fkimwaga88
Member
- Dec 18, 2012
- 28
- 17
- Thread starter
- #21
Nashukuru kwa muda wako juu ya Jambo langu, hayo uliyataja nayajua yote, hesabu rahisi mfano umekopeshwa laki 1, utakatwa magarama ya bima na huduma ya mkopo Kama sh 9000/-,utalipwa kwa muda wa miezi 12 na Kila mwezi nilipe 10000/-, hivyo jumla ya hela yao ni 120000/-. Sasa unaambiwa uingize mkopo wa sh 125000/- kwa afisa utumishi.Mimi sijaelewa makato yanayozidi ni yapi? sababu kiasi ulichokopa na riba havijulikani huenda hata wewe pia huvijui.
niliwahi kuelimishwa kwamba unapoenda kukopa kwenye taasisi za kifedha kwa riba zingatia haya.
1. kiwango cha riba kinahimilika?
2. hiyo riba ni reducing balance
ama ni flat rate ?
katika kufuatilia, nilibaini benki nyingi riba zao ni flat rate.
wengi hayo hatuyajui tunaishia kuulizia riba ni kiasi gani na makato au marejesho kwa mwezi itakuwa kiasi gani basi! lakini katika mambo mengine maafisa wa benki hawatakwambia mfano bima ya mkopo na gharama ya kuandaa mkopo wako. Kumbuka fedha hizi zitakatwa kutoka kwenye mkopo wako ulioomba. kiwango utakachopewa hakitakuwa sawa na kiwango ulichoomba kukopeshwa lakini utarejesha kiwango ulichoomba kukopeshwa
Hivyo Basi, Kama Kila mwz ni 10000 nilipe kwa miez 12 nitalipa 120000/-. Hii sh 5000/- imetoka wapi? Kwani sikuiona wakati nasaini mkataba wa 120000/-?