Msaada kisheria juu ya uuzaji na ununuzi wa nyumba

jperson

Member
May 12, 2019
98
158
SCENARIO
(A). Tuseme ni Ayuoub( ni mmliki wa nyumba) .
(S).Tuseme ni Salim ( mteja wa nyumba ya Ayoub 2014).
(P).Tuseme ni peter pia nae ni ( mteja wa nyumba ya ayoub 2019 ).


Ayoub ni mmliki wa nyumba ndani ya manisipa iliopo ndani ya jiji X .mwaka 2014 alipokea kiasi cha shilingi 5milion kwa njia ya simu.kama malipo ya awali ya mauziano ya nyumba yenye thamani ya 14.5 milionkutoka kwa Salim .baada ya mdaa wakaamua wakaandikishane kwa maandishi kama malipo ya awali.baada ya mda kupita na deni halijalipwa ayuob akawasiliana na Salim na kumuuliza kua amalizie deni au auuze ile nyumba? Salim akadai aiuze maana kwa wakati ule hakuwa na pesa..NB:yote haya peter ambae ni mnunuaji wa pili hakuyajua ameyajua baada ya mgogoro.

Mwaka 2019.ayoub akamuzia nyumba peter kwa kiasi cha shilingi 15milion.wakaandikishana tu kwa makaratasi, lkn baadae akaamua kuboresha mkataba wa mauziano kwa mwanasheria huku akiendelea kufatilia hati miliki.

Ilipofika 2020 salim akafungua kesi ya madai ya ardhi na katika kesi hiyo alimshinda ayoub. Baada ya kuja na forgery ya maabdish ya malipo yaliyosoma amelipa kiasi cha milion11 na kitu.baada ya ushindi salim akaenda kukaza hukumu baraza la ardhi la wilaya ambapo . Alipewa kibali cha kuenda kuvunja na kutoa vyombo vya peter katika hiyo nyumba.

SWALI:NAHITAJI KUJUA NI TARATIBU ZIPI HASWA ZA KISHERIA ZINAPASWA KUFWATWA NA PETER ILI APATE HAKI YAKE YA KISHERIA?

NB: ayoub muuzaji wa nyumba yuko upande wa peter.
 
Back
Top Bottom