Msaada: Mtoto wa miezi 10 kupata choo kidogo kidogo mara nyingi kwa siku

JF Member

JF-Expert Member
Dec 14, 2014
7,354
9,606
Habari wana jamii,

Kuna ndugu yangu wa damu anasumbuliwa na tatizo la kinyesi kwa bintie wa miezi kumi.

Mtoto ana afya nzuri kabisa kila choo chake ndio tatizo.

Anjisaidia Mara kwa mara kidogo kidogo..ukizingatia anatumia pampas basi kwenye makalio kimeungua hadi kunatoa damu .
Ameshaenda hospital na amewaona madaktari Wa Watoto.. Ikiwemo muhimbili na aghakani.. Akapewa dawa za kupaka aina ya zincast.

Afanyeje? Maana mtoto analia muda wote kwa sababu ya maumivu.
 
Asante sana.
Vipi kuhusu choo cha Mara kwa Mara afu kidogo kidogo?
Apunguze kumlisha mtoto kila saa
ampe chakula kila baada ya mda flani na asimshindilie machakula mengi na wakati anaona mtoto ana puuu asimuhangaishe amuache apuu vyote Mara nyingi mtoto akipuu tuu alaf ukamsumbua au kumshtua anaacha kabisa anakuja tena Ku puu baadae
 
Tumia nepi, mlishe kwa muda maalumu siyo kila dakika hii itasaidia hata yeye hatajisaidia Mara kwa Mara, halafu kuwa makini akijisaidia uwahi kumsafisha na ujitahidi kumbadilisha kila akikojoa, mkojo huwa unatabia ya kutoa vidonda
 
Tumia nepi, mlishe kwa muda maalumu siyo kila dakika hii itasaidia hata yeye hatajisaidia Mara kwa Mara, halafu kuwa makini akijisaidia uwahi kumsafisha na ujitahidi kumbadilisha kila akikojoa, mkojo huwa unatabia ya kutoa vidonda
Asantee sana
 
Apunguze kumlisha mtoto kila saa
ampe chakula kila baada ya mda flani na asimshindilie machakula mengi na wakati anaona mtoto ana puuu asimuhangaishe amuache apuu vyote Mara nyingi mtoto akipuu tuu alaf ukamsumbua au kumshtua anaacha kabisa anakuja tena Ku puu baadae
Hata mkubwa
 
Ana aleji na pampers anazotumia, usimvalishe kwa muda atumie nepi, zincast ni nzuri sana aendelee kutumia.
pia akijisaidia usimfute na wipes tumia maji masafi na kitambaa kumsafisha
Tatizo wamama wengi siju hizi ni wavivu ajabu. Mtoto anakaa na diaper muda mrefu, akijisaidia wanamfuta na wipes ndo imetoka. Hii inawafa ya watoto kuungua makalio na kupata uti zisizoisha. Wamama badilikeni aisee. Valisheni watoto diaper pale kqenye ulazime, sio mtoto anashinda na diaper siku nzima, na hivi dada wa kazi ndo anaachiwa mtoto basi mtoto hata kama ka poo dada atasubiri amalize rundo la nguo aliloachiwa ndo akamsafishe mtoto. So bad
 
Habari wana jamii,

Kuna ndugu yangu wa damu anasumbuliwa na tatizo la kinyesi kwa bintie wa miezi kumi.

Mtoto ana afya nzuri kabisa kila choo chake ndio tatizo.

Anjisaidia Mara kwa mara kidogo kidogo..ukizingatia anatumia pampas basi kwenye makalio kimeungua hadi kunatoa damu .
Ameshaenda hospital na amewaona madaktari Wa Watoto.. Ikiwemo muhimbili na aghakani.. Akapewa dawa za kupaka aina ya zincast.

Afanyeje? Maana mtoto analia muda wote kwa sababu ya maumivu.
Sema tu ni mwanao wala sio wa ndugu yako
 
Apunguze kumlisha mtoto kila saa
ampe chakula kila baada ya mda flani na asimshindilie machakula mengi na wakati anaona mtoto ana puuu asimuhangaishe amuache apuu vyote Mara nyingi mtoto akipuu tuu alaf ukamsumbua au kumshtua anaacha kabisa anakuja tena Ku puu baadae
kupuu ndio nini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom