Msaada kupata/kusafirisha bidhaa kutoka Kenya

Bora ungetaja kabisa nini unataka kuagiza, maana kila kitu kina mfumo na mkakati wake. Kunazo hata hutumwa kwa Dar express hayo mabasi ya Dar to Nairobi.
Lakini uwe makini maana upande wa Tanzania wanatia viberiti hata vifaranga, japo umesema wazee wa ligi tukae pembeni ila ni muhimu kukumbushia tu, kale kachuki ka watu wenu katakupeleka hasara hadi utamani kujitoa uhai.
Alivojieleza nadhani anaongea kuhusu mzigo bulk, yaani mkubwa mno, kama sivyo nadhani umemuongezea option nyingine. Kuna watu hapa wamegeuza kabisa mada ya wenyewe.
 
Mkuu wasiliana na mkenya ambaye unanua bidhaa kutoka kwake ili ujue jinsi anavotaka kupokea hela zake. Ukifanya biashara yote hii kupitia benki kila kitu kitakuwa rahisi. Benki itakupa fomu muhimu ya Import Declaration ambayo humo ndani inaashiria aina ya bidhaa, malipo ambayo unatakiwa ulipie bidhaa zenyewe n.k, n.k. Equity huwa wako very fast na ukianza process yenyewe leo hii ikifika jioni watakuwa wametuma fomu yenyewe Dar kwa TISCAN, kampuni ya inspectors ya kitanzania ya kushughulikia imports za aina hizi. Ukisha wasiliana na TISCAN uanze shughuli ya kuzisafirisha kutoka Kenya. Upande wa Kenya hutapata stress nyingi. Utapata usaidizi wote na fomu zote sehemu moja, Huduma Centre iwe boda pale Sirare, Namanga au Nairobi na watakushauri kuhusu malipo yeyote ya ziada.

Shukran sana mkuu ngoja nifanyie kazi ushauri wako.
 
Nilitaka kumueleza afafanue zaidi kuhusu bidhaa anazotaka kusafirisha ila nikakumbuka hii ni Jf na hata mimi mwenyewe huwa sipendi kabisa kuanika shughuli zangu hadharani. Akianza shughuli yenyewe kama nilivomueleza hapo juu nadhani atafanikiwa bila stress nyingi.

Ni material fulani za kutengenezea plates kwa ajili ya printings, ni liquid ila zinauzwa kwa kg, hivo nataka kg kadhaa.
 
Dah! Leo umeniamulia sio bure. Hivi unatarajia mzalendo kama mimi nikalie fence kila mara ndio waniite tikiti maji kama Kalonzo Musyoka? Wakati mnaishambulia nchi yangu? Mijadala ya kutupiana vijembe huwa ina utamu wake wa kipekee ila chuki sina kabisa ndugu yangu. Alafu ukiendelea na hii offensive yako dhidi yangu ntaongea na mawakili wangu jombaa.
Haha unazungumzia mawakili, ngoja nikae pembeni sina hela ya fidia.

Lakini hapana, kama wewe unaleta mawakili, mimi naleta Nissan yeupe.
 
Naaaam! Mwanzi1 ongea na Bishop hapa akuelekeze hadi kwenye hiki kiwanda. Maanake ulivoamka na mguu wa kushoto leo naona ni kama hirizi zako zote ulizozivalia zimeisha betri. Zangu zinatumia solar.
Usicheze na sayansi yetu ya jadi. Hivi vibuyu hata mzungu hajuwi aanzie wapi Ku uncode.
 
Bora ungetaja kabisa nini unataka kuagiza, maana kila kitu kina mfumo na mkakati wake. Kunazo hata hutumwa kwa Dar express hayo mabasi ya Dar to Nairobi.
Lakini uwe makini maana upande wa Tanzania wanatia viberiti hata vifaranga, japo umesema wazee wa ligi tukae pembeni ila ni muhimu kukumbushia tu, kale kachuki ka watu wenu katakupeleka hasara hadi utamani kujitoa uhai.
Hii njia ya bus nayo ni nzuri, maana mzigo sio mkubwa.
 
Sio bulk kivile ni kama dumu ya 5 to 10 litres.
Ni material fulani za kutengenezea plates kwa ajili ya printings, ni liquid ila zinauzwa kwa kg, hivo nataka kg kadhaa.
Nilidhani ni mzigo wa tani moja kuenda juu. Basi usijipe stress kibao, MK254 amekushauri kuhusu Dar Express Couriers ama kampuni yeyote ile nyingine. Wasiliana nao kwanza jombaa, watakufanyia processing bila ya kukubidi kusafiri.
 
Haha unazungumzia mawakili, ngoja nikae pembeni sina hela ya fidia.

Lakini hapana, kama wewe unaleta mawakili, mimi naleta Nissan yeupe.
Labda ulete boda boda nyeupe, nissan nyeupe kabla inifikie huku mashinani Nkaimoronya maeneo ya Olemudimusirkon si nitakuwa tayari nishapashwa na intelligence yangu ya undercover moran? Teh teh! Huwa wanavalia kanzu kwahivyo huwezi wastukia.
 
Back
Top Bottom