kambagasa
JF-Expert Member
- Aug 18, 2014
- 2,241
- 1,748
Ndugu zangu jana nilipata wageni saba (viongozi wa serikali za mitaa) wakitaka mazungumzo ya faraga na mimi. Naomba nisitaje maeneo wanayotoka kwa sababu maalumu lakini baada ya kuwasikiliza kwa makini hata mimi nimeamua kuwasaidia kwa njia hii baada ya kuwaambia sina uzoefu na sijawahi kuwaza jambo kama hili.
Ndugu zangu pasipo kujali vyama vyetu vya siasa kama walivyokuja wao (UKAWA na CCM) wameomba niwasaidie namna watakavyopata nafasi ya kumuona raisi wa nchi hii Mh. Dr. John Pombe Magufuli ikulu Dar es salaam au popote atakapokuwa baada ya jitihada zao za kupatiwa ufumbuzi ngazi ya wilaya kukwama (kuahidiwa pasipo kutekelezewa).
Jumla yao wako kumi na saba (17) na kiini cha ombi lao ni kwenda kumweleza raisi wakiwa na ushahidi uliokamilika namna viongozi wa Kitanzania walioko MGODINI.............. wanavyowakandamiza jamii ya eneo la mgodi huo kwa kutoa rushwa kubwa kubwa kwa baadhi ya viongozi wa wilaya pia wakiingiza makampuni yao mgodini pasipo kuisaidia jamii hata vyumba vya madarasa. Wamewataja mameneja wakuu na makampuni yao (sitawataja hapa) na namna ambavyo wamekuwa wanawakomoa wananchi mara tu raisi alipotoa tamko la kuyataka makampuni yanayochimba dhahabu nchini kuinufaisha jamii INAYOZUNGUKA mgodi na makampuni madogomadogo yaliyoko katika migodi yatokane na jamii inayozunguka migodi hii.
Wenyeviti walienda mbali sana kwa kutoa mifano ambayo ina uhalisia wa wazi. Mmoja wao alisema hata wafanyakazi wanaoajiliwa mgodini asilimia 90% hawatoki maeneo ya vijiji hivi isipokuwa huletwa kwa kujuana, ukabila na rushwa kulingana na kazi unayoomba na mshahara wake na kazi hii huratibiwa kwa umakini na kitengo cha HR.
Ndugu zangu nikiyaandika yote hapa waliyonipatia kwa kopi ambayo wameiandaa kumpa raisi nafahamu sitakuwa salama maana wametaja hadi kampuni moja ina uhusiano na mke kati ya maraisi wetu waliostaafu wakishirikiana na mbuge mmoja mwenye makazi yake Dar ambapo kazi ya kampuni hii hata wao jamii wanaweza kuifanya kwa kuingia makubaliano na kampuni yenye utaalamu huo maana vifaa vyote viko hapo mgodini na ni bure.
Ndugu zangu pasipo kujali vyama vyetu vya siasa kama walivyokuja wao (UKAWA na CCM) wameomba niwasaidie namna watakavyopata nafasi ya kumuona raisi wa nchi hii Mh. Dr. John Pombe Magufuli ikulu Dar es salaam au popote atakapokuwa baada ya jitihada zao za kupatiwa ufumbuzi ngazi ya wilaya kukwama (kuahidiwa pasipo kutekelezewa).
Jumla yao wako kumi na saba (17) na kiini cha ombi lao ni kwenda kumweleza raisi wakiwa na ushahidi uliokamilika namna viongozi wa Kitanzania walioko MGODINI.............. wanavyowakandamiza jamii ya eneo la mgodi huo kwa kutoa rushwa kubwa kubwa kwa baadhi ya viongozi wa wilaya pia wakiingiza makampuni yao mgodini pasipo kuisaidia jamii hata vyumba vya madarasa. Wamewataja mameneja wakuu na makampuni yao (sitawataja hapa) na namna ambavyo wamekuwa wanawakomoa wananchi mara tu raisi alipotoa tamko la kuyataka makampuni yanayochimba dhahabu nchini kuinufaisha jamii INAYOZUNGUKA mgodi na makampuni madogomadogo yaliyoko katika migodi yatokane na jamii inayozunguka migodi hii.
Wenyeviti walienda mbali sana kwa kutoa mifano ambayo ina uhalisia wa wazi. Mmoja wao alisema hata wafanyakazi wanaoajiliwa mgodini asilimia 90% hawatoki maeneo ya vijiji hivi isipokuwa huletwa kwa kujuana, ukabila na rushwa kulingana na kazi unayoomba na mshahara wake na kazi hii huratibiwa kwa umakini na kitengo cha HR.
Ndugu zangu nikiyaandika yote hapa waliyonipatia kwa kopi ambayo wameiandaa kumpa raisi nafahamu sitakuwa salama maana wametaja hadi kampuni moja ina uhusiano na mke kati ya maraisi wetu waliostaafu wakishirikiana na mbuge mmoja mwenye makazi yake Dar ambapo kazi ya kampuni hii hata wao jamii wanaweza kuifanya kwa kuingia makubaliano na kampuni yenye utaalamu huo maana vifaa vyote viko hapo mgodini na ni bure.