Pseudomonas
Member
- Dec 9, 2011
- 45
- 126
Salam wakuu,
Juzi kuna mdau alianzisha uzi juu ya watu wenye kuhitaji ufafanuzi na usaidizi katika sheria ya ardhi sasa naona mods wamefuta/wamehamisha na siuoni tena ule uzi na niliuliza swali la msingi lenye kuhitaji ufafanuzi na kuna mdau alinijibu wakati nafungua uzi nikaambiwa invalid topic kwa hiyo ukiona swali limejirudia usichoke kutoa ufafanuzi tena.
Tatizo lenyewe ni kuna taasisi moja ya kidini ilimilikishwa eneo la ardhi zaidi ya hekari 300 ambapo maeneo hayo yalikua ni mashamba ya wananchi kwa shughuli za kilimo sasa kwa kuwa yalikua ni maeneo ya urithi wengi walipewa tu kifamilia bila nyaraka zozote na waliendelea na shughuli zao bila shida. Baada ya muda baadhi yao walitaka kuyaendeleza maeneo yao kwa shughuli za ujenzi hivyo kwenda ofisi za ardhi za wilaya kwa ajili ya kupata utaratibu wa kupimiwa maeneo hayo huko ndio walipokutana na janga. Walitaarifiwa kuwa maeneo hayo tayari kuna taasisi ilishapimiwa tangu mwaka 2007. Sasa maswali yakaja inawezekanaje watu maeneo yao apimiwe mtu mwingine na kumilikishwa bila mwenyekiti wa kitongoji, mtendaji kata au hata wao wamiliki wenyewe kuwa na taarifa? Kwa nini maeneo hayo ilipewa hiyo taasisi bila hata wahusika kuitwa kulipwa fidia?
Sheria ya ardhi kwa kesi kama hii inasemaje? Naomba ufafanuzi wajuvi wa sheria.
Juzi kuna mdau alianzisha uzi juu ya watu wenye kuhitaji ufafanuzi na usaidizi katika sheria ya ardhi sasa naona mods wamefuta/wamehamisha na siuoni tena ule uzi na niliuliza swali la msingi lenye kuhitaji ufafanuzi na kuna mdau alinijibu wakati nafungua uzi nikaambiwa invalid topic kwa hiyo ukiona swali limejirudia usichoke kutoa ufafanuzi tena.
Tatizo lenyewe ni kuna taasisi moja ya kidini ilimilikishwa eneo la ardhi zaidi ya hekari 300 ambapo maeneo hayo yalikua ni mashamba ya wananchi kwa shughuli za kilimo sasa kwa kuwa yalikua ni maeneo ya urithi wengi walipewa tu kifamilia bila nyaraka zozote na waliendelea na shughuli zao bila shida. Baada ya muda baadhi yao walitaka kuyaendeleza maeneo yao kwa shughuli za ujenzi hivyo kwenda ofisi za ardhi za wilaya kwa ajili ya kupata utaratibu wa kupimiwa maeneo hayo huko ndio walipokutana na janga. Walitaarifiwa kuwa maeneo hayo tayari kuna taasisi ilishapimiwa tangu mwaka 2007. Sasa maswali yakaja inawezekanaje watu maeneo yao apimiwe mtu mwingine na kumilikishwa bila mwenyekiti wa kitongoji, mtendaji kata au hata wao wamiliki wenyewe kuwa na taarifa? Kwa nini maeneo hayo ilipewa hiyo taasisi bila hata wahusika kuitwa kulipwa fidia?
Sheria ya ardhi kwa kesi kama hii inasemaje? Naomba ufafanuzi wajuvi wa sheria.