Msaada kwa macho haya!

G M S

JF-Expert Member
Mar 30, 2011
502
53
Wajumbe naomba msaada kujua je kwa mtu mwenye macho mekundu kuna njia ya kuyafanya yawe meupe?
 
duuh... Una bibi shinyanga nini? Na mambo yanataka kuharibika wamezani naye ni m*h*w*i? Natania...
Wenye uelewa waje washushe somo.
 
Macho kuwa mekundu inaeza kuwa inflammation (conjuctivitis) ambayo mara nyingi inasababishwa na allergy au infection. Kabla ya kutumia eye whitening drops lazima ujue kuwamacho yako yanasababishwa na nini kuwa mekundu, kama ni allergy au infection.

Lakini kuna watu wengi tu huwa wanakuwa na macho mekundu bila kuwa na inflammation (allergy au infection), bali ni kuwa tu msukumo wa damu kwenye macho yao umekuwa mkubwa kutokana na mishipa midogo ya damu kwenye conjuctiva imepanuka (vasodilation, si ugonjwa). Hapa matibabu ni kutumia dawa zinazofanya mishipa hiyo ya damu kupungua/kubana (vasoconstriction) na hivyo macho kuwa meupe. Kuna dawa zinauzwa pharmacy zinaitwa 'eye whitening drops', ulizia dawa inaitwa 'systane' au 'visine'. Utakuwa unaweka kila unapoona macho yanakuwa mekundu.

NB: Hakikisha kuwa sio inflammation kwa kumuona daktari!
 
Back
Top Bottom