Msaada jinsi ya Kubadili course chuo kikuu UDOM

Melxcom991

Member
Aug 2, 2021
48
25
Samahanini.kuna mdogo wang kachaguliaw UDOM course ya IT,anataka akajaribu kufanya transfer ya course kutoka course ya IT kwenda MD kweny matokeo yake ya form six ana D flat dvs 2 point 12,,,,je inawezekana???
 
Samahanini.kuna mdogo wang kachaguliaw UDOM course ya IT,anataka akajaribu kufanya transfer ya course kutoka course ya IT kwenda MD kweny matokeo yake ya form six ana D flat dvs 2 point 12,,,,je inawezekana???
Ushauri muache asome IT akisoma na kuweka juhudi zaidi kwa vitendo hatawahi kujutia uamuzi wa kubaki, anyway MD kwa matokeo ya DDD labda yaweza kuwa bahati yake
 
Hizi coz huwa zinawekwa kwa vigezo vya ufaulu wa chini, yaani walau mtu awe na principal pass, lakini wanapoomba, wanafunzi wengi huwa na ufaulu wa juu zaidi hivyo kupelekea vyuo vikuu kupandisha madaraja (cutting point) ya kuchukua wanafunzi kwa ufaulu walionao.

Na hapo si mwishow Bali pia TCU hutoa kibali Cha namba ya juu ya wanafunzi wanaotakiwa kudahiliwa kwa kozi husika, piga hesabu labda MD UDOM wanahitajika wanafunzi 400, na walionaufaulu kuanzia Dv 1 ya tatu mpaka Div. 1 ya Saba ni 800 kwa awamu zote zaudahili, na hapo Bado Kuna wanafunzi wa Diploma yako wenye GPA labda za 4.3 na kuendelea wanahitaji nafasi pia, kwa sifa za nduguyo hawezi pata nafasi hiyo UDOM, asijepoteza muda tu mpaka anakaa sawa ashamiss vipindi vingi kwa kozi alochaguliwa.

Kama mnauwezo kifedha na mmedhamilia asome MD.
Vyuo vikishafungua achukue admission letter ya UDOM aende nayo kwenye vyuo binafsi vinavyotoa MD, ( Kairuki na vinginevyo) na aombe kuhamia chuoni hapo kw kozi ya MD, na matumaini atapata maana ada yake ni ndefu ni watu wachache sana wanaweza kulipa ivyo unakuta Ile idadi ya kudahili walopewa na TCU Bado haijafikia
 
Vigezo vya MD hajakidhi, pitia vizuri guide book ya TCU. Hawezi soma MD kwa bongo labda nje.
 
MD MD MD, mwisho wa siku mnabakia kuwa maskini tu. Mtafute tajiri wa facebook muulize kwanini baba yake aliyekua Daktari aliamua kumpeleka yeye asomee computer science.
 
Admission capacity itakua imeshajaa na bora angekua ata na CCC kigogo wangemfikilia lakini kwa DDD flat ni ngumu kubadili hapo.
 
HAIWEZEKANI.

DDD hapati MD popote pale Tanzania sababu ya competition.

Mwacheni asome IT, akiweka juhudi atakuwa mtu mzito kama Chief-Mkwawa ambaye pia amesoma hapo hapo UDOM.
 
Atleast angekuwa na I.7 (PCB-CBB) wangemfikiria Ila kwa DDD ni ngumu. Vigezo vya MD-UDOM havipishani sana na MUHAS.

DDD Iliwekwa kama minimum requirement kwa ajili ya wale wanaoenda kusoma MD nje ya nchi.
Ili usome MD nje ya nchi ni lazma uwe na minimum requirement ya kusoma MD hapa nchini, so hii ni favour kwa ajili ya wanaoweza kwenda nje ya nchi.

Hautawahi skia mtu kasoma MD na DDD hapa Tanzania, never ever haitokaa Iwezekane, labda PCB, CBN & CBM wote wapate DDD.

Muandae dogo kisaikolojia apige IT, hiyo course ni nzuri sana akipambana.

Mcheki Chief-Mkwawa kwa ushauri zaidi.
 
HAIWEZEKANI.

DDD hapati MD popote pale Tanzania sababu ya competition.

Mwacheni asome IT, akiweka juhudi atakuwa mtu mzito kama Chief-Mkwawa ambaye pia amesoma hapo hapo UDOM.
Ni kweli mkuu ushindani ni mkubwa na sizani kama kuna mwenye DDD anasoma md kwa nchi hii
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom