Sigara Kali
JF-Expert Member
- May 28, 2017
- 3,623
- 8,428
Wakuu salaam,
Kama mada inavyojieleza,
Miaka ya karibuni hasa kuanzia 2015 mwishoni nimekua mtu nisiyekua na furaha na nikiwa na furaha basi ndani ya siku chache huondoka
labda nieleze kinagaubaga jinsi maisha yangu yalivyo.
Wazazi wangu washafariki almost 16 years ago, tangu wakati huo ndugu ambao nilikua nawategemea wakaanza mizinguo so nikaanza kuishi ghetto tangu nipo form 1 hadi namaliza form 4, then nikachaguliwa kuingia advance so kipindi chote nasoma advance likizo zangu karibia zote zikiishia maghettoni kwa masela kwa sababu kule home sikua na watu ambao wa kuwategemea sana.
Ada nilikua nalipiwa tu na msamaria mwema mmoja.Nimemaliza form 6 nikafaulu kwenda chuo na Mungu si athumani nikapata mkopo kwa 90% nikaanza maisha ya chuo pale SUA, baada ya muda nikaamua kutoka hostel nikapanga ghetto maisha yakaendelea.
Wakati huu nikiri kwamba nilikua mtu mwenye furaha muda wote sikua mtu wa mawazo mawazo. Mwaka 2012 nikakutana na mwanamke barabarani pale mjini Moro yupo na mabahasha yake anatafuta kazi nikamwomba namba, nikaanza kumtongoza mtoto akakubali tukawa wapenzi.
Baada ya muda binti kapata ujauzito nikamwambia atoke kwao (kwa mama mdogo wake) nikaishi nae ghetto kwa amani na upendo. Wakati ana mimba akaitwa interview akapiga fresh, akarudi ghetto, maisha yakaendelea ya furaha, amani na upendo, binti kajifungua salama salimini.
Kumbukeni wakati ana ujauzito nilimfungulia biashara ndogo
baada ya mtoto kutimiza kama miezi 4 hivi mama yake akapata kazi kule alikofanya interview tena kwa mshahara mnono zaidi ya ule wa aupatae mwenye degree. Nikauza baadhi ya vitu vyangu mama na mtoto na ndugu yake wakasafiri hadi kituo cha kazi alichopangiwa.
Wakati huo mimi nishamaliza degree yangu nikaingia rasmi kitaa, kama mnavyojua nchi yetu ina changamoto za ajira, hapo ndo suala la kutokua na furaha likaanza. Nikasafiri hadi kwa mama mtoto nikakaa kwa muda then nikaingia mkoa jirani huku huku lake zone kutafuta mishe nikapata nikaanza kazi na nikapanga chumba, mwisho wa siku ikawa mtihani kulipwa basi kazi ikashindikana nikaondoka kurudi kwa mama mtoto.
Nimekaa kwa mama mtoto mwisho wa siku tukashauriane nikasome inshu ya ualimu ili nikimaliza niajiriwe moja kwa moja tusaidiane maisha. Nikaingia kusoma PGDE ile namaliza tu kusubiri ajira akaingia Rais Magufuli na roho yake mbaya akasitisha ajira za walimu hasa wa arts.
Nikaanza mdogo tena na hali ya kukosa furaha na msongo wa mawazo ikaanza upya, nikaona kukaa kwa mwanamke bila kazi ni noma nikaingia mkoa jirani tena kutafuta mishe nikapata chuo kufundisha, nikaanza maisha.
Sasa kitu kinachoniumiza na kutokua na furaha ni huyu mwenzangu yani sasa hivi naona mapenzi yamepungua sana, mawasiliano ni ya shida yani nisipomtafutaga hewani basi hana muda mimi japo ananisaidia kwa baadhi ya mambo manake mwenzangu ana kipato cha juu sana, lakini naona kunipa ile heshima na kunijali kama mzazi mwenzake haipo.
Nampenda ila anavyonipotezeaga nahisi kutengwa na walimwengu wote,
tangu mwaka Jana sina furaha na nakuwa na msongo wa mawazo ,nilitegemea huyu mwenzangu awe mtu wa kunitia moyo kunifariji katika mihangaiko yangu lakini hilo halipo hata kama ananisaidia lakini hanipi ile heshima yangu kama mwanaume hata kama sina hela naona kwangu ni sawa na bure.
Daily Mimi ndo nahangaika kumtafuta hewani, nilitembelea kwake suala la unyumba likawa la kusua sua hadi nikaanza kuwakumbuka michepuko yangu.
Sasa wakuu naombeni ushauri niishi style gani ili nisiweze kupoteza furaha yangu na nisiwe na muda tena wa kumuwaza waza huyu mwanamke na hata ile hali ya kumtafuta tafuta hewani ipotee.
Nifanyaje nisaidieni manake kila siku naona mimi ndo nahangaika juu yake halafu mwenzangu anaonekana hajali mawasiliano yangu .
