Msaada: Naomba kufahamishwa namna ya kuwadhibiti mende

Mwite mmoja na umwambie kwa lugha kistaarabu tu kuwa wanatakiwa kuhama hivyo awataarifu na wenzake. Wape na muda kama wiki 2 ili wapate nafasi ya kuhamisha familia zao. Mende ni waelewa naamini watakuelewa na wataondoka wenyewe.

Wakigoma wapeleke mahakamani.
 
Hata Kama ni msafi jitahidi kumwaga dawa kwenye shimo la maji ya vyombo jikoni ndo wanazaliana huko.
 
Straight to the point.

When we were growing up, tulizoea kuona Yale ma mende makubwa makubwa flani ambayo in those times we thought they were originated from the lavatories.

Ila kwa sasa kuna hivi vi periplaneta americana vidogovidogo hivi vinasumbua balaa. Ukichek chini ya sofa au sehemu nyingine za maficho ni balaa.

Maajabu yake sasa mchana huwaoni, lala usiku halafu ingia sebuleni ghafla washa taa uone mambo vinakufanyia. Vinaanza kwanza toka nduki. Seriously mwenyewe kujua solution yao please.
Mabaki ya chakula yanasababisha mende na hasa kama unakula chakula kwenye makochi.
 
Ndo faida ya kuoa mkuu. Nyumba yake mwanamke.

Hapo solution ni usafi,manake hata ukipiga dawa ikiisha watarud tena kama hapo si pasafi
Unaongelea Hawa wanawake walevi tunaoshinda nao sehemu za starehe na wwnakunywa pombe kushinda baba zao ? Nyumba ni usafi tu iwe ya mwanaume au mwanamke, Hawa wanawake wa siku hizi mzee utaishia kujifulia kila kitu.

Kuna mmoja humu alikuwa anasimulia anavyoipenda Kvant duh nikaona basi tumekwisha.
 
Unaongelea Hawa wanawake walevi tunaoshinda nao sehemu za starehe na wwnakunywa pombe kushinda baba zao ? Nyumba ni usafi tu iwe ya mwanaume au mwanamke, Hawa wanawake wa siku hizi mzee utaishia kujifulia kila kitu.

Kuna mmoja humu alikuwa anasimulia anavyoipenda Kvant duh nikaona basi tumekwisha.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Pole mkuu
Kosa la mmoja sio wote,kuna wengine wasafi mno hujakutana nao tu
 
hiyo fursa mkuu,Kama wapo hapo kwako ,waandalie mahali ambapo unaweza ukawavuna kirahisi.wanauzwa Bei ghari Sana hao.
 
Fanya usafi kisha itafute hii sumu ya Mende,hii ni powder unaweka pembeni yaani ukutani,hii kitu 100% itamaliza tatizo lako ila usisahau kufanya usafi na kutokubakisha mabaki ya chakula ndani.

View attachment 1822488
Hii dawa ni nzuri sana mende hawachomoki hapo,ukitaka kuwatokomeza kabisa ,kabla ya kuweka hiyo dawa hakikisha hupiki chakula au huleto chakula hapo ndani kwa siku nne,namaanisha ukale hotelini,halafu usiache maji yaliyowazi funika au yaondoe,baada ya hizo siku nne wawekee hiyo dawa uliyoonyeshwa hapo na mdau kwenye kona zao,hakika utawamaliza wote.
 
Kuna dawa zinauzwa kwenye vipaketi vya kijani Tsh buku buku... Nunua mwaga sehemu tofautitofauti ndani utawaona wanakuja mbiombio kula na baada ya siku chache hutowaona tena.

Hivo vidawa huwa vinapendwa sana na mende ila wakila ndio mwisho wao... Utawakuta wamekufa kifo cha mende
Jina la dawa tafadhali
 
Hivo vidude nilikua navyo Mbagala aisee. Kuna uwezekano umevipata kutoka kwa jirani yako ila kwako vimekuja kwasababu kuna mazingira rafiki. Punguza vitu ndani, usafi, usiache mabaki ya chakula usiku, na mzee baba OA au tafuta girl awe anasimamia show ya usafi.
Na mimi nilitaka kusema kama wako sehemu yote mpaka kwa majirani, kuwadhibiti vigumu hapo.

Utadhibiti kiasi kwa usafi, lskini wanaweza kuja kutoka kwa jirani.
 
Jina la dawa tafadhali
Inaitwa Green leaf powder.

Picha hii hapa
images (32).jpeg
images (33).jpeg
 
Back
Top Bottom