Msaada: Namna ya kufika mji mpya wa serikali (Mtumba) jijini Dodoma

ISLETS

JF-Expert Member
Dec 29, 2012
8,121
5,332
Heshima kwenu.

Kwa wenyeji wa Dodoma, mgeni nipo hapa. Naomba kufahamiswa namna ya kufika mji mpya wa serikali - Mtumba kutokea maeneo ya Sabasaba hapa, kujua umbali na aina ya usafiri ulio rahisi kufika.

Pia nauliza kama Wizara zote zimehamia hayo maeneo au bado kuna Wizara zinafanyia kazi UDOM?

Mgeni wenu nipo siku ya 4 leo, jiji limekuwa busy na kasi sana katika ukuaji, hongereni.
 
Shukrani mkuu. Hivi chamwino ni wilaya nyingine kabisa kutoka hapa mjini au mtu unaweza kwenda na kurudi siku hiyohiyo?
Panda magari ya Chamwino...shuka mji wa Serikali ,ukifika hapo jiongeze ....kuwa makini,unaweza kuta Wizara nyingine huko Zina PS wa Waziri,Km na Wakurugenzi 2,3...!
Lazima ujue unafuata issue gani Wizarani...ndio ujue uende Mtumba au la
 
Huku panakoitwa mji wa serikali pako ukiwa kweli kweli, hakuna huduma za kijamii.
Bado ziara inaendelea.
 
Back
Top Bottom