Biashara ya Mbao na Miti: Fahamu Uendeshaji, Faida na Changamoto zake

Nitakutafuta mkuu kwenye hili bado natafuta Shamba huko Njombe kwa ajili ya Miti

Kama utakuwa mjini siku ya 09 feb 2013, njoo Lunch Time Hotel ukutane na jf wenzako wanaootesha miti huko unakotafuta wewe shamba.
 
Kama utakuwa mjini siku ya 09 feb 2013, njoo Lunch Time Hotel ukutane na jf wenzako wanaootesha miti huko unakotafuta wewe shamba.

Sitakuwa mjini ila naweza kuipanga hiyo safari nikaja kwa ajili hiyo najua wanaweza nisaidia kupata mashamba huko ntajitahidi ratiba zikikaa sawa.
 
Habarini za jioni waungwana, samahanini wakuu ninakusudia kuja kufanya biashara ya kununua na kusafirisha mbao toka makambako ama Njombe kwenda Dar.

Sina uzoefu na biashara hiyo naomba mwenye clue au aidia ya hii biashara anitupie kabla sijaanza.

Natumaini msaada toka kwenu.

Ahsanteni
 
Nakushauri peleka Mwanza inalipa zaidi kuliko DSM

Sijawahi kufanya biashara hii, ila kwa utafiti mdogo niliofanya huku hakuna misitu, kuna miti-miti na vichaka vya hapa na pale kitu kinacholepekea mbao kuletwa kutoka tabora!! Ila nadhani ukitoa Makambako itakua nzuri kwakua kuna miti mizuri kuliko ya unyamwezini kule ILA gharama za usafirishaji ndiyo shughuli ilipo, huku usukumani ni mbali sana ukitokea Makambako!!
 
Habarini za jioni waungwana, samahanini wakuu ninakusudia kuja kufanya biashara ya kununua na kusafirisha mbao toka makambako ama njombe kwenda Dar.

Sina uzoefu na biashara hiyo naomba mwenye clue au aidia ya hii biashara anitupie kabla sijaanza.

Natumaini msaada toka kwenu.
Ahsanteni

Ni vizuri pia ufahamu biashara ya mbao ni kati ka biashara zinazo ongoza kwa kupotezea watu hela hasa wageni kwenye hizo biashara. Kuwa tayari kupoteza kabla hujapata. Nalinganisha na gemstone kwa wanao anza.
 
Nashukuru kwa mchango wenu!!kuhusu biashara ya upandaji miti! Nimevutiwa na mchango wa kila mmoja!
 
KVM naona hii kazi uliinza muda mrefu kidogo, mimi binafsi naipenda sana hii biashara maana nilishawahi onja utamu wa pesa yake baada ya kuuza miti kidogo niliyopanda nikiwa sekondari. Nimefanikiwa kunua ekari 200 huko njombe najipanga kuanza kupanda january 2013 na 2014 ili mwaka 2022 niwe milionea sio kuanza kulalamikia mafao!
Nipo Iringa kama utakuwa tayari naomba tuwasiliane. Nina ekari 20 Kidabaga - Kilolo naona hazitoshi na huku bei kwa ekari moja imepanda sana. Nahitaji shamba huko Njombe.
 
Nipo Iringa kama utakuwa tayari naomba tuwasiliane. Nina ekari 20 Kidabaga - Kilolo naona hazitoshi na huku bei kwa ekari moja imepanda sana. Nahitaji shamba huko Njombe.

Kidabaga vijiji gani mkuu? Uko karibu na hawa New Forest kule Magome au Ng`ang`ange? Maeneo hayo bei iko juu sana sababu ya hawa NF. Jaribu kwenda Ng`ingula au Masisiwe, kule bado ardhi ipo, ila Lupilo bei iko juu sana.

Njombe mambo bado hayajaharibika sana. Wahi wahi.
 
Kidabaga vijiji gani mkuu? Uko karibu na hawa New Forest kule Magome au Ng`ang`ange? Maeneo hayo bei iko juu sana sababu ya hawa NF. Jaribu kwenda Ng`ingula au Masisiwe, kule bado ardhi ipo, ila Lupilo bei iko juu sana.

Njombe mambo bado hayajaharibika sana. Wahi wahi.

Ni katika vijiji vya Idete maeneo ya hao New Forest lakini kwa mbele.
 
KVM naona hii kazi uliinza muda mrefu kidogo, mimi binafsi naipenda sana hii biashara maana nilishawahi onja utamu wa pesa yake baada ya kuuza miti kidogo niliyopanda nikiwa sekondari. Nimefanikiwa kunua ekari 200 huko njombe najipanga kuanza kupanda january 2013 na 2014 ili mwaka 2022 niwe milionea sio kuanza kulalamikia mafao!

Eneoo la hekari 200 umepata kwa kiasi gani mkuu?
 
hii mitiki(teak) inachukua muda mrefu sana kuwa na bei nzuri ni ya miaka 15 na kuendelea, ila ukiwa unafanya thining ya shamba unaanza kuuza kuanzia miaka saba, na ina hela mti unaweza fika hadi milioni moja (wanatumia kwa nguzo za umeme, kujenga meli na fenicha za gharama), kuhusu mbegu sifahamu ila european union wanafadhili mradi huko kilombero nasikia tayari wana hekta 3000.
MIMI NIMEPANDA MITIKI LINDI ndo nimeanza, mbegu zinapatikana wakala wa mbegu za misitu, Morogoro (kihonda) barabara ya kwenda Dodoma.
 
MITIKI INAPANDWA SEHEMU ZENYE JOTO. Mikoa ya pwani yote LINDI, MTWARA, PWANI, TANGA, DAR, MORO, na mbegu zinauzwa WAKALA WA MBEGU ZA MISITU MOROGORO.
 
Naomba kuuliza hivi miti ukiwa unapanda kuna haja ya kufyeka pori au inapandwa tu humo humo mchanganyiko?
 
Bei ya mitiki ipoje kwa sasa? kwa mti mmoja wa miaka kama 10

Cjajua bei kwa kweli.

Nilifanya research ya matumizi yake, nikaambiwa ni floo za meli na meli ,pamoja na boti za kisasa, nguzo za umemenna baadhi ya vifaavya umeme kama vile radio na spika, kitu kingine niliambiwa ukiwa na shamba zuri miti ikifika miaka mitano, unaweza chukua mkopo bank, na shamba likawa dhamana.
+note this hii mikopo ni kwa miti ya MITIKI vs PINES
 
Back
Top Bottom