Msaada kuhusu izi Intel hd

chuxxe

JF-Expert Member
Feb 4, 2019
600
361
Habari zenu wana jf Leo nilikuwa naomba kujuzwa kuusu izi Intel HD 3000, 4000 na zingne pia nimekuwa naangaika sana kuelewa maaana Intel HD 3000 nimeikuta kwenye core i3 na Intel hd 4000 nimeikuta kwenye core i3 pia hapa nilikuwa naomba kuelewa kitu wazee kuhusu izi Intel HD
 
dah umeniacha kidogo kaka embu nifafanulie vizuri hapo kwenye izo version
Kwenye computer kunakuwa na unit au unaweza kuiita chip au processor (GPU), inayoshughulika na video. Display ya computer au monitor inapata signal kutoka kwenye hiyo chip (GPU) ndipo inaonesha picha.

Kwa hiyo chochote kinachoonekana kwenye kioo cha computer kinatokea kwenye hiyo GPU.

Sasa kama vile tunaposema GPU ya computer yako inaweza kuwa labda ni INTEL au AMD au NVIDIA . Zote hizo zinatengenezwa na manufacture tofauti. Kwa hiyo ukisema INTEL inakuwa na model au version yake.

Ukisema AMD inakuwa na Model au version yake. Na Nvidia hivyo hiyo.

Kwa hiyo kwa upande wako hizo Intel HD 3000 na intel HD 4000 ni matoleo tofauti ya GPU ya INTEL.
 
Angalia nimeweka sample ya GPU screenshots hapa.
IMG_20200702_141319.jpg
IMG_20200702_141247.jpg
15936887158001460185636059381815.jpg
 
sorry lakin na vipi kwenye upande wa matumiz zinatofautiana? au ni HD tu ndio itakuwa tofauti
 
sorry lakin na vipi kwenye upande wa matumiz zinatofautiana? au ni HD tu ndio itakuwa tofauti
Zinatofautiana kwenye sifa zake (Specifications). Kama ifuatavyo.

- Resolution inayosapoti :
hapa ni katika ubora wa picha yaani unakuta GPU nyingine inaweza kuonyesha picha katika resolution ya 1024x600pixels na GPU nyingine inasaport 1080x768pixels au zaidi na hapa ndipo utakutana na HD, FHD, UHD.

- Memory:
Hapa unakuta GPU nyingine ina Memory ya 512MB na wakati nyingine inakuwa 2GB au zaidi.

-Refresh Rate:
Refresh rate inatofautiana kati ya GPU na GPU . Refresh rate kubwa ndio bora zaidi na pia inatakiwa display nayo ikubaliane na hiyo refresh rate.

Angalia hapo nimeweka properties za INTEL HD 520 ina total Memory ya 2112MB ~ 2GB.

Na hiyo nyingine Intel HD Graphics
Ina total Memory ya 1792MB ~ 1.7GB


Pia unaweza kuangalia hapo zote zimewekwa refresh rate ya 60Hz
JPEG_20200702_144458_909751864583039213.jpg
JPEG_20200702_144813_1407075110360045127.jpg
 
Habari zenu wana jf Leo nilikuwa naomba kujuzwa kuusu izi Intel HD 3000, 4000 na zingne pia nimekuwa naangaika sana kuelewa maaana Intel HD 3000 nimeikuta kwenye core i3 na Intel hd 4000 nimeikuta kwenye core i3 pia hapa nilikuwa naomba kuelewa kitu wazee kuhusu izi Intel HD
Kuongezea
HD 2500/3000 hio ni gen ya 2
Hd 4000 ni gen ya 3
Hd 4400/4600 ni gen ya 4
Hd 5500 ni gen ya 5
Hd 520/530 ni gen ya 6
Hd 620/630 imetumika kote kuanzia gen ya 7 mpaka ya 10.
Xe graphics zinakuja gen mpya baadae mwaka huu zina nguvu kama dedicated graphics.

Pia gen ya 10 zipo za aina mbili kuna comet lake inayotumia HD 620/630 na ice lake yenye gpu kali sema upatikanaji wa tabu.

Kwenye huo mtiririko jinsi gen ilivyo kubwa ndio jinsi hio intel HD inavyokuwa na nguvu kasoro gen ya 4 kwenda ya 5. Ya 4 ina nguvu kushinda ya 5.

Kwa matumizi ya kisasa angalau hd520 ama 620 zinakidhi, vitu kama video za 4k ama games zitacheza kwa low quality.

Ukikosa kabisa angalau hio hd4600
 
Kuongezea
HD 2500/3000 hio ni gen ya 2
Hd 4000 ni gen ya 3
Hd 4400/4600 ni gen ya 4
Hd 5500 ni gen ya 5
Hd 520/530 ni gen ya 6
Hd 620/630 imetumika kote kuanzia gen ya 7 mpaka ya 10.
Xe graphics zinakuja gen mpya baadae mwaka huu zina nguvu kama dedicated graphics.

Pia gen ya 10 zipo za aina mbili kuna comet lake inayotumia HD 620/630 na ice lake yenye gpu kali sema upatikanaji wa tabu.

Kwenye huo mtiririko jinsi gen ilivyo kubwa ndio jinsi hio intel HD inavyokuwa na nguvu kasoro gen ya 4 kwenda ya 5. Ya 4 ina nguvu kushinda ya 5.

Kwa matumizi ya kisasa angalau hd520 ama 620 zinakidhi, vitu kama video za 4k ama games zitacheza kwa low quality.

Ukikosa kabisa angalau hio hd4600
swali kidogo mkuu me natumia pentium g3250 hd 4000 Ila nikigoogle uwa naambia ni 4then
 
Back
Top Bottom