfu 10 tu?
Kwa mara ya mwisho nilitenfeneza ya kijikaratasi ya miezi mitatu Tsh 6 elfu na ni baada ya kuipoteza ile ya karatas ya afrika mashariki na kati ambayo ilini cost 17 elfu kua makini kwani kwenye 30 unaongeza ngapi kupata mkoba permanent?
 
Mimi nataka kupitua njia ya panya kwa sababu kuu moja, naenda kununu mbegu ya ng'ombe wa maziwa ( mbegu ya kupandikiza kwa njia ya chupa) najua fika nikipitia njia halali huo usumbufu wa wizara ya kilimo na mifugo, mkemia mkuu,....acha nifanye magendo tu maana hakuna namna!
DUH! HAYA..
 
Kwa mara ya mwisho nilitenfeneza ya kijikaratasi ya miezi mitatu Tsh 6 elfu na ni baada ya kuipoteza ile ya karatas ya afrika mashariki na kati ambayo ilini cost 17 elfu kua makini kwani kwenye 30 unaongeza ngapi kupata mkoba permanent?
Ilikuwa Mwaka gani huo?
 
2011 tarehe kama ya leo mkuu tena unajua kilichonisibu kaka? Niulize nikuhadithie kwa undani
Miaka 6 imepita mengi yamebadilika siku hizi ni 10000 na hakuna tena zile karatasi za kutolewa pale mpakani, ila ni vyema pia ukiadithia itatusaidia
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom