Msaada: Napataje AVN na ikiwa nilishawahi unda account lakini taarifa zake nilipoteza?

Ndugu Watanzania wenzangu,

Naombeni msaada wa kuweza kutimiza ndoto zangu.

Nilihitimu Diploma ya Kilimo mwaka 2015 Mbeya kwenye chuo kilichojulikana kama Ilemi Polytechnic College ambacho kilikuwa na usajili wa namba REG/BMG/031, chuo hicho ni miongoni mwa vyuo ambavyo vimefutiwa usajili miaka ya hivi karibuni. Sasa kwa kipindi hiki nilitaka kuendelea na masomo ya degree.

Lakini katika harakati za kutaka ku_apply chuo nikagundua kuna kitu kinaitwa AVN baada ya harakati za kufuatilia ndipo nikajua kwamba chuo hakikuwahi kuwasilisha taarifa za matokeo NACTE. Hapo ndipo nikawa njiapanda hadi wakati huu sijui nifanye nini.

Naombeni ushauri kutoka kwenu ndugu maana naamini hapa wapo wataalamu wa masuala haya ambao wataweza kunishauri vema.

Ahsanteni.
 
Pole sana, hapo uwezekano wa kudahiliwa degree haupo. Cha kufanya soma upya Diploma kwenye chuo kinachoeleweka.
 
Nimejaribu kufanya nao tena mawasiliano kwa njia ya email na hivi ndio wamenijibu

1627386532930.png


"Huna matokeo kwenye mfumo, na pia vyeti vyote vya kilimo hutolewa na wizara ya kilimo."
---
sasa wamenichanganya zaidi wanaposema vyeti vyote vya kilimo hutolewa na wizara ya kilimo wakati chuo nilichosoma ni private na sio government.
 
Kwanza cheki cheti chako kimetolewa na nani. Na pili je una transcript? Kama ni kweli kilimo basi waone hao uwalilie shida yako. Kama sivyo basi kimbia haraka Nacte.
 
Wakuu naombeni msaada.
Zaidi ya mwezi nafuatilia AVN lakini hakuna mabadiliko, lila nikirequest naambiwa bill generated waiting for control number.

Nimeishazunguka sana pale NACTE ila hakuna ufumbuzi wa tatizo. Hadi watu wa GePG nimewapigia Nawao wanasema hii ni kwao NACTE wala wao hawahusiki.

Sijui nifanyeje ili niweze kuendelea na masomo japo siku za kuapply zimebaki chache.
Kama kuna mtu anaweza kunisemea ili nisaidike nitashukuru sana 🙏

20210827_175540.jpg
 
Wakuu naombeni msaada.
Zaidi ya mwezi nafuatilia AVN lakini hakuna mabadiliko, lila nikirequest naambiwa bill generated waiting for control number.

Nimeishazunguka sana pale NACTE ila hakuna ufumbuzi wa tatizo. Hadi watu wa GePG nimewapigia Nawao wanasema hii ni kwao NACTE wala wao hawahusiki.

Sijui nifanyeje ili niweze kuendelea na masomo japo siku za kuapply zimebaki chache.
Kama kuna mtu anaweza kunisemea ili nisaidike nitashukuru sana

View attachment 1911374

Anza upya,
 
Wakuu naombeni msaada.
Zaidi ya mwezi nafuatilia AVN lakini hakuna mabadiliko, lila nikirequest naambiwa bill generated waiting for control number.

Nimeishazunguka sana pale NACTE ila hakuna ufumbuzi wa tatizo. Hadi watu wa GePG nimewapigia Nawao wanasema hii ni kwao NACTE wala wao hawahusiki.

Sijui nifanyeje ili niweze kuendelea na masomo japo siku za kuapply zimebaki chache.
Kama kuna mtu anaweza kunisemea ili nisaidike nitashukuru sana

View attachment 1911374
Kama upo Dar/Karibu na Dar fika ofisini kwao, hawa watu wanahitaji kufuatwa huko ndipo utatuliwe shida yako
 
Kama upo Dar/Karibu na Dar fika ofisini kwao, hawa watu wanahitaji kufuatwa huko ndipo utatuliwe shida yako
Nimeishaenda mara kadhaa lakini sikupata ufumbuzi.
Mara ya mwisho mdada aliniambia control number zinasumbua niwe na subira.
Inaonekana hawajui namna ya kusolve hili tatizo, sina imani nao kabisa.
 
Anza upya halafu kwenye namba ya chuo usiandike andika NS... ikifuatiwa na namba ya fom 4
Mf. NS1234/0000/0000
Unamaanisha nianze upya kulogin au.?
Kwasababu nimejaribu ila imekataliwa hii ni kutokana na username na password wanakutumia wenyewe kwenye email na unakuwa unaitumia hiyo tu.
 
Back
Top Bottom