Priscallia
JF-Expert Member
- Nov 9, 2019
- 495
- 2,427
Kama kuna mwanafunzi anayesoma Chuo cha Mipango Dodoma ama mtumishi wa hicho chuo ama mzazi mwenye mtoto anayesoma hapo naomba anithibitishie hili kuna mdogo wetu namlipia ada katika chuo taja hapo juu kozi ya “Bachelor Degree in Human Resource Planning and Management (BDHRPM).
Sasa jumamosi hii nilikuwa katika huo mji mkuu wa serikali nikasema nimpigie simu ili nipate kumkaribisha mahali apate chakula cha mchana na jioni kupokea hakutaka ila akanitext kwamba ana emergence kasafiri kaenda wilaya ya jirani kwa field? na sehemu alipo hakuna network nzuri bora tuwasiliane kwa text.
Alivyotaja FIELD akili yangu ikagutuka kidogo maana miaka yetu field huwa tunafanya mwishoni mwa semester, kengele ikanijia kichwani huwenda huyu mdogo wetu ndio keshaanza kuitembea Tanzania na viunga vyake akiwa hapa dodoma pamoja na wabab wa watu.
Na isitoshe huyu mdogo wetu tunatumia gharama nyingi kumsomesha kwa kweli hata ile morali ya kujiachia nikiwa dodoma ikapotea maana nilikuwa na mawazo mengi kichwani moja wapo ni kuwa huwenda kuna kibaba cha mtu kimemsafirisha mkoani ukitegemea wiki ilikuwa na likizo ndefu kidogo takribani siku nne kupisha sikukuu ya pasaka.
Hivyo nimekuja humu ndani kupata ukweli, hasa ukitegemea JF imesheheni watu wa aina mbalimbali na katika nyaja tofouti tofouti huwenda wakawa na ABC,s kuhusiana na hiki chuo ni kweli hawa wanafunzi wa mipango wameanza field katikati ya masomo, ama huyu mdogo wetu ameamua kunidanganya kuficha uchafu anaofanya pindi akiwa chuo kwa kutoroka vipindi kwenda kufanya maovu mikoani huko.
Naomba nipate ukweli kama kweli wameanza ratiba ama laah.
Sasa jumamosi hii nilikuwa katika huo mji mkuu wa serikali nikasema nimpigie simu ili nipate kumkaribisha mahali apate chakula cha mchana na jioni kupokea hakutaka ila akanitext kwamba ana emergence kasafiri kaenda wilaya ya jirani kwa field? na sehemu alipo hakuna network nzuri bora tuwasiliane kwa text.
Alivyotaja FIELD akili yangu ikagutuka kidogo maana miaka yetu field huwa tunafanya mwishoni mwa semester, kengele ikanijia kichwani huwenda huyu mdogo wetu ndio keshaanza kuitembea Tanzania na viunga vyake akiwa hapa dodoma pamoja na wabab wa watu.
Na isitoshe huyu mdogo wetu tunatumia gharama nyingi kumsomesha kwa kweli hata ile morali ya kujiachia nikiwa dodoma ikapotea maana nilikuwa na mawazo mengi kichwani moja wapo ni kuwa huwenda kuna kibaba cha mtu kimemsafirisha mkoani ukitegemea wiki ilikuwa na likizo ndefu kidogo takribani siku nne kupisha sikukuu ya pasaka.
Hivyo nimekuja humu ndani kupata ukweli, hasa ukitegemea JF imesheheni watu wa aina mbalimbali na katika nyaja tofouti tofouti huwenda wakawa na ABC,s kuhusiana na hiki chuo ni kweli hawa wanafunzi wa mipango wameanza field katikati ya masomo, ama huyu mdogo wetu ameamua kunidanganya kuficha uchafu anaofanya pindi akiwa chuo kwa kutoroka vipindi kwenda kufanya maovu mikoani huko.
Naomba nipate ukweli kama kweli wameanza ratiba ama laah.