Msaada tafadhali.
Kama mada inavyojieleza,
Miaka ya karibuni hasa kuanzia 2015 mwishoni nimekua mtu nisiyekua na furaha na nikiwa na furaha basi ndani ya siku chache huondoka
labda nieleze kinagaubaga jinsi maisha yangu yalivyo.
Wazazi wangu washafariki almost 16 years ago, tangu wakati huo ndugu ambao nilikua nawategemea wakaanza mizinguo so nikaanza kuishi ghetto tangu nipo form 1 hadi namaliza form 4, then nikachaguliwa kuingia advance so kipindi chote nasoma advance likizo zangu karibia zote zikiishia maghettoni kwa masela kwa sababu kule home sikua na watu ambao wa kuwategemea sana.
Ada nilikua nalipiwa tu na msamaria mwema mmoja.Nimemaliza form 6 nikafaulu kwenda chuo na Mungu si athumani nikapata mkopo kwa 90% nikaanza maisha ya chuo pale SUA, baada ya muda nikaamua kutoka hostel nikapanga ghetto maisha yakaendelea.
Wakati huu nikiri kwamba nilikua mtu mwenye furaha muda wote sikua mtu wa mawazo mawazo. Mwaka 2012 nikakutana na mwanamke barabarani pale mjini Moro yupo na mabahasha yake anatafuta kazi nikamwomba namba, nikaanza kumtongoza mtoto akakubali tukawa wapenzi.
Baada ya muda binti kapata ujauzito nikamwambia atoke kwao (kwa mama mdogo wake) nikaishi nae ghetto kwa amani na upendo. Wakati ana mimba akaitwa interview akapiga fresh, akarudi ghetto, maisha yakaendelea ya furaha, amani na upendo, binti kajifungua salama salimini.
Kumbukeni wakati ana ujauzito nilimfungulia biashara ndogo
baada ya mtoto kutimiza kama miezi 4 hivi mama yake akapata kazi kule alikofanya interview tena kwa mshahara mnono zaidi ya ule wa aupatae mwenye degree. Nikauza baadhi ya vitu vyangu mama na mtoto na ndugu yake wakasafiri hadi kituo cha kazi alichopangiwa.
Wakati huo mimi nishamaliza degree yangu nikaingia rasmi kitaa, kama mnavyojua nchi yetu ina changamoto za ajira, hapo ndo suala la kutokua na furaha likaanza. Nikasafiri hadi kwa mama mtoto nikakaa kwa muda then nikaingia mkoa jirani huku huku lake zone kutafuta mishe nikapata nikaanza kazi na nikapanga chumba, mwisho wa siku ikawa mtihani kulipwa basi kazi ikashindikana nikaondoka kurudi kwa mama mtoto.
Nimekaa kwa mama mtoto mwisho wa siku tukashauriane nikasome inshu ya ualimu ili nikimaliza niajiriwe moja kwa moja tusaidiane maisha. Nikaingia kusoma PGDE ile namaliza tu kusubiri ajira akaingia Rais Magufuli na roho yake mbaya akasitisha ajira za walimu hasa wa arts.
Nikaanza mdogo tena na hali ya kukosa furaha na msongo wa mawazo ikaanza upya, nikaona kukaa kwa mwanamke bila kazi ni noma nikaingia mkoa jirani tena kutafuta mishe nikapata chuo kufundisha, nikaanza maisha.
Sasa kitu kinachoniumiza na kutokua na furaha ni huyu mwenzangu yani sasa hivi naona mapenzi yamepungua sana, mawasiliano ni ya shida yani nisipomtafutaga hewani basi hana muda mimi japo ananisaidia kwa baadhi ya mambo manake mwenzangu ana kipato cha juu sana, lakini naona kunipa ile heshima na kunijali kama mzazi mwenzake haipo.
Nampenda ila anavyonipotezeaga nahisi kutengwa na walimwengu wote,
tangu mwaka Jana sina furaha na nakuwa na msongo wa mawazo ,nilitegemea huyu mwenzangu awe mtu wa kunitia moyo kunifariji katika mihangaiko yangu lakini hilo halipo hata kama ananisaidia lakini hanipi ile heshima yangu kama mwanaume hata kama sina hela naona kwangu ni sawa na bure.
Daily Mimi ndo nahangaika kumtafuta hewani, nilitembelea kwake suala la unyumba likawa la kusua sua hadi nikaanza kuwakumbuka michepuko yangu.
Sasa wakuu naombeni ushauri niishi style gani ili nisiweze kupoteza furaha yangu na nisiwe na muda tena wa kumuwaza waza huyu mwanamke na hata ile hali ya kumtafuta tafuta hewani ipotee.
Nifanyaje nisaidieni manake kila siku naona mimi ndo nahangaika juu yake halafu mwenzangu anaonekana hajali mawasiliano yangu .
Msaada tafadhali.