Msaada: Kufungua Mashine ya Kusaga na Kukoboa

Bavaria

JF-Expert Member
Jun 14, 2011
53,102
53,353
Habari wanaJF.
Naombeni msaada wenu, nataka nifungue mashine ya kukoboa na kusaga mahindi. Naombeni mnisaidie jumla ya gharama kwaajili ya kufanikisha hiyo shughuli. Inshort nataka kufungua kikampuni changu cha kusambaza sembe madukani ila nikiwa nasaga mimi mwenyewe.
Natanguliza shukrani za dhati.
 
Vitu vinavyohitajika kinu cha kukoboleya mahindi, kinu cha kusagia mahindi, motor mbili kwa ajili ya vinu hivyo. Kuna aina mbili ya vinu cha kwanza kinatengenezwa sido na cha pili kinatengenezwa mtaani kwa moter zipo za china na italy piya zipo za kusukwa mtaani bei ya kinu ni 1.2 million *2 na motor nayo ni kama 1.5 millioni *2 vinu na moter mkaanda, pulling, inaweza kufika kama millioni 7 hadi 8 mizani kubwa, eneo kwa ajili ya hiyo biashara, umeme 3 phase , leseni kutoka mamlaka ya chakula. Mahindi kwa sasa kg ni 750/= gunia 75000/= bei ya kiroba kwa ajili ya package ni 400 kwa kiroba, tani 10 inatowa viroba 270 hadi 280 vya sembe kg 25 tani 10 piya inatowa magunia 45 ya pumba umeme ni kama 150000/=, labour charges ni kama 100,000/= bei ya tani 10 ya mahindi kwa sasa ni 7,500,000/= kazi kwako kufanya hesabu kama inalipa au hapana
 
mkuu mimi ninauza vinu vyangu vyote 2 na motor zake 30 na 40hp na stater zake jumla tsh5m ni pm tufanye biashara!
 
vp kuhusu upatikanaji wa malighafi(mahindi),kwa aliyejianda ndani ya wiki moja tani 30 zinawezakupatikana?hii nikimaanisha bila kikomo.
 
Vitu vinavyohitajika kinu cha kukoboleya mahindi, kinu cha kusagia mahindi, motor mbili kwa ajili ya vinu hivyo. Kuna aina mbili ya vinu cha kwanza kinatengenezwa sido na cha pili kinatengenezwa mtaani kwa moter zipo za china na italy piya zipo za kusukwa mtaani bei ya kinu ni 1.2 million *2 na motor nayo ni kama 1.5 millioni *2 vinu na moter mkaanda, pulling, inaweza kufika kama millioni 7 hadi 8 mizani kubwa, eneo kwa ajili ya hiyo biashara, umeme 3 phase , leseni kutoka mamlaka ya chakula. Mahindi kwa sasa kg ni 750/= gunia 75000/= bei ya kiroba kwa ajili ya package ni 400 kwa kiroba, tani 10 inatowa viroba 270 hadi 280 vya sembe kg 25 tani 10 piya inatowa magunia 45 ya pumba umeme ni kama 150000/=, labour charges ni kama 100,000/= bei ya tani 10 ya mahindi kwa sasa ni 7,500,000/= kazi kwako kufanya hesabu kama inalipa au hapana

Hawa ndio aina ya wachaingiaji tunaowataka. safi sana. Sasa ndugu inaonekana unajua sana ungesema moja kwa moja kama biashara ina faida au la.
 
Habari wanaJF.
Naombeni msaada wenu, nataka nifungue mashine ya kukoboa na kusaga mahindi. Naombeni mnisaidie jumla ya gharama kwaajili ya kufanikisha hiyo shughuli. Inshort nataka kufungua kikampuni changu cha kusambaza sembe madukani ila nikiwa nasaga mimi mwenyewe.
Natanguliza shukrani za dhati.

POLE lakini naona huyo jamaa keshakujibu. haraka haraka zitahitajika si chini ya sh 7m. sasa inategemeana wewe umejiandaa na vitu gani sasa hivi, eneo, ardhi ,mifumo ya maji ,usafi umbali wa umeme, lakini pia unataka machine yenye ukubwa gani( ie power)
 
kuna kitu kimoja nilisahau hapo juu hii biashara ningumu sana kupata masoko ya cash watu wengi wanakopesha unga madukani then wanapita kukusanya hela baada ya siku kadha na ukilipwa inabidi umpatie mzigo mwingine, ANGALIZO USINUNUWE MACHINES ILIYOTUMIKA ITAKUSUMBUWA BIASHARA YA SASA NI USHINDANI USIWE NA KITU CHA ZAMANI AMBACHO KINAGHARAMA KUBWA YA MATENGENEZO KILA WAKATI UKIFUNGA MPYA UNAKUWA NA GHARAMA YA UMEME MAINTENANCE COST INAKUWA NDOGO SANA, MAHINDI MAZURI NI YA KITETO, KIBAIGWA, KONDOA, KUNA AINA MBILI ZA MAHINDI AINA YA KWANZA INATOWA UNGA MWENGI NA AINA YA PILI HATOWI UNGA MWENGI KUJUWA NI KUANGALIA UKUBWA WA MAHINDI MAKUBWA SIO MAZURI WAO WANAYAITA PANADOL MFANO MAHINDI YA SONGEA, RUKWA , IRINGA NA TANGA, PIYA BAADHI YA SEHEMU ZA DODOMA, KONDOA, NA KITETO
 
Vitu vinavyohitajika kinu cha kukoboleya mahindi, kinu cha kusagia mahindi, motor mbili kwa ajili ya vinu hivyo. Kuna aina mbili ya vinu cha kwanza kinatengenezwa sido na cha pili kinatengenezwa mtaani kwa moter zipo za china na italy piya zipo za kusukwa mtaani bei ya kinu ni 1.2 million *2 na motor nayo ni kama 1.5 millioni *2 vinu na moter mkaanda, pulling, inaweza kufika kama millioni 7 hadi 8 mizani kubwa, eneo kwa ajili ya hiyo biashara, umeme 3 phase , leseni kutoka mamlaka ya chakula. Mahindi kwa sasa kg ni 750/= gunia 75000/= bei ya kiroba kwa ajili ya package ni 400 kwa kiroba, tani 10 inatowa viroba 270 hadi 280 vya sembe kg 25 tani 10 piya inatowa magunia 45 ya pumba umeme ni kama 150000/=, labour charges ni kama 100,000/= bei ya tani 10 ya mahindi kwa sasa ni 7,500,000/= kazi kwako kufanya hesabu kama inalipa au hapana
Kwa mahesabu haya inaonekana hii biashara hailipi. Swali: hawa waliopo kwenye hii biashara wanapataje faida?
 
Kwa mahesabu haya inaonekana hii biashara hailipi. Swali: hawa waliopo kwenye hii biashara wanapataje faida?

Wanatumia vipimo feki wakati wa kununua au wananunua kwa bei ya chini sana huko mashambani au wanapunja ujazo ktk packing za product zao na option ya mwisho ni kukwepa kodi.
 
Ndg,,, naomba niulize kama kuna anauejua anisaidie.. Wapi naweza kupata mifuko ya jumla (viroba) vya kuweka mazao kama mahindi kwa bei ya chin kwa ajili ya kuuza?
 
Back
Top Bottom