Wanajamii, ninaomba msaada wa kueleweshwa kuhusu kodi iitwayo "Withholding" (Withholding Tax) kwenye nyumba za kupanga.Nimempangisha mtu kwenye nyumba yangu iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam - Tanzania. Tumekubaliana kuhusu kodi na kusainiana mkataba. Malipo aliyonipa ni pungufu na matarajio yangu, nilipomuuliza akasema amepunguza "withholding tax" ambayo atailipa TRA.Swali langu kwenu wanajamii;1. Ni nani anayepaswa kulipa hii kodi? I mean ni mwenye nyumba yeyote au kuna baadhi?2. Nisipolipa madhara ni nini? - asipolipa huyo mpangaji nani ataulizwa?3. Hii kodi ni asilimia ngapi ya kodi ya jengo?4. Hii kodi ni kwa baadhi ya maeneo au ni kila sehemu?Natanguliza asante kwa majibu yenu.