MSAADA: laptop inawaka ila haitoi mwanga kwenye screen.

Fasouls

JF-Expert Member
Jun 24, 2011
939
316
Habari zenu.
Naomben msaada leo asubuhi nilivyoiwasha ikawaka ila haikutoa mwanga kwenye screen feni pia halizunguki...
 
Je ukiangalia kwa karibu unayaona maandishi kwa mbali? Kama maandashi yanaoneka kwa mbali sana hiyo itakuwa imeunguza circuit inayoendesha taa za screen. Hiyo circuit inaitwa display inveter au display switch.
 
Kwani ulifanya installation ya software.Manake kama graphic ya 32bit ukaweka kwenye 64bit haita display mpaka iwe compatible na bit ya comp.Yangu ndo hayo
 
Je ukiangalia kwa karibu unayaona maandishi kwa mbali? Kama maandashi yanaoneka kwa mbali sana hiyo itakuwa imeunguza circuit inayoendesha taa za screen. Hiyo circuit inaitwa display inveter au display switch.
Yani iko nyeusi kabsa haina mwanga hata kidog na wala haineshi kama inataka kuwaka halafu inazima
 
Kwani ulifanya installation ya software.Manake kama graphic ya 32bit ukaweka kwenye 64bit haita display mpaka iwe compatible na bit ya comp.Yangu ndo hayo

sijawahi kuifanyia hiyo kitu tangu ninunue
 
Umejuaje kama inawaka kama haitoi mwanga na feni haizunguki????? jaribu kutumia tochi
 
Mkuu umejaribu kucheck na ram kama iko lose? maana bila ram kufanya kazi vizuri huwezi kamwe kuiona Display.Check na adaptor yako na battery pia kama vyote viko connected fresh.
 
Hilo ni tatizo la kawaida sana, wala usipate shida mkuu. Hapo taa ya screen haiwaki, inaweza kuwa imeungua au imeharibika tu. Unachotakiwa kufanya ni kumuona fundi wa computer hardware, atafungua screen na kubadili hicho kitaa. Ikishindikana unaweza kununua screen nyingine, fundi ataipachika tu na utaendelea kupiga mzigo.
 
Habari zenu.
Naomben msaada leo asubuhi nilivyoiwasha ikawaka ila haikutoa mwanga kwenye screen feni pia halizunguki...

Kwa kuwa hujatoa inferences za moja kwa moja acha nijaribu jibu tokana na uzoefu wangu.

Hapo sababu zaweza kuwa kama ifuatavyo:

Kama screen haiwaki kabisa na kuonesha andishi hata moja tokea mwanzo ubonyezapo power button, then matatizo yaweza kuwa ni RAM imekufa, ama LCD display imekufa

Pia umezungumzia FAN kutozunguka, hilo ni tatizo jingine. FAN kazi yake ni kufanya mzunguko wa hewa katika circuit board na kupoza vifaa vilivyomo juu yake.

Kama nilivyotajwa hapo juu i.e RAM na display ni vizima na FAN pekee ndio haiwaki then ungeona laptop inawaka kwa dakika kadhaa na kuzima ikiwa njiani kufanya booting ya O.S. Hii ni sababu joto litapanda tokana na FAN kushindwa supply hewa ya kupoza motherboard na imedesigniwa temperature ikizidi kiwango fulan laptop ijizime ili kuondoa further damage including kuungua kwa on board equipments.

Na mwisho kabisa sababu ya kutowaka yawezekana motherboard yenyewe tayari imeshaungua baaadh ya equipmens zake. Na hivyo kuifanya laptop yako kutowaka kabisa.

Nadhan 90% tatizo linaweza kuwa ndani ya nilichokielezea. Jaribu kufanya trace na unaweza vumbua tatizo linaloisibu laptop yako.
 
Mkuu kwanza pole na matatizo, kama laptop yako ni aina ya hp ama compaq mara nyengine huwa wanaweka graphic card inaitwa nvidia na hii kitu haina maisha marefu ikichoka huwa inaleta matatizo kama haya na kutatuka inakua tabu sana hata hivyo itapona kwa muda mdogo tu tatizo litajirejea .

ushauri wangu kama itakua ni aina hizo ama itakua kabila nyengine na kuona hii graphic nvidia katika laptop yako ni lebo ndogo tu mfano kama lebo ya window ama vista ama 7 , usipoteze pesa zaidi . lakini inawezekana pia ram ama inverter zimekufa vitu ambavyo rahisi kubadilisha.

kila la heri mkuu.
 
Kwa kuwa hujatoa inferences za moja kwa moja acha nijaribu jibu tokana na uzoefu wangu.

Hapo sababu zaweza kuwa kama ifuatavyo:

Kama screen haiwaki kabisa na kuonesha andishi hata moja tokea mwanzo ubonyezapo power button, then matatizo yaweza kuwa ni RAM imekufa, ama LCD display imekufa

Pia umezungumzia FAN kutozunguka, hilo ni tatizo jingine. FAN kazi yake ni kufanya mzunguko wa hewa katika circuit board na kupoza vifaa vilivyomo juu yake.

Kama nilivyotajwa hapo juu i.e RAM na display ni vizima na FAN pekee ndio haiwaki then ungeona laptop inawaka kwa dakika kadhaa na kuzima ikiwa njiani kufanya booting ya O.S. Hii ni sababu joto litapanda tokana na FAN kushindwa supply hewa ya kupoza motherboard na imedesigniwa temperature ikizidi kiwango fulan laptop ijizime ili kuondoa further damage including kuungua kwa on board equipments.

Na mwisho kabisa sababu ya kutowaka yawezekana motherboard yenyewe tayari imeshaungua baaadh ya equipmens zake. Na hivyo kuifanya laptop yako kutowaka kabisa.

Nadhan 90% tatizo linaweza kuwa ndani ya nilichokielezea. Jaribu kufanya trace na unaweza vumbua tatizo linaloisibu laptop yako.
Samahani mkuu! Naomba kuuliza, ivi bahadhi ya vifaa vya motherboard vikiharibika suluhisho lake ni kubadili vifaa vilivyoaribika ama motherboard kiujumla?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom