MSAADA: Mtoto kutoa mate kila mara!

teetotaller

JF-Expert Member
Dec 16, 2014
307
203
wasalaam,

Naombeni ufumbuzi wa tatizo la mtoto kutoa mate kila mara...Hapo awali niliambiwa kuwa akikua yatakata ila mpaka sasa nina wasi wasi maana mda unaenda sioni mabadiliko.

NB: Mtoto ana mwaka mmoja na miezi mitano
 
wasalaam,

Naombeni ufumbuzi wa tatizo la mtoto kutoa mate kila mara...Hapo awali niliambiwa kuwa akikua yatakata ila mpaka sasa nina wasi wasi maana mda unaenda sioni mabadiliko.

NB; Mtoto ana mwaka mmoja na miezi mitano
Mate ni kati ya body fluids, kumbuka kumpa maji anywe kila mara. Mengine muone daktari wa watoto
 
Mate ni kati ya body fluids, kumbuka kumpa maji anywe kila mara. Mengine muone daktari wa watoto
Niliwahi kumpeleka kwa dokta wa watoto alipokuwa ana miezi tisa, jibu alilonipa ni kuwa yataisha tu baada ya muda.
tatizo naona mda unaenda na bado hali ipo pale pale,
 
Niliwahi kumpeleka kwa dokta wa watoto alipokuwa ana miezi tisa, jibu alilonipa ni kuwa yataisha tu baada ya muda.
tatizo naona mda unaenda na bado hali ipo pale pale,
Ni kawaida mate kutoka kwa watoto lakini kama yanaendelea kutoka kadiri anavyokuwa hitilafu inakuwa kwenye ubongo. Nenda hospitali ya uhakika afanyiwe vipimo vya kueleweka.
 
Ok ni mwaka mmoja na miez iyo bado usiwe na kimuemue subiria mpaka afike miaka miwili ivi ndo uwe na wasiwas ..kwahuo umri mtoto anakua bado hana uwezo wa kuiongoza misuli ya mdomo wake nahata kumeza mate na ukizingatia nameno ndo yanachomoza.
 
asante mkuu, nitampeleka tena!!
Nilivyoona heading ya habari yako nikajua may be ni mtu wangu kafungua hii thread maana mtoto wangu naye ana umri huo huo na anatoka mate ingawa inapungua kadri siku zinavyoenda.... Juzi nilimpeleka hospital lugalo daktari akaniambia ni kawaida kwa watoto na wengine huenda mpaka miaka mitano.

Ingawa matatizo hutofautiana so ni bora na wewe ukacheki shida ni nini.

Swali, alivyokua na miezi 9 na sasa kiwango cha denda ni kile kile? Ni mchangamfu? Meno yake vipi?
 
Mpeleke hosptal, linaweza kuwa tatizo la kawaida mkuu au la anaweza kua tahira mwenye uchizi ndani yake
 
Nilivyoona heading ya habari yako nikajua may be ni mtu wangu kafungua hii thread maana mtoto wangu naye ana umri huo huo na anatoka mate ingawa inapungua kadri siku zinavyoenda.... Juzi nilimpeleka hospital lugalo daktari akaniambia ni kawaida kwa watoto na wengine huenda mpaka miaka mitano...
kiwango naweza sema kinapungua kwa kiasi kidogo! ndio maana nikawa na wasi wasi, ni mchangamfu sana, meno yake yapo sawa!
 
Mara nyingi watoto wanaozaliwa na matatizo ya akili huwezi kuwatambua mapema wengi hutambuliwa wakianza kutambaa au kujifunza kuongea.

Nenda naye hospitali za watoto mfano meta rufaa mbeya au popote zilipo hospitali za watoto specialist.
 
Nakupa hapa njia za asili kama upo Karibu na MTO wa au kama unaweza pata Samaki aina ya kambale akiwa mzimaaa yaaani yu hai mshike kichwa alafu kule mkian mlambishe mwanao ,au nunua maandazi nenda futia Yale mate kwa uchache kisha MPE mjomba ake huyo mwanao ale lakini asijue kama kuna kitu kimefanyika mtoto wako atapona hilo tatizo
 
Nakupa hapa njia za asili kama upo Karibu na MTO wa au kama unaweza pata Samaki aina ya kambale akiwa mzimaaa yaaani yu hai mshike kichwa alafu kule mkian mlambishe mwanao ,au nunua maandazi nenda futia Yale mate kwa uchache kisha MPE mjomba ake huyo mwanao ale lakini asijue kama kuna kitu kimefanyika mtoto wako atapona hilo tatizo
Hii Njia Noma Sana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom