Msaada natafuta kazi nina Elimu ya Certificate in Community health

Goldenboy24

Member
Aug 11, 2021
29
5
Habarini wakuu kama kichwa cha habari kinavosema mimi ni kijana mwenye miaka 22 nimesoma hadi ngazi ya certificate in community health

Natafuta kazi katika mashirika binafsi (NGO) yanayoshughulikia masuala ya kijamii hata Kwa kujitolea kwa ujumla naweza fanya kazi kama social worker pia

Mbali na ujuzi huo pia nilishawahi fanya Sales and marketing kwenye kampuni flani Kwa muda wa miezi 6 Kwa iyo nina uzoefu wa kazi hii pia

Asanteni naamini mtanipatia connection wana Jf Asanteni
 
Kaombe kazi kama medical attendant hospitalini utapata tena kwa asilimia 100...matajiri uchwara wengi wanapendelea kuwaajiri medical attendants kwa sababu huwa hawaitaji mishahara mikubwa....
 
Vipi kwa waliosomea certificate ya uongozi na usimamizi pia??

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
Omba ajira za utendaji wa vijiji....lakini pia usisite kuomba ajira zinazohusiana na masoko hasa kwenye makampuni..mtu aliesomea uongozi na usimamizi anaweza pia kusimamia biashara au kutafuta masoko ya biashara husika
 
Omba ajira za utendaji wa vijiji....lakini pia usisite kuomba ajira zinazohusiana na masoko hasa kwenye makampuni..mtu aliesomea uongozi na usimamizi anaweza pia kusimamia biashara au kutafuta masoko ya biashara husika
Sawa mkuu tatizo hata kupatikana kwake ningumu yani kwa hizo kazi

Sent from my TECNO K7 using JamiiForums mobile app
 
Wacha kutuambia habari za Elimu taja uzoefu wako ulifanya kazi wapi na wapi na Kwa muda gani?
 
Dah! Nimechelewa kusoma ujumbe huu, jingekwambia ujaze maombi online kwa watu wa MHD wametoa kazi nyingi sana na deadline bila shaka ni leo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom