Msaada juu ya godoro lipi ninunue

mavangah

Senior Member
Sep 9, 2015
113
23
Habar za muda huu wakuu na kheri ya mwaka mpya kwenu, naomba msaada wa kisayansi ,kimila au wauzoefu juu ya GODORO zuri la kununua kwa matumizi binafsi.

Mwaka huu umeaanza katika malengo niliyojiwekea makuu matano ya mwaka huu, moja wapo nikupata muda mzuri wa kupumzika ikiwa ni pamoja na kupata usingizi mwanana Kwajili ya afya ya mwili na akili.

Bila kupoteza wakati, nawasilisha hii mada :- Nahitaji kununua godoro zuri hivyo ni lipi chaguo zuri kati ya haya, COMFY, GODORO DODOMA,DODOMA HALISI, TANFORM ARUSHA, Na mengineyo Mnayoyafaham.......

Nawasilisha , size ni 5 kwa 6, bajet kati ya laki 130 - 300k.Shukran za dhat kwenu.
 
kutokana na kasi ya bwana yule,mimi nakushauri daka la sufi tu mkuu!
 
Nunua lenye bei kubwa kuliko mengine. Mfano ukikuta 5ft*6ft*10in ya kampuni tano tofauti nunua lenye bei kubwa zaidi
 
Natumia dodoma inch 12 5*6 …...nimenunua kiwandani keko 227,000 kko wanauza fake kuwa makin....ama yale yenye vitambaa wanakuwa wameunganisha pis mbili.....NB dodoma.haibonyei so n nzur kama unapenda kulala bila kubonyea bonyea ....
 
Lipi ni godoro bora kati ya Tanfoam na Vita Supreme? Mwenye uzoefu maana hapa natafuta godoro bora la kudumu muda mrefu.
 
Kiboko Dodoma

Mpaka unatamani uajiri panya walimalize haraka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom