Msaada: Jinsi ya Kumaster Manual Car!

Aman peaceful

Member
Mar 2, 2018
89
63
Ndugu wana JF.

Hivi karibuni nitaanza kujifunza kuendesha manual car! Msaada wenu tafadhali kwenye vitu muhimu vya kuzingatia hasa C-B-A (Clutch-Brake-Accelerator).

Nawasilisha.
 
Mkuu vipi automatic unaweza kuiendesha?unajifunzia chuo au mtaani? Kama ni chuo ukienda uko utapata maelekezo na mafunzo yote. Ila kama ni mtaani Tafuta dereva mzuri akufundishe na sehemu nzuri ya kujifunzia anzia kwenye kiwanja kikubwa kidogo kilicho wazi nikimaanisha kisiwe na miti mingi n.k. anza kwa kuzunguka uwanja huo mara nyingi kadri uwezavyo ukitembelea gia namba moja na mbili.

Ukizoea kuingiza gia bila kuangalia hapo unaweza kwenda hadi namba tatu ila muhimu tafuta dereva mzoefu wa manual akufundishe namna ya kubalance clutch na accelerator hasa wakati wa kuondoa gari kwenye mlima pia atakua anakusaidia kutambua makosa na kukurekebisha.

Ukishaiva uwanjani ingia barabara za mitaani zenye magari machache uanze kupata uzoefu ukijua manual ni raha sana.
 
manual haina ugumu wowote zaidi ya watu kuukuza... kuendesha gari ni mojawapo ya kazi rahisi sana duniani ndio maaana hata daktari au director, ceo anajiendesha na akifika hospitali au ofisini kwake anaanza fanya majukumu yake ya u ceo au udaktari
 
Mkuu vipi automatic unaweza kuiendesha?unajifunzia chuo au mtaani? Kama ni chuo ukienda uko utapata maelekezo na mafunzo yote. Ila kama ni mtaani Tafuta dereva mzuri akufundishe na sehemu nzuri ya kujifunzia anzia kwenye kiwanja kikubwa kidogo kilicho wazi nikimaanisha kisiwe na miti mingi n.k. anza kwa kuzunguka uwanja huo mara nyingi kadri uwezavyo ukitembelea gia namba moja na mbili...
Mkuu Asante sana kwa darasa hili maridhawa! automatic nimeshaiweza! ntajifunzia mtaani hiyo manual na ninashukur kwa mapendekezo yako!
 
manual haina ugumu wowote zaidi ya watu kuukuza... kuendesha gari ni mojawapo ya kazi rahisi sana duniani ndio maaana hata daktari au director, ceo anajiendesha na akifika hospitali au ofisini kwake anaanza fanya majukumu yake ya u ceo au udaktari
Shukran mkuu! taratibu nitaanza kujifunza!
 
Mkuu vipi automatic unaweza kuiendesha?unajifunzia chuo au mtaani? Kama ni chuo ukienda uko utapata maelekezo na mafunzo yote. Ila kama ni mtaani Tafuta dereva mzuri akufundishe na sehemu nzuri ya kujifunzia anzia kwenye kiwanja kikubwa kidogo kilicho wazi nikimaanisha kisiwe na miti mingi n.k. anza kwa kuzunguka uwanja huo mara nyingi kadri uwezavyo ukitembelea gia namba moja na mbili...
hapo kwenye timing ya gia mkuu ningependa kupata elimu zaidi!
 
Ndugu wana JF.
Hivi karibuni nitaanza kujifunza kuendesha manual car! Msaada wenu tafadhali kwenye vitu muhimu vya kuzingatia hasa C-B-A (Clutch-Brake-Accelerator).
Nawasilisha.
Kama unaweza kuendesha Automatic basi kwenye manual nenda kwenye miinuko sehemu ambapo ukiachia brake gari inarudi nyuma.Hapo jifunze kubalance brake,MOTO na clutch.
Usilazimishe kukalili jinsi ya kuondoka,KIKUBWA ISIKILIZE GARI INATAKA GEAR NO NGAPI.
Utazoea tu muda sio mrefu hata mlimani unasimama kwa kutumia clutch na moto bila brake.
 
Kama unaweza kuendesha Automatic basi kwenye manual nenda kwenye miinuko sehemu ambapo ukiachia brake gari inarudi nyuma.Hapo jifunze kubalance brake,MOTO na clutch.
Usilazimishe kukalili jinsi ya kuondoka,KIKUBWA ISIKILIZE GARI INATAKA GEAR NO NGAPI.
Utazoea tu muda sio mrefu hata mlimani unasimama kwa kutumia clutch na moto bila brake.
nitaleta mrejesho mkuu! asante!
 
Back
Top Bottom