Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Ninampango wa kuuza bidhaa mbali za electronics kama vile simu za mikononi, laptop, flash disk, camera n.k. Ili niweze kufanikisha hilo ninaombeni msaada wenu kwa yeyote mwenye ufahamu juu ya soko la bidhaa za electronics hasa zile za IT ambazo zinafanya vizuri katika soko la Tanzania na zinazouzika kwa haraka. Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa yeyote ambaye atajitokeza kunisaidia katika hili.
Habari Wapambanaji.
Nina wazo la kuanzisha duka la vifaa vya umeme wa majumbani na baadhi ya vifaa vya viwandani.
Vifaa vya majumbani kama vile.. Taa, switches, conduits pipes, cables, wires, earth roads, circuits breakers, junction boxes, square boxes, distribution boards nk.
Vifaa vya viwandani kama. Magnetic Contactors, timers, relays, CBs push button switches nk.
Pia katika duka hilo natarajia niwe natoa na huduma za kusuka starters kwa wale wahitaji kwakuwa nina ujuzi wa ku design circuits mbalimbali kama za DOL, YD, Jogging, Forward and reverse nk. Nimeongea na bank moja kwamba naweza kupata mkopo wa angalau 35m.
Je hiyo inatosha au naweza ku fail katika biashara hiyo. Nipo katika Wilaya moja ambayo inakuwa sana kiuchumi na kazi za viwandani ni nyingi sana.
Ushauri please.
Habari wana jamvi,
Mimi ni kijana niliedhamiria kujiajiri, hivyo biashara niipendayo na niliyokua naifikiria kwa muda mrefu ni hii ya uuzaji wa ELECTRONIC DEVICES; Used or New [Simu, Laptops, Camera za Digitali, iPads, iPods, etc].
Sasa ishu ni kwamba, kwanza sina Tathmini, pili sina uzoefu wa kutosha. Please mwenye uzoefu wa katika deal kama hizi anisaidie, hasa ni mahali gani kwa hapa Africa naweza nunua mzigo, usafirishaji [ikiwezekana njia za panya].
Pia market kubwa ni wapi hapa Tanzania? Mtaji ni kama Mil 4 mpaka 5..
Ahsante..
Baadhi ya maoni ya Wadau wa JamiiForums
Soko si hoja biashara matangazo na ubora kama laptop ni vyuoni zaidi na miezi mizuri ni ile ya kufungua vyuo vikuu (Sept/Oct kila mwaka)
Kuhusu vifaa vingine vya electronic ni kazi kwani kila kifaa kinategemeana na kazi husika na ndipo upeleke na hakuna soko moja kwa bidhaa zote za electronic lakini sehemu kubwa ni katika tasisi za ELIMU YA JUU YAANI VYUONI
Sehemu chache sana nje ya watu walioko chuoni kununua vifaa hivyo maana vingine vinahitaji uelewa wa jinsi ya kuvitumia.
Na lazima uwe na Ofisi ya Kudumu ili wanapopata tatizo juu ya kifaa ulichowauzia uwape maelekezo au uwape kingine/vingine kwa vyenye garantii.
Na pia ufanye market survey ili uuze bei pungufu na ili vitoke mapema badala ya kuuza kwa bei juu wanaweza aamua kufuata sehemu ya karibu na kwenda kununua mahitaji mengine ya electronics
Nimefanya utafiti wa vifaa hivyo vya electronic unavyokusudia kufanya biashara, kwa upembuzi wangu yakinifu ni bora jaribu kufanya utafiti wa kutosha usije jutia kuweka mtaji katika biashara ambayo soko lake limeshakaliwa na wengi.
Kila kona na hasa mitaa mingi mijini imejaza vifaa vya electronic kwa sana tu. Kariakoo ndo usiseme. Mwenyewe nilikuwa nafanya utafiti wa kuanzisha biashara hiyo nimeona ni kupoteza mtaji wangu bora nibuni kitu kingine.
Wengi wenye biashara hiyo wana mikataba na makampuni husika, hivyo huuza vitu kwa bei ya chini, sasa we ukiamua kununua vitu kwa njia za panya unaweza kushtukia unawajibika kuuza kwa bei mbaya kuliko hao wanaoletewa na makampuni.
Kwa ujumla vifaa vya electronics hakikisha umefanya utafiti wa kutosha na eneo gani linafaa vinginevyo ushindani ni mkubwa sana. Ila unaweza kupata eneo ambalo halina ushindani ukawa na biashara nzuri na hasa kama una bidhaa za kiwango ambacho wenye pesa wanataka unaweza kufanya biashara nzuri tu.
Mimi naamini mkopo ni kwa ajili ya kuendeleza/kukuza biashara. Sio kuanzisha biashara.
Lazima ujue biashara yako Ina mzunguko kiasi gani, wateja ni wakina nani, kipi hasa kinatoka zaidi.
Lakini pia biashara sio kujaza duka/kupendezesha ila kuwa na mzunguko mkubwa ulioambatana na ushawishi wa lugha nzuri kwa wateja.
Ukishakuwa na wateja kiasi huwezi kumudu kuwahudumia kutokana na uchache wa mtaji wako hapo ndipo wazo la kuchukua mkopo huja, maana tayari watu wa kuwauzia bidhaa zako unao.
Ila kuanza mtaji na mkopo ni risk sana, kwa kuwa inachukua muda kiasi kuanza kuiona ile faida halisi kwenye biashara mpya. Kumbuka hapo wateja bado hujapata wa kutosha na marejesho yanahitajika. Hivyo ikitokea biashara haijachangamka kwa haraka ni rahisi wewe kufilisika na kubaki na Deni juu.
Mimi ni hayo tu mkuu. Wazo lako la biashara ni nzuri.