Msaada: Mume wangu asipokunywa pombe, akimaliza kukojoa lazima matone madogo ya damu yatoke

okiwira

JF-Expert Member
Jul 23, 2018
2,787
2,853
Ni baba wa watoto 3 tangu ameoa amechepuka mara 4.

Kwa sasa ametulia kama miaka 2 bila kuchepuka.

Ila kuna tatizo ameliona yeye ni mnywaji wa konyagi na bingwa.

Akinywa pombe hizo halioni tatizo hilo ila asipokunywa analiona.

Shida ni nini hasa?

Asipokunywa siku tatu na kuendelea kila anapokojoa akimaliza mkojo lazima yatoke matone madogo ya damu.

Nini chanzo na tiba yake pia.

Msaada wenu.
 
Ni baba wa watoto 3 tangu ameoa amechepuka mara 4. Kwa sasa ametulia kama miaka 2 bila kuchepuka. Ila kuna tatizo ameliona yeye ni mnywaji wa konyagi na bingwa. Akinywa pombe hizo halioni tatizo hilo ila asipokunywa analiona. Shida ni nini hasa? Asipokunywa siku tatu na kuendelea kila anapokojoa akimaliza mkojo lazima yatoke matone madogo ya damu. Nini chanzo na tiba yake pia. Msaada wenu.
Aende hospitali, au ikimpendeza, Kawe kwa Mwamposa
 
Ni baba wa watoto 3 tangu ameoa amechepuka mara 4.

Kwa sasa ametulia kama miaka 2 bila kuchepuka...

Huu ni ushauri kwenu na watu wengine, sababu pekee ya kuja kuuliza hapa iwe ni uwezo wa kifedha!

Kama mtu ana issue swali Hospital akaangaliwe na kupata msaada, aibu na issue nyingine wont help, kuna wakati hatowezq ficha!

Kuchepuka mara 4 na hizo bla bla bla! Ni sound tu na irrelevant, inawezekana kachepuka jana usiku!
 
Ni baba wa watoto 3 tangu ameoa amechepuka mara 4.

Kwa sasa ametulia kama miaka 2 bila kuchepuka...
Naona ume Generalise sana, Hebu tueleze kwa kina, akikojoa wapi? Chooni au wakati wa Tendo la ndoa?
 
Fafanua upotoshaji wangu nami nielimike
Njia ya mkojo inahusiana na figo, ungesema figo zimeathirika hapo sawa, maana utumbo mpana umeunganima na njia ya haja kubwa na sio njia ya mkojo so hakuna sehemu mtu atapata madhara kwenye utumbo mkubwa na effect zake zionekane kwenye njia ya mkojo, haiwezekani.

Pia ini likiathirika effect zake haziwezi kuonekana kupitia njia ya mkojo (kwenye figo) bali dalili za ini kuharibika huwa kama tumbo kujaa (ascitice) na hepatitis so kwa maelezo yako hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa hivyo ulivyovitaja na mtu kukojoa damu.
 
Njia ya mkojo inahusiana na figo, ungesema figo zimeathirika hapo sawa, maana utumbo mpana umeunganima na njia ya haja kubwa na sio njia ya mkojo so hakuna sehemu mtu atapata madhara kwenye utumbo mkubwa na effect zake zionekane kwenye njia ya mkojo, haiwezekani.

Pia ini likiathirika effect zake haziwezi kuonekana kupitia njia ya mkojo (kwenye figo) bali dalili za ini kuharibika huwa kama tumbo kujaa (ascitice) na hepatitis so kwa maelezo yako hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa hivyo ulivyovitaja na mtu kukojoa damu.
Asante kwa elimu nimeelimika sasa....kumbe badala ya ini nilipaswa kuweka figo.. Kwa ufafanuzi huu NAFUTA post yangu
 
Konyagi na Bingwa, ila wanume saa zingine sijui lengo letu ni nini,inaonekana huyu jamaa ni hatari sana...!
 
Hizo konyagi, kuchepuka mara 4, sijui watoto watatu etc, ni bla bla!! Nenda ukamwone urologist na waweza kuta ni UTI Sugu au Kichocho tu!
 
Hizo konyagi, kuchepuka mara 4, sijui watoto watatu etc, ni bla bla!! Nenda ukamwone urologist na waweza kuta ni UTI Sugu au Kichocho tu!
Usiseme bla bla dogo.
Lazima atoe background kidogo ya mgonjwa ili mnapotoa ushauri mnakua na picha halisi.
 
Ni baba wa watoto 3 tangu ameoa amechepuka mara 4.

Kwa sasa ametulia kama miaka 2 bila kuchepuka.

Ila kuna tatizo ameliona yeye ni mnywaji wa konyagi na bingwa.

Akinywa pombe hizo halioni tatizo hilo ila asipokunywa analiona.

Shida ni nini hasa?

Asipokunywa siku tatu na kuendelea kila anapokojoa akimaliza mkojo lazima yatoke matone madogo ya damu.

Nini chanzo na tiba yake pia.

Msaada wenu.
Anaweza kuwa na kichocho nenda kapime hospitali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom