MeruA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2017
- 1,391
- 2,125
Habarini za mchana ndugu zangu,kuna kijana wangu amechaguliwa kujiunga na shule ya Kamagi Sekondari, kidato cha tano (HGL) iliyoko wilaya ya Sikonge mkoani Tabora na kama mnavyojua mwezi ujao wanatakiwa kuripoti shuleni, nimefatilia matokeo yao siyo ya kuridhisha kabisa na hata mazingira pia mtoto naona kama hajavutiwa kabisa kwenda huko,nataka kumtafutia shule nyingine ya serikali hasahasa kanda ya ziwa Mwanza, Geita, Shinyanga.
Kwanini Kanda ya Ziwa?
Ana changamoto ya kiafya hivyo nataka awe mikoa ya karibu ili hata inapotokea dharura iwe rahisi kufika na kumpa msaada.
Taratibu za uhamisho kwa shule za kidato cha tano zipoje??
Naombeni msaada, Natanguliza shukrani zangu.
Kwanini Kanda ya Ziwa?
Ana changamoto ya kiafya hivyo nataka awe mikoa ya karibu ili hata inapotokea dharura iwe rahisi kufika na kumpa msaada.
Taratibu za uhamisho kwa shule za kidato cha tano zipoje??
Naombeni msaada, Natanguliza shukrani zangu.