Msaada: Mnafanyaje mambo yenu yaende poa?

Mimi hii ndio naikataaga. Yaani kosa afanye babu yangu huko nyuma kabla sijazaliwa afu me mtu mwingine nibebe msalaba hapana kwa kweli. Huucni uonevu wa hali ya juu. Imagine me nifanye kosa afu mwanangu aje apate shida kisa eti mimi kuwa ni baba ake yeye ndo iwe shida na mahangaiko kwake. Sijui hii imekaaje
Wewe unaelewa nini kuhusu "laana"?
 
Keep on praying, wakati wako waja...

Hujasema mambo gani Ila? Stress kila kona how?

Mfanowe me siku hizi Nina vihasira vya hapa na pale, kuna muda naona Kama sijielewi 😁 Ila najua 7bu. Kichupa kimejaa sana... Hebu check na huko kwanza u boost akili.
Hiyo avatar ni wewe? Una dimpo zuri.
 
Wewe unaelewa nini kuhusu "laana"?
Ni nuio kwa mtu aliyekutendea mabaya ili naye apate dhara.
Nb Kama sijakutendea baya iweje nipate dhara. Mf mimi wa kizazi cha nne huku ambae sikuwepo na wala sikukutenda lolote.
A man is a result of what he thinketh. Naamini nilizaliwa kwa kucopy DNA sio madhambi ya watu. Kama mshahara wa dhambi ni mauti basi huyo babu yangu alipotea na hiyo laana siku ya kufa kwake. Afu eti me nizaliwe nayo.
 
Kwanza angalia ukoo wako Kuna mtu aliwahi kuwa na pesa ,..?

Kwenye familia yenu Kuna mtu alishawahi kutoboa ,kuwa na maisha mazuri ,biashara n.k..?


Siku zote maji hufuata mkondo,ndugu Kama umezaliwa kwenye familia masikini utaendelea kuwa masikini mpaka mwisho ....


Labda ije external push ,nje na famalia yenu ikuboost ,vinginevyo upo kwenye mkondo wa umasikini na huwezi chomoka walahi
 
Ni nuio kwa mtu aliyekutendea mabaya ili naye apate dhara.
Nb Kama sijakutendea baya iweje nipate dhara. Mf mimi wa kizazi cha nne huku ambae sikuwepo na wala sikukutenda lolote.
A man is a result of what he thinketh. Naamini nilizaliwa kwa kucopy DNA sio madhambi ya watu. Kama mshahara wa dhambi ni mauti basi huyo babu yangu alipotea na hiyo laana siku ya kufa kwake. Afu eti me nizaliwe nayo.
Hujawahi kusikia, "umelaaniwa wewe pamoja na uzao wako wote"? Yaani ukilaaniwa au kupewa laana ya namna hiyo basi ujue laana hiyo Haina kikomo! Aliyepewa atakufa lakini laana hiyo itaendelea kuwepo kwa kizazi chake! Bila external power ya kuvunja laana hiyo, itawatafuna mpaka mwisho wa Dunia!
 
Kwanza angalia ukoo wako Kuna mtu aliwahi kuwa na pesa ,..?

Kwenye familia yenu Kuna mtu alishawahi kutoboa ,kuwa na maisha mazuri ,biashara n.k..?


Siku zote maji hufuata mkondo,ndugu Kama umezaliwa kwenye familia masikini utaendelea kuwa masikini mpaka mwisho ....


Labda ije external push ,nje na famalia yenu ikuboost ,vinginevyo upo kwenye mkondo wa umasikini na huwezi chomoka walahi
Nimejiongelea binafsi na siyo ukoo au familia. Ni just kipindi hiki hali ni mbaya lakini siyo siku zote na sitaki kujinenea hvyo kwamba hali itakua hivi forever.

Pia, ukoo wetu watu wengi wanajiweza vizuri tu but again maisha yao hayanihusu naangalia maisha yangu.

My problem is I wanted to know how watu wanavyoboost uchumi wao kivyovyote vile. Kama kuhustle, nimehustle sana.
 
Jiamini 100%,

Muamini Mungu 100 %

Siyo kila ushauri ni wa kufuata,

Simama kama wewe,

Punguza starehe,

Achana na mahusiano kwa muda.

Stand with your own feet.
Hapa hujamshauri kitu, hebu tafakari ulichoshauri kama atakitendea kazi itakuwaje?
 
Hujawahi kusikia, "umelaaniwa wewe pamoja na uzao wako wote"? Yaani ukilaaniwa au kupewa laana ya namna hiyo basi ujue laana hiyo Haina kikomo! Aliyepewa atakufa lakini laana hiyo itaendelea kuwepo kwa kizazi chake! Bila external power ya kuvunja laana hiyo, itawatafuna mpaka mwisho wa Dunia!
Kwa nini asiyehusika na ambae hayupo apewe tabu hii??
 
Tunapigwa kweli, hatupewi asilimia zote, inawezekana tumepewa asilimia kumi tu, izo 90 inabidi kujitafutia
Sure mkuu kuna mtu hapo juu kamuelezea mtoa mada kuwa abadili mifumo ya mishe zake.
Ila hili la laana naamini kama nikikosea mm nalipwa mimi tu. Wengine hawaguswi.
 
Habari zenu,

Ndugu zangu, mnaombaje kwa Mungu mpaka mnapata baraka tele. Mimi binafsi kila ninachogusa mambo hayaendi, stress kila corner mpaka kuna wakati unatamani ujiwaishe tu mbinguni.

I am working really hard and sitamani kukataa tamaa zaidi.Naombeni ushauri huwa mnafanyaje fanyaje mambo yenu yaende poa.

Asante.
Je unajua kwamba kuna watu wengi sana hawafanyi kazi lakini wanaishi maisha ya kuwatumikisha wengine pasipo wao kujua kwamba wanatumikishwa? Yawezekana wewe ni mmoja wao unatumikishwa pasipo wewe kujua. Huhitaji kuamini ninachosema hata kama huamini mambo haya yapo sana kila siku na dawa yake ni kukaa vizuri na Mungu Aliye Hai.
 
Je unajua kwamba kuna watu wengi sana hawafanyi kazi lakini wanaishi maisha ya kuwatumikisha wengine pasipo wao kujua kwamba wanatumikishwa? Yawezekana wewe ni mmoja wao unatumikishwa pasipo wewe kujua. Huhitaji kuamini ninachosema hata kama huamini mambo haya yapo sana kila siku na dawa yake ni kukaa vizuri na Mungu Aliye Hai.
Amen
 
Upo kwenye redline ya kuchakazwa vibaya mno kama hautakua na msimamo + kuridhika na hali yako
 
Kichupa kimejaa.
Keep on praying, wakati wako waja...

Hujasema mambo gani Ila? Stress kila kona how?

Mfanowe me siku hizi Nina vihasira vya hapa na pale, kuna muda naona Kama sijielewi Ila najua 7bu. Kichupa kimejaa sana... Hebu check na huko kwanza u boost akili.
 
Tunakwenda kwa waganga na unachanganya na mafuta ya mwaiposa sometimes hivyo yaani Mambo yanakwenda
 
lady Jay

Pole sana dear,
Ukweli ni kwamba unayopitia ww ni wengi wanapitia,wamepitia na wataendelea kupitia.

Ni moja ya hatua muhimu maishani, kamwe usicomplain endelea kusali,endelea kuwa na imani na Mungu, Endelea kupiga kazi, Fanya kama unachopitia sasa kuwa ni maisha yako halisi yazoee. Ni kusali na kufanya kazi, haijalishi unapata au vipi?

Kamwe usiwe na hisia hasi kuhusu ww, Mungu ana makusudi yake. Wengi wamepitia hali yako tunachotofautiana ni ustahimilivu tu.

Kwa uzoefu wangu kuna neema kubwa inakuja mbele yako baada ya hii hali unayopitia. Zidisha kusali, Fanya kazi, Piga mazoezi, Pumzika, Relax kuna something big inakuja wala usiweke matarajio yeyote ww yazoee maisha ya sasa yafanye kuwa maisha yako ya kila siku.
 

Similar Discussions

16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom