Msaada: Namtafuta Carlos Sendwa

Lekanjobe Kubinika

JF-Expert Member
Dec 6, 2006
3,020
576
Jamani naomba anayejua mtu huyu alipo anisaidie kumpata. Anaitwa Mr Carlos Sendwa, alisoma PCB sekondari ya Pugu STream G 1980-82. Wakati huo mimi nilikuwa PCB stream F, mwenyeji wa Mbeya. Wazazi wake walikuwa wanaishi Mikocheni (?), ni mhehe wa Iringa.

Tulipoteana kiaina hata sielewi, enz hizo hakukuwa na urahisi wa mawasiliano kama sasa. He was a very good friend of mine. Siku moja nadhani 2002 niliwona maeneo ya Muhimbili akitoka kupitia geti la MUHAS, nilikuwa kwenye daladala na sikufanikiwa kumshawishi konda asimame nishuke kumwona huyu bwana, niliporudi nikakuta ameshaondoka, nadhani alipanda daladala.

Why important now? Ihave remembered this friend so much that I feel it fair to start tracing him through this platform. Nikijua yuko wapi lazima tutafanya kila njia tukutane na angalau tusalimiane. Nimesoma nao watu wengi lakini this guy was special of his kind.

Do me a favour, please. Namshukuru mwana JF mmoja aliyenielekeza njia ya wapi niweke hili - kama tangazo.

Leka
 
Una bei gani mkuu. si unajua town hapa

Tumsifu Yesu Kristu.
Kwanza wewe ni Paster. Tena Original basi. Unahubiri mapendo, sijakusikia ukihubiri uzuri wa tamaa ya pesa. Bei yake si unajua tena, utalipwa Mbinguni???

Wewe toa tu ulicho nacho unajiongezea hazina Mbinguni. Niambie basi, unamjua huyu mtu?

Leka
 
unamtaka wa nin?
Ebo! Simtaki, namhitaji. Tumepoteana siku nyingi mno na asa nimeanza kumkumbuka. Kumwona nikiwa kwenye daladala ndio kabisa kumeongeza kasi ya kutaka kuonana naye. Ni rafiki yangu na sina tatizo naye. Kwanza jamaa mwenyewe yule si mgomvi kiasi cha kuhofia kuniambia. Labda kama kabadilika. N mbali, tangu 1982!!! Najua pa kuanzia ni hapa.

Geoff, au una mashaka gani nami au naye? JF si mojawapo ya raha yake ni kuwasiliana marafiki? Majina yenyewe sio rahisi kujua hapa, labda ni wewe? Nimeeleza kwa kina, kama ungekuwa ni wewe bila shaka ungevuta picha na ukakumbuka. Hata kama nitasema tuonane wapi kama sio wewe nitajua ntu, maana jamaa hajabadilika sana, hata mimi atanitambua upesi sana. Ni mtani wangu lakini tuliishi kama ndugu zaidi ya rafiki. JKT ilitutawanya.

Leka
 
Ebo! Simtaki, namhitaji. Tumepoteana siku nyingi mno na asa nimeanza kumkumbuka. Kumwona nikiwa kwenye daladala ndio kabisa kumeongeza kasi ya kutaka kuonana naye. Ni rafiki yangu na sina tatizo naye. Kwanza jamaa mwenyewe yule si mgomvi kiasi cha kuhofia kuniambia. Labda kama kabadilika. N mbali, tangu 1982!!! Najua pa kuanzia ni hapa.

Geoff, au una mashaka gani nami au naye? JF si mojawapo ya raha yake ni kuwasiliana marafiki? Majina yenyewe sio rahisi kujua hapa, labda ni wewe? Nimeeleza kwa kina, kama ungekuwa ni wewe bila shaka ungevuta picha na ukakumbuka. Hata kama nitasema tuonane wapi kama sio wewe nitajua ntu, maana jamaa hajabadilika sana, hata mimi atanitambua upesi sana. Ni mtani wangu lakini tuliishi kama ndugu zaidi ya rafiki. JKT ilitutawanya.

Leka
Mkuu ulishampata????
 
Hahaha
Ila watu wana ujasiri. utamtukanaje mtu humjui?
Umeelewa tofauti mkuu,
Kuna movie inaitwa three idiots.
Ila hao kwa vile ni wawili washikaji nikaweka 2.
Ila pia kimtukana nisiyemjua naweza tu🤣🤣🤣 japo sijawahi. Fa mchezo jua hili
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom