Mzalendowadamu
JF-Expert Member
- Jul 10, 2016
- 218
- 318
Natoa salamu za heshima kwenu nyote wadau wa jukwaa hili pendwa. Mwaka 2016 niliomba ushauri humu na kusadiwa kuhusu kuagiza gari toka Japan na kufanikiwa kwa asilimia mia, nasema asanteni sana kwa mara nyingine.
Sasa nimerudi kwenu kuomba tena msaada wa ushauri wenu kuhusu namna ya kuagiza gari toka barani Ulaya. Lengo langu ni kununua gari la mizigo lenye uimara na ikiwezekana liwe na unafuu wa bei. Katika kuzungumza na wadau kadhaa hasa madereva wa haya magari makubwa ili kupata machache ya awali, wengi wao wamenishauri kununua Scania, Pia iwe ya kichwa kinachovuta trailer(wakimaanisha ndizo zinaweza kubeba mzigo mkubwa) na vilevile upatikanaji wa vipuri.
Ombi langu kwenu wanajukwaa hili ni hasa kujua Makampuni ya kuagizia gari hizi toka UK, pia kujua website ya makampuni hayo hasa yaliyo salama na fanisi ikiwezekana yenye mawakala hapa Tazania kama ilivyo kwa beforward. Kwa yeyote mwenye kujua lolote kuhusu gari gani ni imara au inayofaa kwa kazi za mizigo mizito kwa ubora wowote kuanzia uimara, matumizi ya mafuta na sifa zingine basi nawaomba sana mnitoe ujinga. Pia ningependa kujua namna ya kupata trailer imara kwa hapa Tazania.
Natagemea msaada wenu.
Asanteni sana na karibuni sana.
Sasa nimerudi kwenu kuomba tena msaada wa ushauri wenu kuhusu namna ya kuagiza gari toka barani Ulaya. Lengo langu ni kununua gari la mizigo lenye uimara na ikiwezekana liwe na unafuu wa bei. Katika kuzungumza na wadau kadhaa hasa madereva wa haya magari makubwa ili kupata machache ya awali, wengi wao wamenishauri kununua Scania, Pia iwe ya kichwa kinachovuta trailer(wakimaanisha ndizo zinaweza kubeba mzigo mkubwa) na vilevile upatikanaji wa vipuri.
Ombi langu kwenu wanajukwaa hili ni hasa kujua Makampuni ya kuagizia gari hizi toka UK, pia kujua website ya makampuni hayo hasa yaliyo salama na fanisi ikiwezekana yenye mawakala hapa Tazania kama ilivyo kwa beforward. Kwa yeyote mwenye kujua lolote kuhusu gari gani ni imara au inayofaa kwa kazi za mizigo mizito kwa ubora wowote kuanzia uimara, matumizi ya mafuta na sifa zingine basi nawaomba sana mnitoe ujinga. Pia ningependa kujua namna ya kupata trailer imara kwa hapa Tazania.
Natagemea msaada wenu.
Asanteni sana na karibuni sana.