careenjibebe
JF-Expert Member
- May 28, 2020
- 1,604
- 1,646
Kifupi jana nilikutana na kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 16 alikuwa anauza vitumbua kwa kutembeza. Katika mazungumzo nikagundua kijana yule ametoka mazingira magumu sana kiasi kwamba anasema hampendi kabisa mama yake kwa sababu alimuacha kwa baba yake akiwa mdogo na hajui alipoelekea mpaka leo.
Yeye alikuwa akiishi na kaka zake waliochangia baba kwa hiyo alikuwa akipigwa sana hali iliyosababisha atoroke nyumbani.
Sasa mimi nafikiri kumchukua na kumlea kama mwanangu lakini sijui nifanyaje kisheria ili isijeniletea tabu siku za baadae.
Naomba mwenye uzoefu na jambo hili kisheria au vinginevyo anipe ushauri ili nimnusuru yule mtoto.
Yeye alikuwa akiishi na kaka zake waliochangia baba kwa hiyo alikuwa akipigwa sana hali iliyosababisha atoroke nyumbani.
Sasa mimi nafikiri kumchukua na kumlea kama mwanangu lakini sijui nifanyaje kisheria ili isijeniletea tabu siku za baadae.
Naomba mwenye uzoefu na jambo hili kisheria au vinginevyo anipe ushauri ili nimnusuru yule mtoto.