Msaada kujua gharama ya kufyatua tofali 4,800

Watu mnabwabwaja tu ili muonekane wazee wa viwango, ni aidha mnaishi kwa shemeji hamjui kitu au lengo lenu ni kukatisha tamaa wenzenu!

Mfuko tofali 19!!!!

Mara tofali 25!!!

We unafikiri hiyo tofali ungeuziwa 1000-1200? Mpigaji angefanya biashara kichaa namna hiyo!

Tofali zote unazoona zinauzwa mtaani huko ni wastani wa zaidi ya 40 na kila siku unaona zinaondoka na maghorofa yanainuka... jipe muda kuwauliza wapigaji japo wanaweza wasikwambie ukweli.

Huu mjadala wa ujenzi upo juu ya uwezo wenu hivyo mlipaswa kuuamkia na kukaa kwa kutulia.

Mfuko wa simenti kwa tofali za ujenzi wa nyumba, 32.5R au 42.5R inatoa tofali 40-50 tena ni zenye ubora wa kiwango cha juu.

Na huyu ni mpigaji wa mikono, kwa mashine zinaweza kuzidi hapo na zikafaa tu.

Acheni ubishani na mizaha, hii ni moja ya sababu mnaogopa kujenga.
aina ya mchanga nayo ina tija sana kwenye wingi wa tofali mara nyingi sana ukitaka tofali bora kabisa kwa kanda za mikoa yenye maji chumvi yaana mikoa ya kanda ya kati na pwan pamoja na baadhi yanmikoa ya kanda ya ziwa angalau ukitumia 32.5R kwa mkono basi ili tofali Iwe bora basi anzia tofali 30-35 na kwa cement ya 42.5R basi tofali anzia 36 hadi 45 hizo ni za mkono hapo utapata tofali bora kabisa.

ila kwa ukanda wa nyanda za juu kusini yan mbeya huko na kaskazin ya arusha moshi huko basi cement ya 32.5R angalau tofali 36 hadi 50 na cement ya 42.5R angalau tofali 51 had 65 hapo utapata tofali bora kabisa

NB: Maelezo hayo ninkwa cement ambayo haijazidisha siku 6 hadi 10 tangu itoke kwenye mkanda. kadri inavyo zidi kukaa ndivyo na idadi ya tofali inavyo pungua
 
Umeandika uzi mrefu usiokuwa na faida. Kwa taarifa yako unaweza kufyatua tofali hata 20 kwa mfuko na zisiwe imara kama fundi hatozingatia ratio nzuri ya cement, compaction na umwagiliaji mzuri. Fundi mwingine anaweza kufyatua mpaka tofali 45 na zaidi zikawa imara kwa kuzingatia hayo mambo muhimu matatu
tofali zinataka vitu muhimu vifuatavyo ili kuliboresha
1. aina ya mchanga hapa zingatia mchanga wenye punje kubwa kubwa usiwe powdered sana
2. mchanganyiko mzuri wenye vipimo sahihi kati ya maji mchanga na cement
3.umwagiliaji maji ya kutosha baada ya tofali kufyatuliwa
ukizingatia hayo tofali litatoka imara kabisa.
 
Nipo mbeya mwezi huu nataka kufyatua tofari, mfyatuaji aliniambia ratio nzuri kwa cement ya 42.5 ni tofari 35,kutokana na huu uzi nitafanya research kidogo, namwambia afyatue tofali 40 kwa mfuko kwa mifuko 10 kwanza, napiga Maji ya kutosha afu nasimamia mwenyewe mwanzo mwisho nione ubora wa hilo tofari ukoje, tutaleta mrejesho humu
 
On a roughly but serious note:

Kwa hesabu ya tofali 45, kwa tofali 4800 utahitaji simenti mifuko takribani 110. Kwa bei ya 20,000/- kwa mfuko ni 2.2M.

Mchanga kila tripu ikupe tofali 200, utahitaji tripu 24... bei ya mfano ni 50,000/- kila hivyo itakula 1.2M.

Fundi wa kupiga tuseme utamlipa 150 hadi 200 kwa tofali, tuweke 800k.

Jumla kuu ni 2.2M+1.2M+800k = 4.2M.

Hapo bado maji, hatujui kama ni ya kulipia au niaje... na ishu ya kumwagilia hizo tofali sijui itakuwa kwako au kwa mpigaji!

Weka laki hapo ziada ihusishe huduma kama hizo.

Wakati huo, tofali zilizo tayari zinauzwa 1000 hadi 1200.... jumla 4.8M hadi 5.8M sijui kuhusu usafiri.

Piga hesabu utajua kiasi cha kuokoa hapo, na muda wako na usumbufu wa kusimamia na kuhakikisha kazi inafanyika kwa ubora.

Laki tano hadi milioni unaweza kuokoa.

Kumbuka mwaka huu sio wa kupata raha sana.
Asante kwa uchambuzi. Kumbe hakuna faida ni usumbufu wa bure
 
Ni vema tujifunze kufuata viwango (sisi sio wa kwanza kufyatua tofali, walishafyatuaga wenzetu huko miaka ya nyuma) ndio maana ikaonekana ni vema kuweka viwango katika kila kitu kinachofanyika, kwa mujibu wa Viwango(tukumbuke kila kitu kina kiwango chake kinachokubalika kimataifa, kikanda au hata kwa nchi), mfuko mmoja wa simenti unatakiwa kutoa tofali 25(hiki ndo kiwango kinachotumiwa na Serikali kwa sasa).

Hivyo, ukitoa tofali 25 -35 (kwa mfuko mmoja) ZITAKUWA IMARA, lakini tofali 45 kwa mfuko SISHAURI. Ukifyatua tofali mbovu bado hatuna teknolojia ya kurudisha mkanda nyuma Ili kuitumia sementi ileile kurekebisha makosa!!!!! Inakuwa hasara, labda uyatumie matofali hayo kama kifusi!
Mchanga unaweka ndoo ndogo ngapi?
 
Nipo mbeya mwezi huu nataka kufyatua tofari, mfyatuaji aliniambia ratio nzuri kwa cement ya 42.5 ni tofari 35,kutokana na huu uzi nitafanya research kidogo, namwambia afyatue tofali 40 kwa mfuko kwa mifuko 10 kwanza, napiga Maji ya kutosha afu nasimamia mwenyewe mwanzo mwisho nione ubora wa hilo tofari ukoje, tutaleta mrejesho humu
Mrejesho?
 
Ni vema tujifunze kufuata viwango (sisi sio wa kwanza kufyatua tofali, walishafyatuaga wenzetu huko miaka ya nyuma) ndio maana ikaonekana ni vema kuweka viwango katika kila kitu kinachofanyika, kwa mujibu wa Viwango(tukumbuke kila kitu kina kiwango chake kinachokubalika kimataifa, kikanda au hata kwa nchi), mfuko mmoja wa simenti unatakiwa kutoa tofali 25(hiki ndo kiwango kinachotumiwa na Serikali kwa sasa).

Hivyo, ukitoa tofali 25 -35 (kwa mfuko mmoja) ZITAKUWA IMARA, lakini tofali 45 kwa mfuko SISHAURI. Ukifyatua tofali mbovu bado hatuna teknolojia ya kurudisha mkanda nyuma Ili kuitumia sementi ileile kurekebisha makosa!!!!! Inakuwa hasara, labda uyatumie matofali hayo kama kifusi!
Tofali 45 kwa mfuko wa sement ya 42.5 standard ni sawa kabisa tena mafofali imara sana, issue hapo ni mchanga mzuri na kunyeshea maji ya kutosha basi, ubora wa tofali ni curing, mchanga bora na proper mixing basi,
 
Hizo tofali ni za fensi sio nyumba utanishukuru fanya tofali 40 kwa mfuko. Na inategemeana na aina ya mchanga kama una chumvi ama udongo utafanya chini yaa hapo.
Utapiga hesabu mwenyewe
Trip moja ya 4.5qm hufyatua mifuko 7
Kila mfuko hutoa tofali 40
Kufyatua ni 6000 kwa mfuko
Kumwagilia weka laki 1 hadi siku 10
 
Back
Top Bottom