Gama
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 13,266
- 4,716
Wana JF, nimekuwa nikitafakari juu ya majengo ya kilichokuwa chuo cha TANESCO kuporwa na kukabidhiwa kwa kikundi cha watu wachache. Ikumbukwe kuwa majengo haya yalikuwa ni mali ya walipakodi wote wa Tanzania sasa ni kwanini iwe sasa ni mali ya kikundi kimoja tu wakati watanzania wote wakiendelea kubeba mzigo wa kulipa madeni ya mashirika ya umma yaliyofirisika?, naleta ombi kwenu wana JF wenye uchungu na mali ya umma na wenye uelewa wa sheria wanisaidie niweze kufungua kesi mahakamani kudai mali hii irudishwe mikononi mwa walipakodi wa Tanzania. Nawasilisha.